image

Quran haikutoka kwa Mtu zezeta wala mwenye upungufu wa akili

Quran haikutoka kwa Mtu zezeta wala mwenye upungufu wa akili

(iii)Dai la Kujidhania Kupata Wahy (Self Revelation)



Bwana E. Birmngham katika kitabu chake anadai kuwa, kwa sababu Muhammad (s.a.w) alikuwa mkweli na mwadilifu alichukia sana moyoni mwake kwa jinsi uovu na ufisadi ulivyoshamiri katika jamii yake. Kutokana na mwangaza aliokuwa nao yeye mwenyewe binafsi akaona kuwa ipo haja ya kuijenga upya jamii hiyo. Huenda pia alisikia juu ya kitabu cha Wayahudi na Wakristo lakini hakupendezwa na mafundisho ya Utatu Mtakatifu (Trinity). Na yawezekana alisikia kuwa atakuja nabii kutoka katika eneo hilo. Mambo hayo yakawa yanazunguka ndani kabisa ya nafsi yake, hadi kufikia kuamini kuwa yeye ni mtume na ndipo akaanza kupata fikra za kimazezeta kuwa Malaika wanamsemesha.



Udhaifu:
Endapo kama chimbuko la Qur-an ni hisia za ndani za nafsi ya Muhammad (s.a.w) (subconsciousness), basi Qur-an itakuwa inatokana na elimu na mazingira yake. Lakini ukiiangalia Qur-an kwa makini utaona kuwa imetoa taarifa nyingi sana ambazo itakavyokuwa vyovyote haziwezi kuwa zimetoka katika nafsi ya Muhammad (s.a.w).
Kwa mfano Qur-an inaeleza matukio ya kihistoria au matukio yatakayotokea baadaye ambayo Muhammad(s.a .w) hakuyajua na wala hakuwa na namna ya kuyajua. Kwa mfano:



(1 )Sura ya 18 ya Qur-an, Al-Kahf iliteremka baada ya Muhammad (s.a.w) kuulizwa maswali matatu na makafiri wa Makka ili kumjaribu. Maswali hayo waliyauliza baada ya kushauriana na watu wa Kitabu (Mayahudi). Maswali hayo yalikuwa:


(i)Ni kipi kisa cha vijana wa pangoni?
(ii)Ni kipi kisa cha Al-Khidhr?
(iii)Unajua nini juu ya Dhul-qarnain?



Kwa kuwa maswali haya yalifungamana na historia ya Wakristo na Wayahudi, na habari zake hazikujulikana Hijaz, yalikusudiwa kumpima Mtume (s.a.w) kuwa kweli alikuwa Mtume wa Allah (s.w) aliyekuwa akipokea wahy kutoka kwake au ni mzushi tu.


Alipoulizwa maswali hayo Muhammad (s.a.w) alisema, "Nitakujibuni kesho" lakini hakusema, 'I nshaa-Allah'. Siku iliyofuata alikuwa bado hajapata wahy, hivyo walipokuja makafiri kusikiliza majibu, akawaambia waje siku iliyofuata. Walipokuja hakuwa na majibu. Hali ikaendelea hivyo kwa muda wa siku 15. Makafiri wakaanza kumkejeli na kumdhihaki. Muhammad (s.a.w) akahuzunika sana kwa kutopata wahy alioutazamia. Hatimaye Jibril (a.s) akamletea wahy akafahamishwa majibu ya maswali yote. Kule kuchelewa kuja kwa wahy kulikuwa ni fundisho kwake:


Wala usiseme kamwe kwa lolote lile kuwa: "Nitalifanya kesho." Isipokuwa (uongeze) Ishaa-Allah. Na umkumbuke Mola wako unaposahau, na useme "Asaa Mola wangu ataniongoza njia iliyo karibu zaidi na uongofu kuliko hii" (18:23-2 4)



Ingawa kuchelewa kwa kuja wahyi kulimsononesha sana Muhammad (s.a.w) ilikuwa ni ushahidi kuwa Qur-an haikutungwa na yeye. Laiti angelikuwa mtunzi wa Qur-an angeliyatoa majibu yale kesho yake ili kuepuka fedheha iliyompata.



Kuhusiana na hili la fikra za kimazezeta jambo la kuzingatia hapa ni kwamba Muhammad (s.a.w) aliulizwa maswali kuhusiana na matukio maalum,. Ni vigumu sana kuona jinsi ambavyo fikra za kimazezeta ya kidini zingeweza kumsaidia kujibu kwa usahihi maswali aliyoulizwa. Majibu ambayo yaliwatosheleza na kuwanyamazisha makafiri.
Na miongoni mwa mambo yanayojitokeza katika kisa hiki ni namna ulivyowasilishwa muda wa vijana waliokaa pangoni. Qur-an inasema: Na walikaa katika pango yao miaka mia tatu, na ongeza tisa. (18:25)



Kwa nini aya haikusema moja kwa moja "miaka mia tatu na tisa" na badala yake ikasema "mia tatu na ongeza tisa?" Hii ni kwasababu vijana hao walikaa miaka 300 kwa kufuata kalenda ya jua (solar calendar) na ni miaka 309 kwa kufuata kalenda ya kuandama mwezi (lunar calender). Sababu yake ni kuwa mwaka wa kuandama kwa miezi ni mfupi kwa siku 11 ukilinganishwa na ule wa jua. Hivyo 11 X 300/365 = 9. Yaani siku 11 mara 300 kugawanywa kwa 365 ni miaka 9. Hivyo basi madai kuwa mahesabu hayo sahihi yanatokana na kujidhania au mauzauza yaliyompanda Muhammad (s.a.w) hayana nguvu. Mfano mwingine tunaukuta katika sura ya 89 ya Qur-an ambayo ina aya inayoutaja mji wa kale sana wa Iram:


Je! Hukuona jinsi Mola wako alivyowafanya Adi, wa (mji wa) Iram, wenye majumba marefu marefu ambayo hawakuumbwa mfano wao katika miji (mingine) ." (89:6-8)
Jina la mji huu lilikuwa halijulikani vizuri hata wakati wa uhai wa Mtume (s.a.w). Kwa sababu hiyo kulikuwa na utatanishi mkubwa juu ya ni ipi Jiografia ya mji huo.
Hata hivyo utafiti uliochapishwa katika jarida la chama cha Jiografia huko Marekani liitwalo The National Geographic toleo la December 1978 umeonesha kuwa Iram ni jina la mji. Mwaka 1975 Dk. Paolo Mathiae wa chuo Kikuu cha Roma aligundua huko Syria maktaba ya kale sana iliyokuwa na vigae 15,000 vyenye maandishi. Miongoni mwa maelezo yaliyokuwamo katika vigae hivyo ilikuwa ni taarifa kuwa watu wa mji wa Ebla walikuwa wakifanya biashara na watu wa mji wa Iram.



Ni vigumu sana kuona ni kwa vipi fikra za kizezeta zingeweza kumwongoza Muhammad (s.a.w) kutoa taarifa sahihi juu ya majumba yaliyoharibiwa miaka 3,000 kabla yeye hajazaliwa! Isitoshe Qur-an imetamka katika sehemu kadhaa kuwa Muhammad na watu wake hawakuvijua baadhi ya visa vilivyotajwa katika Qur-an:


Hizi ni katika habari za ghaibu tunazokufunulia. Hukuwa ukizijua wewe, wala watu wako, kabla ya hii (Qur-an kuteremshwa). Hakika mwisho mwema ni wa wamchao Mwenyezi Mungu (11:49)



Yafaa kuzingatia hapa kuwa hakuna hata mtu mmoja aliyejitokeza na kusema, "Ewe Muhammad, hayo uyasemayo si kweli. Mimi ni Mwarabu kama wewe na nilizijua habari hizi kabla ya huu wahy wako. Si hivyo tu, bali pia kama Muhammad (s.a.w) angekuwa ndiye mtunzi wa Qur-an asingethubutu kuitamka aya hii, au kama angeitamka basi angekuwa amejitia katika patapotea ya hatari kabisa kwa sababu zifuatazo:



Kwanza, hata kama tukisema mathalan kuwa Muhammad (s.a.w) kwa hakika alizijua habari hizo kabla lakini hapa anasingizia tu, basi hapana shaka yeye hatakuwa mtu pekee anayezijua. Hivyo asingeweza kusema kwa ujasiri kiasi hiki juu ya kutokujua kwa wengine. Atakuwa na uhakika gani kuwa watu wote wengine hawazijui?


Pili, hata kama ni kweli kuwa watu wengine hawakujua habari hizo, maadui na wapinzani wake wangeweza kusingizia kuwa wao kwa hakika walikuwa wanazijua habari hizo hasa hasa ilivyokuwa kauli hiyo imetamkwa katika Qur-an baada ya kumaliza kukisimulia kisa chenyewe. Lakini pamoja na yote hayo hakuna mtu aliyeitumia fursa hiyo. Muhammad (s.a.w) angewezaje kujua kuwa hakuna mtu atakayeitumia fursa hiyo?




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 268


Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Nini maana ya Quran
Post hii inakwenda kukuambia maana ya Quran Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat an-Nas na surat al Falaq
Sura mbili hizi pia hujulikana kwa jina la al muawidhatain ambazo ni surat an Nas na surat al falaq. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA IDGHAM
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA
SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( Ω…Ω’). Soma Zaidi...

Mpangilio wa quran ni wa kipekee na uliotumia ujuzi mkubwa
Soma Zaidi...

AINA ZA MADA YAANI KUVUTA KWENYE USOMAJI WA QURAN: MADD (Al-Maddul-Far-’iy), Maddul-Jaaiz Al-Munfaswil, Maddul-Liyn,
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Maisha ya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 19. Hapa utajifunza maisha ya Mtume kabla ya utume. Soma Zaidi...

Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s.w)
(ii)Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s. Soma Zaidi...

Sababu za kshuka surat al Asr
Sura hii ni katika sura za kitawhidi sana. Maulamaa wanasema inatosha sura hii kuwa ni mawaidha. Imamu sharifu anasema kuwa sura hii inatosha kuwa muongozo… Soma Zaidi...

Fadhila za kusoma Quran na umuhimu wa kusoma Quran
Unazijua faida za kusoma Quran, na je ni faida gani utapata ukisoma Quran? Soma Zaidi...

Maudhui ya Qur-an na Mvuto wa Ujumbe Wake
Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al alaqa
Asbsb nuzul surat al alaqa, sababu za kushuka surat alaqa. Sura hii imeshuka Makka na ina aya 19. Ni sura ya 96 katika mpangilio wa Quran. Soma Zaidi...