image

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 8: Hadithi ya kisiwa cha uokozi

Simulizi hii ipo ndani ya kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA....

KISIWA CHA UOKOZI

 

Nilikwenda mpaka nikakuta misitu minene na nisijuwe pa kuenda. Kwa ghafla nikasikia sauti za watu wanaowinda na kwa uchovu nilonao nilianguka chini na kwa njaa nilonayo nilipootelewa na fahamu. Hapo sikujuwa kilichoendelea hata nikashituka nipo kwenye kitanda safi na pembeni kuna binti mzuri ananiwekea chakula tayari kwa kuniamsha ili nipate kula chakula. Bila hata kujaribu kuniamsha niliamka kwa upole na kumuuliza swali “eti unaitwa nani, na nimefikaje hapa?”. “naitwa ‘Aisha ni mtoto wa mfalme, umeokotwa porini na baba alipokuwa akiwinda”. Ni maneno aliyoyasema bint Aisha mtoto mfalme.

 

Nikanawa maji tayari kwa kuanza kula, baada ya muda wa dakika takriban 10 aliingia mfalme, na nilimtambua kwa mavazi yake. Baada ya utambulisho nikawaelezea kila kilichonikuta. Na akazungumza kuwa kwa uda wa miaka 10 wamekuwa wakikitafuta kijiji hiko bila mafanikio. Inadaiwa kuwa wakazi wa kijiji hiko sio watu wa kawaida hivyo walishangaa kuniona mimi nimeweza kutoroka kwenye kijiji kile kisichofikika. Basi mfalme aliniuliza mengi kuhusu Baghadad na bila kusita nikawa namjibu kwa uwazi kabisa. Kwa hakika alivutiwa sana na majibu yangu.

 

Mfalme alinitambulisha kwenye baraza lake na kunifanya mimi mmoja ya washauri wake na watu wa karibu. Niliishi pale kwa muda wa wiki moja hata siku hiyo baada ya swala ya magharibi nikasikia mlango unagongwa. Nikaenda kufunguwa nikamkuta mfalme na mkewake. Kwa heshima kubwa nikawakaribisha na walionesha uso wa furaha hata nisiijue sababu ya ujio wao. Baada ya kuwapatia maji ya kunywa mfalme akaanza kuzungumza.

 

“mwanangu, ujio wetu hapa mimi na mama yako ni kutaka ushauri wako. Kama ujuavyo sisi tuna mtoto mmoja tu naye ni wa kike. Pia binti yetu ameonesha kuvutiwa sana na wewe. Hivyo tumekuja kukuomba uwe mkwe wetu na mrithi wa utawala huu baada ya kufa kwangu”. Kimoyoni nilifurahi sana japo nikamwambia mfalme “nashukuru sana kwa maneno yako baba yangu mtukufu mfalme. Naomba muda nifikirie na nitakujibu baada ya mshuko wa swala ya ijumaa keshokutwa in shaa Allah” Basi mfalme akakubali kunipa muda ule na kuondoka.

 

Nilitafakari sana nini nifanye na nikikubali kuoa pale nitaondoaje kwenda Baghadad. Nitakuwa mkwe na mtoto wa kiume wa mfalme, na nitatakiwa kuurithi ufalme ule, hivyo ndoto zangu za akurudi nyumbani zitakuwa zimekwisha. Siku ilofata asubuhi nikaenda kwa rafiki yangu ambaye mkewe alikuwa akiumwa na tumbo. Nikaenda kumuomba ushauri lakini nikamkuta analia sana. Sikuweza kumuomba tena ushauri badala yake nikamuuliza kinachomliza zaidi. “rafiki yangu, tambuwa kuwa katika nchi yetu hii, akifa mke mume atazikwa pamoja na mkewe akiwa hai, na akifa mume mke atazikwa na mkewe akiwa hai. Hivyo nalia kama mke wangu akifa na mimi ndo mwisho wangu.

 

Niliposikia maneno yale pale moyo wnagu ulipasuka na kudunda haraka. Nikaanza kutetemeka miguu na meno. Jasho jingi lilinitoka japo kulikuwa na baridi wakati ule. Yote hayo yalitokea nilipokuwa nawaza nni nitamjibu mfalme. Maana nikikubali kuoa nikifa mimi wa kwanza sio taabu ana ila akitangulia kufa mtoto wa mfalme nitazikwa pamoja naye nikiwa hai. Mawazo haya yaliniumiza sana hata nikakosa hamu ya kula kabisa. Jioni ile mmnikapita nyumbani kwa mfalme na kumkuta binti yake akiumwa eti amekataa kula mpaka asikie jibu langu kwanza.

 

Hali ile ikazidi kuniogopesha zaidi pale niliposikia kuwa binti mafalme ameahidi kujiuwa kama nitamkataa. Nikaogopa zaidi niliposikia hivi. Nilijihisi uchovu na nikaelekea nyumbani kulala. Siku ilofata ilikuwa ndio siku ya ijumaa ambapo mfalme nimemuahidi kumpatia jibu juu ya kumuoa mwanae. Niliamka mapema sana siku ile na kuoga kisha nikaenda msikitini na kuwahi mstari wa mbele. Niliswali rakaa mbili na kufanya istikhara yaani kumuomba Mungu anipe majibu ya maswali yangu.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-10 09:35:43 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 36


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 20: Waliodhulumiwa kufanyiwa suluhisho
Ni mojawapo ya simulizi iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 14: Wageni
Simulizii hii ni nzuri na ni mojawapo ya hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Hatma ya Nurdini
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 9: Hadithi ya deni la mapenzi
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Bostani la kifalme baghadad
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 4: Kisa cha waziri aliyeadhibiwa
Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 8 Part 2: Siri ya kifo
Simulizi hii pia inapatikana kwenye kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 10: Ndoa ya binti mfalme na Sinbad
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza muendelezo...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 1: Hadithi ya chongo watatu, watoto wa mfalme na wanawake wa Baghdad.
Skmulizii hii pia imetoka kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 13: Jaribio kwa Aladini kwa mara ya kwanza
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 7: Sehemu ya nne ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa hadithi ya safari ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 1 Part 2: Simulizi ya kisa cha mfugaji na mkewe
Simulizii hii ni inatoka katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA Soma Zaidi...