Nini maana ya asaba katika mirathi ya kiislamu

Nini maana ya asaba katika mirathi ya kiislamu

Download Post hii hapa

Nini maana ya asaba katika mirathi ya kiislamu

Asaba - Warithi wasio na mafungu maalum



Asaba ni warithi wasiowekewa fungu maalum na hustahiki kupata mali yote ikiwa hapana wenye mafungu au kupata kilichobakia baada ya wenye mafungu kuchukua haki yao. Asaba wenyewe wako wa ama tatu:
(a)Asaba kwa nafsi yake.
(b)Asaba wa pamoja na mtu mwingine.
(c)Asaba kwa sababu ya mtu mwingine.
(a)Asaba kwa nafsi yake


(a)Asaba kwa nafsi yake
Ni wale wanaume tu ambao uhusiano wao na huyu marehemu haukuingiliwa na mwanamke. Nao ni hawa wafuatao:
I .Mtoto mwanamume.
2.Mjukuu (mwanamume).
3. Baba.
4.Babu (baba yake baba).
5.Ndugu wa kwa baba na mama.
6.Ndugu wa kwa baba.
7.Mtoto mwanamume wa ndugu wa kwa baba na mama.
8.Mtoto mwanamume wa ndugu wa kwa baba.
9.Ami wa kwa baba na mama.
1O.Ami wa kwa baba.
11.Mtoto mwanamume waAmi wa kwa baba na mama.
12.Mtoto mwanamume waAmi wa kwa baba.
13.Bwana na bibi mwenye kumuacha mtumwa huru.
14.Asaba wa mwenye kuacha huru mtumwa.



(b)Asaba wa Pamoja na mtu mwingine:
I .Binti akiwa pamoja na kijana mwanamume.
2.Binti wa mtoto wa kiume (mjukuu) akiwa pamoja na mtoto
mwanamume wa mtoto mwanamume (mjukuu wa kiume).
3. Dada wa kwa baba na mama akiwa pamoja na ndugu wa kwa
baba na mama.
4.Dada wa kwa baba akiwa pamoja na ndugu wa kwa baba.
5.Dada wa kwa baba na mama au wa kwa baba akiwa pamoja na babu.



(c) Asaba kwa sababu ya mtu mwingine:
Ni dada wa kwa baba na mama au wa kwa baba tu atakapokuwa pamoja na binti au binti wa mtoto wa kiume au wote wawili.



Musharakah - Kushirikiana fungu:
Ingawa asaba wote utaratibu wao wa kurithi ni mmoja lakini nani kati yao mwenye haki zaidi ya kurithi pindi wakitokea pamoja itategemea na uzawa wa karibu na uwiano wa uhusiano na maiti. Kwa mfano, uhusiano wa kwa baba na mama una nguvu zaidi kuliko uhusiano wa kwa baba tu, kwa hiyo, asaba wa kwa baba na mama ana haki ya kurithi kuliko asaba wa kwa baba tu.



Tumefahamu kwamba asaba hana fungu, bali huchukua urithi wote kama hakuna mwenye fungu, au huchukua kilicho bakia baada ya wenye mafungu kuchukua chao au hukosa kabisa kama hakuna kilicho bakia au wakati mwingine asaba wenye daraja sawa na mwenye fungu, watashirikiana fungu hilo. Kwa mfano: Amekufa mtu akaacha mume, mama, ndugu wa kwa mama zaidi ya mmoja na ndugu wa kwa baba na mam




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1735

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Aina za twahara na aina za najisi
Aina za twahara na aina za najisi

Katika post hii utakwenda kuzijuwa aina za twahara katika uislamu. Utaviona vigawanyo vya twahara kulingana na maulamaa wa Fiqh

Soma Zaidi...
Mambo yaliyo haramu kwa mwenye hedhi na nifasi
Mambo yaliyo haramu kwa mwenye hedhi na nifasi

Katika post hii utakwenda kujifunza mambo ambayo ni haramu kwa mwanamke aliye na hedhi na nifasi

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya Talaka katika uislamu
Ni nini maana ya Talaka katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Hali ya kuzuiliana kurithi katika uislamu
Hali ya kuzuiliana kurithi katika uislamu

KuzuilianaTumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10.

Soma Zaidi...
NI ZIPI NGUZO NA SHARTI KUU ZA SWALA ILI IKUBALIWE
NI ZIPI NGUZO NA SHARTI KUU ZA SWALA ILI IKUBALIWE

Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali.

Soma Zaidi...
Njia za kujitwaharisha, na vitu vinavyotumika kujitwaharisha
Njia za kujitwaharisha, na vitu vinavyotumika kujitwaharisha

Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha.

Soma Zaidi...
Namna ya kutayamamu hatuwa kwa hatuwa
Namna ya kutayamamu hatuwa kwa hatuwa

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu.

Soma Zaidi...