image

Uthibitisho kuwa quran ni maneno ya Allah kutokana na Historia (Hadith)

Uthibitisho kuwa quran ni maneno ya Allah kutokana na Historia (Hadith)

(b)Uthibitisho kutokana na Historia (Hadith)



Historia ya kushuka Qur-an na namna Mtume (s.a.w) alivyoipokea ni ushahidi mwingine unaotuthibitishia kuwa Qur-an si kitabu alichokitunga Muhammad (s.a.w). Kuna maelezo kadhaa ya kihistoria tunayojifunza katika Hadith juu ya namna Mtume (s.a.w) alivyoipokea Qur-an. Hebu turejee hadithi zifuatazo:



(1)Hadithi ya bibi Aysha (r.a) iliyopokelewa na Imamu Bukhari inatufahamisha namna Mtume (s.a.w) alivyopokea wahyi wa kwanza wa Qur-an alipokuwa katika pango la Jabal Hira. Kama tulivyojifunza katika hadithi hiyo Mtume (s.a.w) alistushwa sana na tukio lile la kujiwa na Malaika Jibril (a.s) na kumuamrisha kusoma kinyume na uwezo wake. Tukio lile lilimhofisha sana Mtume (s.a.w) na kumfanya arejee nyumbani kwake akiwa anatetemeka. Tukio la Jabal Hira ni ushahidi mwingine tosha kuwa Qur-an si maneno ya Muhammad (s.a.w) bali ni ujumbe kutoka kwa Allah (s.w) uliofikishwa kwake kwa njia ya wahyi kupitia kwa Malaika Jibril.



(2)Mtume (s.a.w) alikuwa akibadilika haiba yake na kutokwa na jasho wakati wa kupokea wahyi kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:
Bibi aysha (r.a) amesimulia: Kwa hakika nimemuona Mtume akiteremshiwa wahyi siku ya baridi kali na baada ya kumaliza kile kipindi cha kuteremshiwa wahyi alimininikwa na jasho jingi kichwani mwake." (Malik)



Amesimulia Aysha (r.a), "Al-Harith bin Hisham (r.a) alimuuliza Mtume wa Allah, 'Ee mtume wa Allah! Ni vipi wahyi unakuja?' Mtume wa Allah alijibu, "Wakati mwingine ulifunuliwa kwangu kwa sauti mithili ya mlio wa kengele, wahyi ulioletwa kwa namna hii ulikuwa mgumu sana kuliko aina nyingine zote (za wahyi), kisha hali hii ilikwisha baada ya kukidhibiti kile kilichofunuliwa. Wakati mwingine Malaika


(Jibril) alikuja katika umbile la binaadamu na kuzungumza nami, ambapo nilikidhibiti (nilikichukua) chochote kile alichosema." Aysha (r.a) aliendelea kusema: Hakika nilimuona Mtume (s.a.w) wakati anateremshiwa wahyi siku ya baridi kali na kuona jasho likitiririka usoni mwake." (Bukhari)
Hadithi hizi nazo zinatuthibitishia kuwa Qur-an si utunzi wa Muhammad (s.a.w) kabisa,bali ni ujumbe wa Allah (s.w) uliopitia kwake kwa njia ya wahy.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 319


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Fadhila za surat al-fatiha na sababu za kushuka kwake
1. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al Mauun
Sura hii ni katika sura ambazo zinahitaji kusomwa kwa mazingatio sana. Wanaoswali bila ya kuzingatia swala zao, wameonywa vikali sana. Wanaowatesa na kuwanyanyasa mayatima wameonywa vikali. Wanaowanyima wenye haja na masikini huku wakiwakaripia nakuwasem Soma Zaidi...

Mtume hakufundishwa quran na Jabir na Yasir
Soma Zaidi...

IDGHAAM KATIKA LAAM
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Hukumu za waqfu na Ibtida
waqfu ni misimamo ambapo msomaji wa Quran anaruhusiwa kusimama, kuhema au kumeza mate. Na ibtidai ni kuanza baada ya kutoka kwenye waqf Soma Zaidi...

HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Maisha ya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 19. Hapa utajifunza maisha ya Mtume kabla ya utume. Soma Zaidi...

Amri ya Kuchinja Ng'ombe
Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr. Soma Zaidi...

Kwa nini quran ilishuka kidogo kidogo?
Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo Soma Zaidi...

Tafsiri na mafunzo ya sura zilizochaguliwa - Saratul-fiyl
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maana ya Quran na Majina ya quran n amaana zao
Soma Zaidi...

Quran Tafsiri kwa Kiswahili
Tafsiri ya quran kw akiswahili, imeandikw ana Shekh Ali Muhsin al-Barwani Soma Zaidi...