Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Rafiki wa ukweli

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Rafiki wa ukweli

Muendelezo....

Download Post hii hapa

RAFIKI WA KWELI

 

 

 

Mungu ashukuriwe sana, hatimaye miezi kadhaa ikapita bila ya waziri Masoud kugundua siri nzito. Mfalme aliendelea kumkumbusha waziri Faridi hatimaye akasahau kabisa lile swala. Miezi saba ikapita. Maradhi ya ajabu yakampata waziri faridi na akafariki dunia. Baada ya taratibu za mazishi kukamilika haikupita hata miezi mitatu mama Nurdini akafariki dunia. Loo !!!!! yalikuwa ni maonzi juu ya majonzi kwa Nurdini ambaye siku zote alitegemea baba na mama. Kwa kweli kizuri hata hakidumu kwa muda mrefu. Ukweli ni kuwa mzee Faridi aliishi mika mingi na kula chumvi nyingi. Alifariki akiwa na miaka 81. je kizuri hakidumu kweli?

 

 

 

Nurdini sasa akiwa yaima, akawa ndiye mrithi wa pekee wa mali za baba. Hakuweza kuwafahamu ndugu za baba yake hatammoja. Maisha yaliendelea, aliendelea kula mali za baba bila kuzalisha. Aliendelea kufurahi na mkewe kipenzi. Marafiki zake waliendelea kula na kusaza. Waliendelea kutanua na mengineyo kibao. Kama ilivyo mali bila daftari huisha bila habari, hatimaye mali ya Nurdini ikaendelea kupungua kwa kasi sana. Kweli bandubandu hualiza gogo. Baada ya miezi kadhaa pesa zilimuishia. Nurdini akaanza kuuza Watumwa wote apate pesa ya kutumi,.

 

 

 

Mambo hayakumnyookea, marafiki wakakata mguu kabisa kuonana naye. Akaanza kuuza vitu vya ndani hata vikamwishia na kubakiwa na kitanda na vitu vichavche kwa ajili ya kupikia. Mwishowe akaamuwa kwenda kumuuza mewe ambaye alikuwaga ni mtumwa hapo mwanzo. Hii ni kutokana na ushauri wa mkewe kumuonea huruma mumewe hivyo akamwambia amuuze apate pesa, huwenda akazalisha pesa ya kumkomboa na wakakutana mbele ya safari. Nurdini alimpenda sana mkewe lakin aliamini kuwa ushauri huu ni mzuri.

 

 

 

Alimchukuwa mkewe na kwenda kumuuza kwa pesa ile ambayo baba yake alimnunulia. Waziri Masoud alimuona Nurdini akimuuza mtumwa ambaye anafanana sifa na yule aliyekuwa akitafutwa na baba ake. Hapo aliamini kuwa baba yake alimpatia mwanaye mtumwa wa mfalme. Masoud aliweka oda ya kumnunua yule mtumwa, lakini Nurdini alipotambuwa hili akagoma kumuuza maana aliamini kwa ukorofi wa Masoud asingeweza kumpatia pesa. Ikabakia ugomvi kati ya Masoud na Nurdini. Nurdini wakati huo akamchukuwa mkewe na kumtia kwenye farasi tayari kuondoka mbio.

 

 

 

Masoud alitaka kutumia uwaziri wake lakini alishindwa, kwani Nurdini alikuwa ni mjeuri. Masoud akamvuta shati Nurdini na akaanguka chini yeye na mkewe, tena kwenye matope. Nurdini alimpiga ngumi waziri, ngumi iliyomtoa damu. Kisha akatimua mbio. Waziri bila ya kujifuta damu akaenda kwa mfalme kushitaki. Hiko akaeleza wazi kila ambacho kilitokea kwa yule mtumwa aliyemtaka kuwa bwana faridi alimuozesha mwanaye na sasa mtoto anataka kumuuza.

 

 

 

Mfalme alikasirika sana, na akatangaza aletewe Nurdini popote alipo. Jeshi kubwa liliamuriwa likamchukuwe Nurdini. Katika jeshi lile alikuwepo kijana mmoja aliyekuwa na ukaribu sana na baba Nurdini, hivyo akaenda mbio kwa Nurdini na kumtaarifu akimbie haraka sana. Nurdini hakuamini anachoambiwa ila akakubali kuamini, hivyo akajiandaa kuondoka yeye na mkewe. Yule askari akampatia nurdini kiasi cha pesa alicho nacho na kuwafanyia mipango ya kupata jahazi dogo la kuondokea kwasiri. Mambo haya yalifanyika kwa siri sana na haikuchukuwa muda Nurdini akaondoka, na mkewe kuelekea Baghadad.

 

 

 

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Mankaa image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Burudani File: Download PDF Views 409

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 11: Kisa cha Kalid na Jalid
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 11: Kisa cha Kalid na Jalid

Tuendelee kusikiliza na kusoma visa, hadithi, na simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza tuwe pamoja mpka mwisho......

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 9: Hadithi ya binti wa ndotoni.
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 9: Hadithi ya binti wa ndotoni.

Simulizi hii pia inapatikana kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 12: Hadithi ya mfalme alikuwa kwenye kisima
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 12: Hadithi ya mfalme alikuwa kwenye kisima

Wapendwa tuendelee kuoata stori nzuri na za kusisimua kutoka katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Mtumwa wa mfalme na mawaziri
Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Mtumwa wa mfalme na mawaziri

Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha tatu.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 6: Hadithi ya Ndoa ya siri
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 6: Hadithi ya Ndoa ya siri

Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili muendelezo....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 2 Part 3: Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi.
Simulizi za Hadithi EP 2 Part 3: Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi.

Simulizi za HALIF LELA U LELA ni nziri sana tuwe pamoja kusikiliza kisa cha mzee wa pili na mbwa wawili weusi...

Soma Zaidi...