Quran si maneno ya mwenye kifafa

Quran si maneno ya mwenye kifafa

(iv)Dai kuwa Qur-an ni zao la Mwenye Kifafa na Aliyepagawa na Shetani:



Waandishi kadhaa wa kikafiri katika maandishi yao wamedai bila kutoa ushahidi wowote unaotokana na historia kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa mwenye kifafa na mwenye kupagawa na Shetani na maneno yake alipokuwa katika hali ya ugonjwa ndiyo yaliyonukuliwa na kuunda Kitabu cha Qur-an!



Udhaifu:
Udhaifu wa dai hili tunaweza kuuona kwa kujiuliza maswali yafuatayo: Je, kifafa, ugonjwa mbaya kama tunavyoufahamu, umewahi kumtokea mtu katika historia ya mwanaadamu na bado akawa mtu mwenye kutoa sheria za kufuatwa na umati wa watu wengi zaidi ya robo ya dunia? Je, historia ya mwanaadamu imewahi kumshuhudia mgonjwa wa kifafa au mwenye kupagawa na shetani kuwa na hadhi na uwezo mkubwa kuliko mtu yeyote ulimwenguni kama ilivyokuwa kwa Mtume Muhammad (s.a.w)? Kama mgonjwa wa kifafa ndiye aliyeandika Qur-an, inakuwaje waandishi hodari wenye akili timamu na wanafalsafa wakubwa washindwe kuandika kitabu mithili ya angalau sura moja ya Qur-an na kukabili changa moto iliyotolewa na Qur-an karne nyingi zilizopita:



"Je! Ndiyo wanasema ameitunga? Sema: "Hebu (tungeni na nyie) mlete sura moja mfano wake na waiteni muwezao (kuwapata waje).- isipokuwa Mwenyezi Mungu - (wa kuwasaidieni) kama nyinyi mnasema kweli (kuwa haya ameyazua Muhammad)." (10:38)



Kitaalam inafahamika kuwa ugonjwa wa kifafa baada ya muda humfanya mgonjwa kuwa taahira (punguani). Pia ugonjwa wa kifafa humdhoofisha mgonjwa na hutisha wauguzaji na wenye kumuangalia mgonjwa wakati ameshikwa na kifafa. Hapana ushahidi wowote katika historia ya Mtume (s.a.w) ambayo iko bayana mno kuliko historia ya mtu yeyote, kuwa alikuwa mwenye kifafa au mwenye kupagawa na shetani.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1043

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Maana ya Idgham na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Aina za idgham ni idgham al mutamathilain, na idgham al mutajanisain

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA QALQALA

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
HIKUMU YA BASMALLAH YAANI KUSOMA BISMILLAH

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat Al-Kawthar

Sura hii ni miongoni mwa Sura fupi sanya huwenda ndiosura yenye aya chache kuliko sura zote katika Quran.

Soma Zaidi...
Quran na sayansi

3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran??

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al-Falaq na surat an-Nas na fadhila za kusoma sura hizi

SURAT AL-MUAWIDHATAYN (SURAT AL-FALAQ NA SURATUN-NAS) Inaelezwa kuwa sura mbili hizi zilishuka pamoja, na maulamaa wanaelezea kuwa Mtume (s.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Zilzalah

surat Zalzalah ni sura ya 99 katika mpangilio wa Quran, na ina aya 8. Sura hii imeteremshwa Madina ila pia kuna kauli zinathibitisha kuwa ni ya Makkah. Katika hadithi iliyopewa daraja la hassan na Imam Tirmidh Mtume S.A.W amesema kuwa kusoa surat Zilzalah

Soma Zaidi...