Sababu za kushuka surat al adiyat

Sababu za kushuka surat al adiyat

Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah.

Ibni Mas'ud, Jabir, Al-Hasan, Ikrama na Ataa wanasema ya kuwa sura hii ilishuka Makka.

 

Dhabhan ni namna  moja ya mbio za wanyama (Mufradat);  tena ni sauti maalumu inayotoka katika vifua  vya farasi wanapokimbia (Akrab). Wakimbiaji wanaotweta, mradi wa maneno haya ni farasi.

 

 Abdullah bin Abbas na wanazuoni wengine kama Mujahid, Ikrama, Ataa, Qatada na Dhahhaak wote  wanakubali ya kuwa mradi ni farasi.  Na lugha ya Kiarabu pia inasaidia maana hii.

 

Iliposhuka sura hii watu walikuwa na ngamia, na hakukuwa sana desturi ya kuwatumia farasi.  Lakini Mwenyezi Mungu kwa kuiteremsha Aya "Wakimbiaji wanaotweta" akabashiri ya kuwa hawa watu wa Makka  wapandao ngamia siku moja watakuwa wapandao farasi.  

 

Na kweli, baadaye desturi ya kuwapanda farasi ilienea sana, na farasi wakazidi kabisa, na Waislamu wakawa wakimbiaji juu ya farasi katika matukio ya vita na amani.  

 

Kwa neno zima, Aya hii inajulisha ya kuwa Waislamu walikuwa na shauku na huba sana ya kuitumikia dini, hata wakawabana maadui waliokuwa na nguvu nyingi na silaha kubwa.  Wao walikuwa wanakwenda mbio na wakiwakimbiza farasi kwa kutoa sadaka maisha yao. 

 

Sababu za kushuka sura hii: 

Muqatil amesema kuwa Mtume s.a. w Alituma jeshi liende kabila la bani Kinana na akamteua Mundhir bin Amr al Ansariy awe kama kiongozi wa jeshi hilo. 

 

Sasa muda mrefu umepita yapata mwezi habari za jeshi hili hazikufika Madina. Wanafiki wakaanza kutangaza kuwa wotevwaneuliwa. 

 

Hapo ndipo Allah akatoa taarifa za jeshi hili na kisha ikashuka sura hii. 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2559

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI
MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
quran na sayansi
quran na sayansi

2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio.

Soma Zaidi...
quran na tajwid
quran na tajwid

TAJWID Utangulizi wa elimu ya Tajwid YALIYOMO SURA YA 01 .

Soma Zaidi...
 Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum
Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum

SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s.

Soma Zaidi...
Tofauti kat ya sura za Maka na Madina
Tofauti kat ya sura za Maka na Madina

Sura za Makka na Madina Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka Surat al Kafirun
Sababu za kushuka Surat al Kafirun

Sura hii imekuja kukata rai ya Makafiri wa Makka kuhusu ibada ya ushirika. Hivi leo tungesema kuhusu dini mseto.

Soma Zaidi...
HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN
HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...