picha

Kulaaniwa Bani Israil

Pamoja na kuteuliwa na Allah(s.

Kulaaniwa Bani Israil

Kulaaniwa Bani Israil


Pamoja na kuteuliwa na Allah(s.w) kuwa taifa bora kuliko mataifa yote ya wakati huo, Allah(s.w) aliwaghadhibikia Mayahudi na kuwalaani kutokana na matendo yao yafuatayo:

(i)Walikuwa ni wezi wa fadhila

- Allah(s.w) aliwatunukia neema mbali mbali ili wasimamishe
Ufalme wake katika ardhi na wamuabudu ipasavyo.

- Wengi wao walivitumia vipawa hivi kwa maslahi ya dunia na wakawa miongoni mwa wenye kuzama katika maasi.

- Baadhi ya neema walizotunukiwa Mayahudi zimeainishwa katika Qur-an - Rejea (2:47-53, 60, 122),(45:16-17).



(ii) Walipewa maonyo na mazingatio ili waache makosa na watengenee, lakini hawakuonyeka wala kuzingatia bali walikaidi na kuendelea kuzama katika kumuasi Allah(s.w). Rejea Qur-an (2:54-59, 61, 63-74), (5:71), (7:138-141).



(iii)Waliwakadhibisha na kuwaua Mitume wa Allah(s.w) bila ya haki.

"Kwa yakini Tulichukuwa ahadi ya wana wa Israili (Mayahudi kuwa watafuata), na Tukawapelekea Mitume. (Lakini) kila mara alipowafikia Mtume kwa yale zisiyoyapenda nafsi zao, wengine (katika Mitume hao) waliwakadhibisha, na wengine wakawaua (khasa)" (5:70).



(iv) Walivunja ahadi mbali mbali walizowekeana na Allah(s.w).
- Rejea Qur-an (2:83-86, 93, 100), (5:12-13, 70).



(v) Walikuwa na kibri na majivuno kuwa wao ni vipenzi vya Allah (s.w) na kwamba wataingia Peponi bila ya kufanya amali stahiki. Na ikitokea waingie Motoni watakaa muda mchache tu bila ya kujali uovu wanaoufanya:


"Na walisema: Hautatugusa Moto (wa Jahannamu) isipokuwa kwa siku chache tu. Sema: Je! mmepata ahadi kwa Mwenyezi Mungu kwa hivyo hatakhalifu ahadi yake? Au mnamsingizia Mwenyezi Mungu mambo msiyoyajua? (2:80).

- Pia rejea Qur-an (2:88, 91).



(vi) Wanazuoni wao walikuwa wakificha haki. Pia walikuwa wakichanganya haki na batili.

Mnatumaini (nyinyi Waislamu) ya kwamba watakuaminini (hao Mayahudi); na hali baadhi yao walikuwa wanasikia maneno ya Mwenyezi Mungu, kisha wanayabadili baada ya kuwa wameyafahamu; na hali wanajua? (2:75)

Wala msichanganye haki na batili, na mkaficha haki, na hali mnajua. (2:42)

- Pia rejea Qur-an (2:76-79).



(vii) Walibadili vitabu vya Allah(s.w) kwa kupunguza au kuongeza au kuondoa maneno au aya ili kuvuruga maana halisi ya kile kilichokusudiwa kwa maslahi yao binafsi kwa ajili ya dunia.



(viii) Walikuwa wakiwaamrisha watu kutenda mema ambayo wenyewe walikuwa hawafanyi.

Je! Mnawaamrisha watu kutenda mema na mnajisahau nafsi zenu, hali mnasoma kitabu (cha Mwenyezi Mungu kuwa kufanya hivyo ni vibaya)? Basi je, hamfahamu? (2:44)



(ix) Walikuwa wakitekeleza baadhi ya maamrisho ya Allah(s.w) na kukufuru baadhi. Yaani walikuwa wakifuata baadhi ya kitabu na kukufuru baadhi nyingine - Rejea Qur-an (2:85)



(x) Walikuwa wakila riba na kula mali za watu kwa batili - Qur-an (4:161).



(xi) Walikuwa hawaamrishi mema na kukataza mabaya - Qur-an (5:78-79)


(xii) Walikuwa wakifanya urafiki na makafiri - Qur-an (5:80). (xiii) Walipenda sana kuishi na walikuwa wakiogopa sana kufa kutokana na yale maovu iliyotanguliza mikono yao - Qur-an (2:96), (62:6-8).



(xiv) Waligawanyika katika makundi makundi mbali mbali, kila kundi likiwa dhidi ya lingine japo wote wanasoma kitabu kimoja. Qur'an inawaonya Waislamu juu ya hili katika aya zifuatazo:

Hakika wale waliofarikisha dini yao na wakawa makundi makundi, huna ukhusiano nao wowote. Bila shaka shauri yao (ya kuwaadhibu) iko kwa Mwenyezi Mungu; kisha (hapo wakati wa kuwaadhibu) atawaambia yale waliyokuwa wakitenda (6:159).

"Nyenyekeeni Kwake na mcheni, na simamisheni Sala, wala msiwe katika washirikina"
"Katika wale walioitenga Dini yao na wakawa makundi makundi; kila kikundi kinafurahia kilicho nacho" (30:31-32).



(xv) Waliofanya Viongozi wao Miungu Juu ya hili Qur'an inatufahamisha katika aya zifuatazo:


"Na Mayahudi wanasema: "Uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu;" na Wakristo wanasema: "Masihi ni mwana wa Mwenyezi Mungu;: haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasi na kuyapima). Wanayaiga maneno ya wale walio kufuru kabla yao,Mwenyezi Mungu awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa!" (9:30).


"Wamewafanya wanavyuoni wao na watawa wao kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu na (wamemfanya) Masihi mwana wa Maryamu (pia Mungu), hali hawakuamrishwa isipokuwa kumuabudu Mungu Mmoja, hakuna anayestahiki kuabudiwa kwa haki ila Yeye. Ametakasika na yale wanayomshirikisha nayo" (9:31).



(xvi) Walijenga hoja za visingizio.

Mayahudi walikatazwa kufanya kazi Jumamosi. Lakini baadhi yao waliasi ima kwa ujanjaujanja au kwa wazi wazi. Miongoni mwa waliokhalifu kwa unjanja ujanja ni wavuvi wa samaki. Walikuwa wakitega mitego yao Ijumaa jioni na kuchukua samaki Jumamosi jioni au Jumapili asubuhi ili ionekane kuwa Jumamosi hawakufanya kazi. Na wengine waliasi kwa kuleta visingizio kadhaa. Allah(s.w) aliye mjuzi wa nia zao aliwajua kuwa waliamua kumuasi na akawalipa adhabu ya kudhalilisha:

"Na kwa yakini mmekwisha kujua (khabari za) wale walioasi miongoni mwenu katika (amri ya kuihishimu) Jumamosi. Basi Tukawaambia: "Kuweni manyani wadhalilifu" (2:65).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1885

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰6 web hosting   

Post zinazofanana:

HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA

SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( Ω…Ω’).

Soma Zaidi...
Saratul-humaza

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa

Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya.

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya id-gham katika hukumu za tajwid

Hapa utajifunza kuhusu maana ya id-ghamu na aina zake.

Soma Zaidi...
HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushukasurat an Nasr

Sura hii ni katika sura za mwisho kushuka, huwendakuwa ndio ya mwisho kabisa. Masahaba waliamini kuwa sura hii imetabiri kifo cha Mtume S.A.W

Soma Zaidi...
Fadhila za kusoma surat al Imran

Post hii itakufundisha fadhila na faida za kusoma surat al Imran

Soma Zaidi...
Sababu za kshuka surat al Asr

Sura hii ni katika sura za kitawhidi sana. Maulamaa wanasema inatosha sura hii kuwa ni mawaidha. Imamu sharifu anasema kuwa sura hii inatosha kuwa muongozo…

Soma Zaidi...
Viraa saba na herufi saba katika usomaji wa quran

Ni zipi hizo herufi saba, na ni vipi viraa saba katika usomaji wa Quran

Soma Zaidi...