3.
3.0 MAMBO YA FARADH KWA MAITI YA MUISLAMU.
3.1 Kuna aina Kuu mbili za Faradh.
Fardh A’in.
Ni faradh inayomlazimu kila mtu binafsi kuitekeleza, haina uwakilishi.
Mfano; kusimamisha swala, kufunga saumu, kuhiji, kutoa zaka, n.k.
Faradh Kifaya.
Ni faradh ya kuwakilishana, wachache wakitekeleza hutosheleza hitajio.
Mfano; kuswalia maiti, n.k. lakini akikosekana wa kuwakilisha, waislamu wote wanaohusika watawajibika.
3.2 Mambo ya lazima kufanyiwa maiti wa Kiislamu.
- Kila nafsi itaonja mauti (kifo). Qur’an (3:185) na (4:78).
Mambo manne yafuatayo ni lazima kufanyiwa maiti ya kiislamu:
1.Kuoshwa (Kukoshwa).
2.Kuvikwa sanda (kukafiniwa).
3.Kuswaliwa.
4.Kuzikwa.
Mambo muhimu anayofanyiwa Muislamu (mtu) anayekaribia kufa.
Mtu akikaribia kufa huwa hajiwezi kwa lolote lile pamoja na elimu, ujuzi alionao, hivyo huhitajia kufanyiwa mambo yafuatayo;
i.Kuogeshwa, kugishwa mswaki na kumpaka mafuta au manukato kama kuna uwezekano.
ii.Kumlaza kwa ubavu wa kulia au chali na kumuelekeza Qibla iwapo kuna uwezekano.
iii.Kumpa maji ya kunywa.
iv.Kutamka (kumsomea) – Shahada “Laa ilaha illallaah”
Abu Said na Abu Hurarirah wamesimulia kuwa, Mtume wa Allah amesema: “Wasomeeni watu wenu wanaokaribia kufa; ‘Laailahaillallaah”
Pia Mu’az bin Jabal amesema kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Yule ambaye maneno yake ya mwisho yatakuwa; “Laailahaillallaah” ataingia peponi.
(Abu Daud)
- Si lazima anayekufa aitamke kwa sauti, inaweza ikawa kimoyo moyo.
Mambo anayofanyiwa mtu (maiti) mara tu baada ya kufa.
Baada ya mtu kufa inatuwajibikia tuseme: “Innalillah wainnailaihraaji’una”. Qur’an (2:156). Kisha kumfanyia maiti mambo yafuatayo:
i.Kwa taratibu kurudishia mdomo wake usiwe wazi kwa kufunga kwa kitambaa kutoka kidevuni na kuzungushia kichwani.
ii.Kufunga macho ya marehemu na huku ukisema;
“Kwa jina la Allah na kwa kufuata mila ya Mjumbe wa Allah, Ewe Mola wetu mrahisishie mambo yake ya sasa na msahilishie mambo yake ya baadaye. Na jaalia anayokutanayo yawe bora kuliko aliyoyaacha.”
iii.Lainisha viungo vyake (miguu na mikono) kwa kukunja na kukunjua taratibu.
- Kama kuna ugumu maji ya uvuguvugu au mafuta yanaweza kutumika kulaisha na kunyoosha viungo hivyo.
- Baada ya kulainisha viungo, miguu na mikono inyooshwe na kulazwa uso ukielekezwa Qibla kwenye mkeka au kitanda kisicho na godoro.
iv.Maiti avuliwe nguo zote alizokufa nazo na kisha kufunikwa kwa shuka kubwa
- Ni vyema afunwe kitambaa tumboni au kuwekewa kitu kizito ili tumbo lisifutuke.
v.Marashi na ubani vitumike kwa wingi ili kuzima harufu ya uvundo wa maiti.
Baada ya kufanyiwa hatua hizo, sasa ni lazima maiti kufanyiwa yafuatayo:
Mambo haya ni faradh Kifaya, wakifanya wachache wanawakilisha wengine.
Umeionaje Makala hii.. ?
Kipengele hichi tutajifunza namna ya kusimamisha swala ukiwa safarini na vitani na nguzo zake.
Soma Zaidi...Mafungu ya urithi yaliyotajwa katika haya sita yafutayo:1.
Soma Zaidi...Atika uislamu swala la kupanga uzazi linaruhusiwa endapo kutakuwa na sababu maalumu za kisheria.
Soma Zaidi...Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwedna kujifunza jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi kwa mujibu wa mafundiso ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Soma Zaidi...