Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah.
Ibni Mas'ud, Jabir, Al-Hasan, Ikrama na Ataa wanasema ya kuwa sura hii ilishuka Makka.
Dhabhan ni namna moja ya mbio za wanyama (Mufradat); tena ni sauti maalumu inayotoka katika vifua vya farasi wanapokimbia (Akrab). Wakimbiaji wanaotweta, mradi wa maneno haya ni farasi.
Abdullah bin Abbas na wanazuoni wengine kama Mujahid, Ikrama, Ataa, Qatada na Dhahhaak wote wanakubali ya kuwa mradi ni farasi. Na lugha ya Kiarabu pia inasaidia maana hii.
Iliposhuka sura hii watu walikuwa na ngamia, na hakukuwa sana desturi ya kuwatumia farasi. Lakini Mwenyezi Mungu kwa kuiteremsha Aya "Wakimbiaji wanaotweta" akabashiri ya kuwa hawa watu wa Makka wapandao ngamia siku moja watakuwa wapandao farasi.
Na kweli, baadaye desturi ya kuwapanda farasi ilienea sana, na farasi wakazidi kabisa, na Waislamu wakawa wakimbiaji juu ya farasi katika matukio ya vita na amani.
Kwa neno zima, Aya hii inajulisha ya kuwa Waislamu walikuwa na shauku na huba sana ya kuitumikia dini, hata wakawabana maadui waliokuwa na nguvu nyingi na silaha kubwa. Wao walikuwa wanakwenda mbio na wakiwakimbiza farasi kwa kutoa sadaka maisha yao.
Sababu za kushuka sura hii:
Muqatil amesema kuwa Mtume s.a. w Alituma jeshi liende kabila la bani Kinana na akamteua Mundhir bin Amr al Ansariy awe kama kiongozi wa jeshi hilo.
Sasa muda mrefu umepita yapata mwezi habari za jeshi hili hazikufika Madina. Wanafiki wakaanza kutangaza kuwa wotevwaneuliwa.
Hapo ndipo Allah akatoa taarifa za jeshi hili na kisha ikashuka sura hii.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA : Mym sakina ni miym ambayo haina iβrab ( Ω Ω).
Soma Zaidi...Asbab nuzul surat al bayyinh. Sura hii imeteremka Madina na ina aya nane.
Soma Zaidi...FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.
Soma Zaidi...(vii)Dai kuwa Muhammad (s.
Soma Zaidi...FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.
Soma Zaidi...TAHADHARI KWA WASOMAJI WA QURAN Wasomaji wa qurani wawe na tahadhari katika usomaji wao.
Soma Zaidi...Sura hii ni katika sura za mwisho kushuka, huwendakuwa ndio ya mwisho kabisa. Masahaba waliamini kuwa sura hii imetabiri kifo cha Mtume S.A.W
Soma Zaidi...Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya.
Soma Zaidi...