Sababu za kushuka kwa surat Al-Humazah

Zijuwe sababu kuu za kushuka surat Al-Humazah katika quran

<<<<<<< HEAD Sababu za kushuka kwa surat Al-Humazah

Surat Al-Humazah

SURAT ALHUMAZAH
Sura hii imeteremshwa Maka na ina aya 10 pamoja na bismillah.
Wafasiri wengi wanakubaliana ya kuwa sura hii ilishuka Makka. Hali ya watu wa siku za Mtume s.a.w. waliokuwa wakiwaudhi Waislamu na wakijivuna kwa mali zao, imeelezwa katika sura hii.



Humazah, "Msingiziaji." Neno hili limetoka katika neno hamazah lenye maana ya
kusingizia; kukoneka; kupiga kwa kidole; kusukumu; kupiga; kuuma; kusengenya; kuvunja; kutia wasiwasi.



Lumazah (Msingiziaji) ni neno lililotoka katika lamazah, yaani kusingizia, kuaibisha; na ku- koneka.



Masahaba na watu wa baadaye wamehitilafiana katika maana ya Aya hii, na hakuna sababu yake nyingine isipokuwa ya kwamba maneno haya mawili humazah na lumazah yanakaribiana sana katika maana. Inasemekana ya kuwa Mughira, A'as bin Wail na Sharik walikuwa wakishughulika kila mara kumwudhi Mtume s.a.w. na masahaba kwa kuwasingizia na kuwaaibisha; basi Mwenyezi Mungu katika sura hii akawaonya ya kuwa waache mwendo wao huo waila wataangamizwa.



Lakini hakuna haki ya kusema ya kuwa watu hawa watatu tu ndio walioonywa, maana
wangekuwa ni hao watatu tu, basi wangetajwa majina yao. Lakini badala ya kutajwa majina yao Mwenyezi Mungu amesema, Maangamizo kwa kila msingiziaji, msengenyaji. Hili laonyesha ya kuwa watu wote wenye ada na mwendo wa namna hiyo wameonywa - wawe watu wa zamani, wa leo, hata na wa baadaye - wote watapata adhabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa dhambi zao za kuwasingizia, kuwaaibisha, kuwasengenya na kuwateta watu. Hivyo, Mwenyezi Mungu amewaonya
watu wote wa siku zote ili wasishike njia ya namna hii inayoleta machafuko makubwa kati ya jamii za watu na makabila, na watu wanatenguka nguvu zao na kuangamia kabisa.




                   



======= Sababu za kushuka kwa surat Al-Humazah

Surat Al-Humazah

SURAT ALHUMAZAH
Sura hii imeteremshwa Maka na ina aya 10 pamoja na bismillah.
Wafasiri wengi wanakubaliana ya kuwa sura hii ilishuka Makka. Hali ya watu wa siku za Mtume s.a.w. waliokuwa wakiwaudhi Waislamu na wakijivuna kwa mali zao, imeelezwa katika sura hii.



Humazah, "Msingiziaji." Neno hili limetoka katika neno hamazah lenye maana ya
kusingizia; kukoneka; kupiga kwa kidole; kusukumu; kupiga; kuuma; kusengenya; kuvunja; kutia wasiwasi.



Lumazah (Msingiziaji) ni neno lililotoka katika lamazah, yaani kusingizia, kuaibisha; na ku- koneka.



Masahaba na watu wa baadaye wamehitilafiana katika maana ya Aya hii, na hakuna sababu yake nyingine isipokuwa ya kwamba maneno haya mawili humazah na lumazah yanakaribiana sana katika maana. Inasemekana ya kuwa Mughira, A'as bin Wail na Sharik walikuwa wakishughulika kila mara kumwudhi Mtume s.a.w. na masahaba kwa kuwasingizia na kuwaaibisha; basi Mwenyezi Mungu katika sura hii akawaonya ya kuwa waache mwendo wao huo waila wataangamizwa.



Lakini hakuna haki ya kusema ya kuwa watu hawa watatu tu ndio walioonywa, maana
wangekuwa ni hao watatu tu, basi wangetajwa majina yao. Lakini badala ya kutajwa majina yao Mwenyezi Mungu amesema, Maangamizo kwa kila msingiziaji, msengenyaji. Hili laonyesha ya kuwa watu wote wenye ada na mwendo wa namna hiyo wameonywa - wawe watu wa zamani, wa leo, hata na wa baadaye - wote watapata adhabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa dhambi zao za kuwasingizia, kuwaaibisha, kuwasengenya na kuwateta watu. Hivyo, Mwenyezi Mungu amewaonya
watu wote wa siku zote ili wasishike njia ya namna hii inayoleta machafuko makubwa kati ya jamii za watu na makabila, na watu wanatenguka nguvu zao na kuangamia kabisa.




                   



>>>>>>> origin/master

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1465

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 web hosting    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Kwa nini quran ilishuka kidogo kidogo?

Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Quraysh

Qurayh ni jina la kabila la Mtume Muhammad S.A.W. Sura hii itakwenda kukujulisha neema ambazo Maquraysh wamepewa na hawataoewa wao wowote baada ya wao.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA IDGHAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka Surat al Kafirun

Sura hii imekuja kukata rai ya Makafiri wa Makka kuhusu ibada ya ushirika. Hivi leo tungesema kuhusu dini mseto.

Soma Zaidi...
Saratul-humaza

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...