image

Nini maana ya asaba katika mirathi ya kiislamu

Nini maana ya asaba katika mirathi ya kiislamu

Asaba - Warithi wasio na mafungu maalum



Asaba ni warithi wasiowekewa fungu maalum na hustahiki kupata mali yote ikiwa hapana wenye mafungu au kupata kilichobakia baada ya wenye mafungu kuchukua haki yao. Asaba wenyewe wako wa ama tatu:
(a)Asaba kwa nafsi yake.
(b)Asaba wa pamoja na mtu mwingine.
(c)Asaba kwa sababu ya mtu mwingine.
(a)Asaba kwa nafsi yake


(a)Asaba kwa nafsi yake
Ni wale wanaume tu ambao uhusiano wao na huyu marehemu haukuingiliwa na mwanamke. Nao ni hawa wafuatao:
I .Mtoto mwanamume.
2.Mjukuu (mwanamume).
3. Baba.
4.Babu (baba yake baba).
5.Ndugu wa kwa baba na mama.
6.Ndugu wa kwa baba.
7.Mtoto mwanamume wa ndugu wa kwa baba na mama.
8.Mtoto mwanamume wa ndugu wa kwa baba.
9.Ami wa kwa baba na mama.
1O.Ami wa kwa baba.
11.Mtoto mwanamume waAmi wa kwa baba na mama.
12.Mtoto mwanamume waAmi wa kwa baba.
13.Bwana na bibi mwenye kumuacha mtumwa huru.
14.Asaba wa mwenye kuacha huru mtumwa.



(b)Asaba wa Pamoja na mtu mwingine:
I .Binti akiwa pamoja na kijana mwanamume.
2.Binti wa mtoto wa kiume (mjukuu) akiwa pamoja na mtoto
mwanamume wa mtoto mwanamume (mjukuu wa kiume).
3. Dada wa kwa baba na mama akiwa pamoja na ndugu wa kwa
baba na mama.
4.Dada wa kwa baba akiwa pamoja na ndugu wa kwa baba.
5.Dada wa kwa baba na mama au wa kwa baba akiwa pamoja na babu.



(c) Asaba kwa sababu ya mtu mwingine:
Ni dada wa kwa baba na mama au wa kwa baba tu atakapokuwa pamoja na binti au binti wa mtoto wa kiume au wote wawili.



Musharakah - Kushirikiana fungu:
Ingawa asaba wote utaratibu wao wa kurithi ni mmoja lakini nani kati yao mwenye haki zaidi ya kurithi pindi wakitokea pamoja itategemea na uzawa wa karibu na uwiano wa uhusiano na maiti. Kwa mfano, uhusiano wa kwa baba na mama una nguvu zaidi kuliko uhusiano wa kwa baba tu, kwa hiyo, asaba wa kwa baba na mama ana haki ya kurithi kuliko asaba wa kwa baba tu.



Tumefahamu kwamba asaba hana fungu, bali huchukua urithi wote kama hakuna mwenye fungu, au huchukua kilicho bakia baada ya wenye mafungu kuchukua chao au hukosa kabisa kama hakuna kilicho bakia au wakati mwingine asaba wenye daraja sawa na mwenye fungu, watashirikiana fungu hilo. Kwa mfano: Amekufa mtu akaacha mume, mama, ndugu wa kwa mama zaidi ya mmoja na ndugu wa kwa baba na mam




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 627


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

MAMBO YANAYOBATILISHA (HARIBU) SWALA YAKO
Lugha ya Swala Lugha ya swala,kuanzia kwenye Takbira ya kuhirimia Swala mpaka kumalizia swala kwa Salaam, ni Kiarabu. Soma Zaidi...

Je manii ni twahara au najisi?
Post hii itakwenda kukufundisha hukumu ya manii kuwa ni twahara ama ni najis Soma Zaidi...

Usawa na uhuru wa kuchuma mali katika uislamu
Uchumi wa uislamu umeweka taratibu mbalimbali katika kuchuma mali. Soma Zaidi...

Haki na wajibu kwa mayatima
Soma Zaidi...

Ni watu gani wanaopewa Zaka
Soma Zaidi...

Zijuwe funga za sunnah na jinsi ya kuzifunga
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu funga za sunnah na jinsi ya kuzigunga. Soma Zaidi...

kanunu na sheria za biashara katika islamu
Soma Zaidi...

Mambo yanayoweza kutoa udhu wako
Post hii itakufundisha mambo ambayo yanabatilisha udhu. Soma Zaidi...

Jinsi uislamu ulivyokomesha biashara ya utumwa wakati na baada ya mtume Muhammad (s.a.w)
Soma Zaidi...

Kujitwaharisha kutokana na najisi
Post hii itakufundisha namna ya kutwaharisha Najisi. Soma Zaidi...

Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu
Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili. Soma Zaidi...

Mambo yanayoharibu Udhu (yanayobatilisha udhu)
Post hii inakwenda kukufundisha mambo ambayo hubatilisha udhu yaani mam,boa mbayo yanaharibu udhu. Soma Zaidi...