Menu



Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Barua ya mfalme wa baghadad

Muendelezo.....

NURDINI ANARUDI KWAO NA BARUA YA MFALME WA BAGHADAD

Baada ya mfalme kusikiliza hadithi ile akiwa katika mavzi ya mvuvi. Aliwaaga vyema bila hata ya wao kujuwa kuwa huyu ndie mfalme wa hap ana mmilikiwa hili bustani. Baada ya mfalme kuondoka haukupita muda watatu hawa wakalala fofofo. Mfalme kwa upande wake hakupata usingizi kabisa kutokana na yale aliyoyasikia kutoka kwa kijana Nurdini. Ilipofika asubuhi Mfalme akaagiza aletwe mzee Ibrahim una wageni wake mapema kabisa kabla hata hawajaamka.

 

 

 

Basi askari wakatoka muda uleule, walipofika kule loo bado watatu wale wamelala fofofo. Askari wakawaamsha na kuwachukuwa hadi kwa mfalme. Mzee Ibrahim una vijana wake walishikwa na taharuki kubwa sana. Walijuwa kuwa siri yao leo imefichuka. Kijana Nurdini alianza kujuta na kuanza kutubia madhambi yake kwa mungu, maana alijuwa kuwa itakuwa ile sehemu waliolala sio ya kawaida. Mzee Ibrahimu alianza kuwahadithia vijana wake huku wakiwa wanaburuzwa na askari.

 

 

 

Vija wangu tambueni kuwa hii bostani sio mali yangu ni ya mfalme wa Baghadad. Na bila shaka alipata habari ya jambo lililotokea jana. Nisameheni sana vijana wangu kwa kutokuwaambia na kuwasababishia matatizo haya. Nurdini hakujali alijuwa kuwa kila kwenye uzito kutakuwa na wepesi tu. Mrembo mtumwa yeye aliendelea kubalia kimya bila hata ya kutia neno huku akiendelea kufuta machozi yake na ya mume wake Nurdini.

 

 

 

Mbele ya mfalme wakawekwa wakisubiria kitakachojiri. "mzee Ibrahimu na vijana wake wamesha wasili Mfalme" ilikuwa ni kauli ya Jafari akimpa ishara mfalme kuwa wageni wake wameshafika tayari. Mfamel kwa bashasha na tabasamu aliwakaribishwa vyema sana. Hali hii iliwashangaza watu wote pale ndani, inakuweje wafanyaji makosa wanakaribishwa hivi?. Ukweli ni kuwa hata mfalme alifurahia sana siku ya jana. Mfalme akaanza kuelezea yeye kila ambacho kilitokea siku ya jana na namna ambvyo aliazima mavari kwakarimu na kuyavaa. Pia alielezea namna ambavyo aliguswa na tukio la Nurdin.

 

 

 

Mwisho mzee Ibrahimu akaomba msamaha kwa tabia ambayo aliionyesha jana. Nurdini na mkewa wakafuata kuomba radhi. Mfalme alizidi kufurahi zaidi. Kisha aka uuliza Nurdini "je ungependa kuishi hapa ama kurudi kwwenu?" Nurdini baada ya kusita kidogo akauliza "kwani ipo nji aya mimi kurudi bila ya matatizo?" ndio ipo wala hakuna shida, ila itabidi umuache mkeo hapa kwanza. Nurdini alikubaliana na wazo hili. Kwa upande wa binti yeye hata hakupenda kuachwa na Nurdini hata kwa muda mchache.

 

 

 

Kisha mfalme akamkabidhi barua Nurdini na kumwambia "chukuwa barua hii kampe mfalme wa nchini kwako kisha usubirie majibu ila uusiisome barua hii hadi unamkabidhi". Nurdini alimtegemea Mungu maana hakuwa na uhakika kama barua ile ni ya kumuokoa ama ya kumuuza. Siku ya pili aliangana na mke wake na kuanza safari ya klurejea nchini kwao.

 

 

 

Akiwa yeye na farasi yake, huku amechomeka kabendera kadogo ka nchi ya Baghadad. Bendera hii ilikuwa ikimtambulisha kuwa yeye ni mjumbe kutoka mchi husika. Kiendera hiki kingeweza kumlinda asikamatwe mpaka kufika mbele ya mfalme. Na hii ndio maana ya kusema kuwa mjumbe hauwawi. Basi Nurdini hatimaye akawa mbele ya mfalme na kumpatia barua mabyo hata yeye hakujuwa ni nini kimeandikwa humo ndani.

 

 

 

Mfalme alipoisoma tu barua mdomo ukaanza kumtetemeka, hatimaye sura akaikunja kama aliyekula ndimu iliyowekwa kwenye kifuu cha mbata ya mnazi kitamli. Macho yalimtoka hata waziri wake wakaanza kumshangaa. Mfalme alionekana kuishiwa nguvu kabisha na akaondoka ghafla na barua yake mkononi. Alimuangalia sana Nurdini wakati anaondoka. Mawazir wasijuwe ni nini kimetokea pale.

 

 

 

Punde tu baada ya mfalme kutoka waziri Masoud alimng'olea macho Nurdini, kisha akakumbuka kilichotokea na jinsi alivyomdhalilisha mbele za watu. Kisha akaunganisha na barua aliyokuja nayo aliyompataharuki mfalme. Basi waziri Masoudi akaamrisha Nurdini afungwe gerezani. Bila ya kujuwa kinachoendelea ama nininkimo kwenye barua masoud alifanya maamuzi ya kukurupuka sana. Ni siku tatu zimepita toka Nurdini aondoke Baghadad.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Mankaa image Tarehe: 2024-09-10 15:03:43 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF Views 180

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 2 Part 2: Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake

Simulizi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi sana na husikiliwa na kusomwa na wakubwa kwa wadogo pia hadithi hizi zimeenea duniani Kate zikisikilizwa na maelfu ya watu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 9: Hadithi ya binti wa ndotoni.

Simulizi hii pia inapatikana kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 14: Simulizi ya binti wa kwanza na mbwa

Tuendeleee kuburudika na simulizii zetu nzuri kutoka katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 3: Uokozi kwenye kisiwa

Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza......

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 3: Mlevi asimuliwa hadithi

Muendelezo wa simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 8: Aliyekatwa kidole gumba

Kojawapo ya simulizi iliyopo kwenye kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Hadithi ya Nurdini Mtoto wa Waziri

Hii ni hadithi ya kitabu cha tatu cha hadithi za HALIF LELA U LELA...

Soma Zaidi...