Sababu za kushuka surat al adiyat

Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah.

Ibni Mas'ud, Jabir, Al-Hasan, Ikrama na Ataa wanasema ya kuwa sura hii ilishuka Makka.

 

Dhabhan ni namna  moja ya mbio za wanyama (Mufradat);  tena ni sauti maalumu inayotoka katika vifua  vya farasi wanapokimbia (Akrab). Wakimbiaji wanaotweta, mradi wa maneno haya ni farasi.

 

 Abdullah bin Abbas na wanazuoni wengine kama Mujahid, Ikrama, Ataa, Qatada na Dhahhaak wote  wanakubali ya kuwa mradi ni farasi.  Na lugha ya Kiarabu pia inasaidia maana hii.

 

Iliposhuka sura hii watu walikuwa na ngamia, na hakukuwa sana desturi ya kuwatumia farasi.  Lakini Mwenyezi Mungu kwa kuiteremsha Aya "Wakimbiaji wanaotweta" akabashiri ya kuwa hawa watu wa Makka  wapandao ngamia siku moja watakuwa wapandao farasi.  

 

Na kweli, baadaye desturi ya kuwapanda farasi ilienea sana, na farasi wakazidi kabisa, na Waislamu wakawa wakimbiaji juu ya farasi katika matukio ya vita na amani.  

 

Kwa neno zima, Aya hii inajulisha ya kuwa Waislamu walikuwa na shauku na huba sana ya kuitumikia dini, hata wakawabana maadui waliokuwa na nguvu nyingi na silaha kubwa.  Wao walikuwa wanakwenda mbio na wakiwakimbiza farasi kwa kutoa sadaka maisha yao. 

 

Sababu za kushuka sura hii: 

Muqatil amesema kuwa Mtume s.a. w Alituma jeshi liende kabila la bani Kinana na akamteua Mundhir bin Amr al Ansariy awe kama kiongozi wa jeshi hilo. 

 

Sasa muda mrefu umepita yapata mwezi habari za jeshi hili hazikufika Madina. Wanafiki wakaanza kutangaza kuwa wotevwaneuliwa. 

 

Hapo ndipo Allah akatoa taarifa za jeshi hili na kisha ikashuka sura hii. 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021/11/29/Monday - 02:13:01 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1726


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuwapa wanaostahiki
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kwanini wengi wanaoswali hawafikii lengo la swala zao
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuamini siku ya mwisho
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu Soma Zaidi...

Nasaba ya Mtume Muhammad S.A.W na familia yake.
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 1 Soma Zaidi...

Maswali juu ya mtazamo wa uislamu kuhusu dini
Mtazamo wa uislamu kuhusu dini (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mtazamo wa makafiri juu ya dini
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Namna ya kuzuia dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji, ni mbinu mbalimbali ambazo utumika ili kujaribu kuepuka Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji. Soma Zaidi...

Zoezi la 5
Maswali mbalimbali kuhusu fiqih Soma Zaidi...