Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza muendelezo....
KWISHA KWA CHAKULA
Watu waliaanza kumaliza vyakula vyao na wakaanza kufa baada ya siku kadhaa. Tulianza kuwazika mpaka wenzangu wote wakaisha hata nikamzika mwenzeu wa mwisho pekeangu na kubakia mimi tu. Nikiwa na mkate mmoja tu wa ngano ulobakia nikaaza kulia na kijuta kuwa bora nisingesafiri. Nilikata tamaa na nguvu ziliniishia nikajua sasa ndo nakufa mimi. Wakati nilipokuwa nimekaa pale niliona ndege akinywa maji ya kale kajimto. Nilitamani nimuuwe ndege yule nipate chakula.
Nilianza kumvizia ndege yule na hata nikamrushia jiwe, na kwa kiwewe ndege yule akaingia kwenye lile pango ambalo kale kajimto kamepotelea. Nilimsubiri nje ya pango ili atoke lakini hakuweza kutoka hata ikafika jioni. Nikala kipande cha mkate na kubakiwa na kipande kimoja. Ilipofika asubuhi nikapata akili luwa kama yule ndege hakuweza kutoka kwenye [pango lile kutakuwa na mabo makuu mawili yanaweza kutokea, moja huenda ameliwa au ametokea nje ya pango sehemu nyingine. Hapo nikajipa matumaini kuwa mto huu utakuwa umetokea eneo jingine.
Basi nikaanza kuunganisha mabao kisha nikajilaza kifudifudi na kukusanya mali za dhahabu, almasi na mali nyinginezo za madini katika eneo lile na kulweka mabao yangu kwenye mto ule ambao ulinichukuwa na kupotea nami kwneye pango. Niliweza kupitishwa sehemu nyembembe sana ambapo niliumia sana. Nilimaliza kipande cha mkate wangu hata nikawa sina chochote. Nikawa nawaz anaweza kufa humu kabla hata sijaliona jua. Kwa njaa na mawazo na maumivu ya kugongwa nilipoteza fahamu na nisijue kinachoendelea kwenye mto ule.
Nilipokija kuzinduka nikakuta nimezungukwa na watu wengi sana na ni wakubwa zaidi. Wakawa wananiuliza mimi ni nani na nimefika vipi pale kwenye eneo lile. Kabla sijaeleza chochote kwani sikuwa na uwezo wa kusema hivyo nikaomba wanipatie chakula na maji. Nikapewa na kuanza kuridhisha tumbo langu hata nikashiba na kumshukuru Mwenyezi Mungu. Nikawaeleza habari yangu na walishangaa sana. Wakaamuwa kunipeleka kwa mfalme wao ili apate kujuwa yalonikuta.
Walinichukuwa mimi na mabao yangu yale na mali zangu na ku nipeleka kwa mfalme wao wa kisiwa hiki kiitwache Serendib. Kwa heshima na taadhima nikamsalimia mfalme na kumueleza kila kilchotokea bila hata ya kuficha. Mfalme alishangaa sana na kuniona nimezaliwa na nyota ya ajali inayoambatana na uokovu. Mfalme akamumu habari yangu iandikwe kwa maandishi ya dhahabu na iwekwe kwenye hifadhi ya kifalme kwa vizazi vijavyo.
Nilikaa pale Serendib kwa muda wa mwezi mmoja na nikamuomba ruhusa mfalme niweze kurudi nyumbani. Alikubali na kunipatia malinyingi kisha akanipatia barua ili nikampe Sultan Harun Rashid wa Baghadad. Barua ilikuwa imeeandikwa kwenye karatasi cha bluu zilizotengenezwa na ngozi ya nyok. Maadhishi yalikuwa ni ya dhahabu yaliyochovywa na mafuta ya misk. Mfalme pia alinipatia zawadi nyingi sana kwa ajili ya familia yangu na kwa ajili ya Sultani Harun Rashi. Barua ilikuwa na lengo la kuomba urafiki kati ya vuiongozi wawili hawa.
Nilisafiri kwa amani hata nikafika kwenye bandari ya Balsora na kufika nyumbani na mali mengi sana. Niliwaeleza ndugu zangu yalonikuta na safari hii nikaadidi kuwa sasa sitosafiri tena kibiashara. Siku ilofuata nikaongozana na familia yangu na kuelekea kwa Sultan kwenda mpatia barua yake. Sultani alifurahi sana na alipenda zawadi alopewa. [ia aliniuliza habari nyingi kuhusu mfalme wa Balsora na kumridhisha maswali yake. Nikaondoka na kurudi kwangu. Baada ya hapa nikaanza kutengeneza maisha yangu na sikutaka tena kusafiri majini.
Baada ya kumaliza kusimulia hadithi hii ya safari hyake ya sita Sinbad alimpatia Sinbad wa nchikavu pesa kiasi kadhaa kama fidia ya kupoteza muda wake na kumsikiliza. Watu wakatawanyika pale na akamuahidi Sinbada awahi kesho ili asikilize kilichotokea kwenye safari yake yta saba na kwa nini alivunja ahadi yake mara hii.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Mankaa Tarehe 2024-09-10 10:17:46 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 72
Sponsored links
👉1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2
Simulizi za Hadithi Audio
👉3
Kitau cha Fiqh
👉4
Kitabu cha Afya
👉5
Madrasa kiganjani
👉6
kitabu cha Simulizi
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 1: Muuaji ni nani?
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP4 Part 5: Hadithi ya pili ya mtoto chongo wa mfalme
Hadithi za HALIF LELA U LELA huwa zina muendelezo na hadidhi hii ni muondelezo wa kisa cha pili cha mtoto chongo wa mfamle ambayo imetoka ndani ya kitabu cha kwanza cha Hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 8 Part 3: Kijana mchonganishi
Muendelezo.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part24 : Kaka wa tatu wa kinyozi
Muendelezo Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 7 Part 12: Dirisha moja kwanini????
Muendelezo.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 1: Hadithi ya chongo watatu, watoto wa mfalme na wanawake wa Baghdad.
Skmulizii hii pia imetoka kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 10 Part 5: Safari ya kwenda nyumbani
Muendelezo.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 8: Aliyekatwa kidole gumba
Kojawapo ya simulizi iliyopo kwenye kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 6: Hadithi ya Ndoa ya siri
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili muendelezo.... Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 4: Sehemu ya pili ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa hadithi ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...