image

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 9: Hadithi ya binti wa ndotoni.

Simulizi hii pia inapatikana kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...

BINTI WA NDOTONI.

 

Baada ya kufikiri kwa kina na kumuomba mungu nilipitiwa na usingizi. Niliwa usingizini nikaota ndoto ya ajabu sana. Nilipokuja kuamka niliona watu ndo wanaanza kujaa msikitini lakini mfalme bado hajafika. Nikaanza kujiuliza maana na tafasiri ya ndoto ile ya ajabu. Nikiwa katika hali ya mawazo nilikuwa nikikumbuka machache kuhusu tafasiri za ndoto. Nikaanza kuichambua ndoto yangu nilioora. Nikiwa kwenye mawazo hayo nikaona kama kuna mtu amekuja na kuniuliza kuhusu ndoto yangu ili anitafasirie.

 

Nimeota nipo safarini na binti mfalme akiwa kwenye safari ile. Tukiwa tupo kwenye jahazi kwa ghafla tulipatwa na ajali. Mule kwenye jahazi lile hakuna mtu ninayemjua asipokuwa ni binti mfalme tu. Katika ajali ile jino lanhu moja liling’oka na nikatumbukia ndani ya maji. Binti mfalme akaja na kamba na kunirushia nikaikamata kamba ile na kufika kwenye mbao kubwa ambayo binti mfalme alikuwemo. Kwa bahati mbaya bint mfalme aliteleza kwenye mbao ile na kuingia kwenye maji, niliwa sijui uogelea nilijitahidi kumuokoa bila mafanikio na akaniashiria kuwa niondoke niendezangu. Baada ya hapo nikashituka

 

Katika hali kama hiyo yule mtu akanieleza kuwa ndoto ile ni ya ukweli na kunajambo ninaelezwa kwenye ndoto ile. Yule mtu akaanza kunieleza maana ya ndoto ile. “kuhusu kuwa safarini wewe na bint mfalme ni ishara ya kushirikiana. Na kuhusu kupata ajali inamaanisha kuwa katika kushirikiana kwenu mtapatwa na matatizo lakini yeye ndiye atakayekuokoa.

 

Na kwakuwa kwenye ndoto ni wewe ndiye uliyeokolewa inamaana wewe katika matatizo yako utapata njia kupitia kushirikiana nae. Na kuhusu yeye kushindwa kuokolewa na wewe na hatimaye akaishia majini inaonesha atapatwa na matatizo na atafariki bila ya wewe kufanikiwa kumuokoa. Ama jino linamaanisha kituchako cha karibi kama mke na ndugu. Hivyo jino lako lile linaonesha ni bint mfale atakuwa mkeo na kung’oka kwa jino ni ishara ya kufariki kwa mkeo. Hii ndiyo tafariri ya ndoto yako”

 

Baada ya hpo yule mtu akatoweka, nilipokuja kupaa fahamu kutoka kwenye mawazo yale sikumuona yeyote. Nikutaka kutafuta zaidi nikaweka imani kuwa huenda ni malaika ametumwa kunisaidia kufasiri ndoto yangu. Basi nikaamuwa kumuoa bint mfalme kutokana na ndoto ile inaonesha yeye ataanza kufa na mimi nitaokoka. Hivyo nikaamini hii ni mipango ya mungu. Basi baada ya swala nikaende kwa mfalme na kumueleza kuwa nimekubai ombi lake.

 

Nilipokuwa nazungumza na mfalme kumbe yele binti alikuwa akisikiliza mazungumzo yale na aliposikia nimekubali alipata furaha kubwa iliyopelekea akazimia. Tulishangaa kusikia kishindo nyuma ya mlango na kuenda kuangalia alikuwa ni binti mfalme aliyezimia pale chini. Moyowangu uliruka sana nikawa najiuliza ndo qadar zimeanza yaani atakufa kweli hapahapa na kuniacha mimi. Aliitwa muuguzi na kuanza kumpa tiba. Nilirudi nyumbani nikiwa nasikilizia kama atakufa au atapona maana akifa nitazikwa hatakama shererhe ya ndoa haijafanyika.

 

Nikiwa na wasiwasi siku ilofata nilielekea kwa mfalme kwenda kujulia hali ya binti yake. Nilishangaa kuona mfalme akiwa na bashasha punde tu aliponiona “mwanangu, mwenzio amepata fahamu tayari na mama yenu anaandaa maandalizi ili wiki ijayo iwe ni sherehe ya ndoa yenu. Nilifurahi sana kuona kuwa binti yupo hai maana alikuwa amebeba dhamana ya uhai wangu. Nikawa najiambia moyoni kuwa wiki ijayo naingia maisha mapya na nitakuwa mfalme mtarajiwa. Sinbad mimi ndo utakuwa mwisho wa kuiona familia yangu.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-10 09:38:28 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 48


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 4: Simulizi ya chongo wa kwanza mtoto wa Mfalme
Tusikilizie simulizii inahusu chongo wa kwanza wa mtoto wa mfalme iliyopo ndani ya kitabu cha kwanza cha Hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Nudhini akiwa hatiani
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 7: Hadithi ya safari ya majibu juu ya maswali mawili
Wapendwa wasomaji na wasikilizaji wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza karibu tuendelee kusikiliza hadithi zetu mzuri na za kusisimua.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 14: Jaribio la pili kwa Aladini
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 1 Part 2: Simulizi ya kisa cha mfugaji na mkewe
Simulizii hii ni inatoka katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 11: Ndani mwa junba la Aladini
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP7  Part 17: Jaribio la tatu kwa Aladini
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 1: Carmaralzamani prince pekee
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 2 Part 1: Hadithi ya jini na mfanya biashara.
Hadithi hii ya jina na mfanya biashara imetoka katika kitabu cha kwanza cha simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza karibu tusikilize simulizi nzuri na zakusisimua Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 23: Kaka wa pili wa kinyozi
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 8: Aliyekatwa kidole gumba
Kojawapo ya simulizi iliyopo kwenye kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 16: Usaliti
Hadithi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi sana na zinavutia na zinasomwa na kusikilizwa kwa wakubwa na wadogo na hii simulizi inatoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...