image

Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:

(iii)Jinsi Mtume Muhammad (s.

Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:

(iii)Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:



Tumejifunza kuwa Allah (s.w) huwasiliana na wanaadamu kwa njia ya Wahyi (ufunuo) kwa kutumia njia za mawasiliano zifuatazo:
- Il-hamu.
- Kutumwa Malaika.
- Kuongeleshwa nyuma ya pazia.
- Maandishi (yaliyoandikwa tayari)
- Ndoto za kweli.



Qur-an ilishushwa kwa Mtume (s.a.w) kwa njia hii ya wahyi kupitia kwa Malaika Jibril.
Kuonesha kuwa Qur-an ni neno la Allah (s.w) na wala si tungo za Mtume Muhammad (s.a.w) ni ile hali aliyokuwa nayo wakati wa kupokea wahyi. Wakati wa mwanzo mwanzo wa kuanza kushushiwa wahyi Mtume (s.a.w) alikuwa akiyarudia haraka haraka yale aliyokuwa anasomewa na Malaika Jibril kwa wasi wasi kuwa atasahau. Ndipo Allah (s.w) akamtoa wasi wasi huo kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:


Usiutikise ulimi wako kwa (kuufanyia haraka) wahyi (unapoteremka. Wewe sikiliza tu. Usiseme kitu). Kwa hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha (kukukusanyia na kukusomesha). Wakati tunapokusomea, basi fuata kusomwa kwake. Kisha ni juu yetu kuubainisha (kukubainishia). (75:16-19)


Tutakusomesha (tutakusomea) wala hutasahau. Ila Akipenda Mwenyezi Mungu; Yeye anajua yaliyodhahiri na yaliyofichikana. (87:6-7)
Kwa hiyo kutokana na aya hizi Qur-an si maneno ya Mtume Muhammad (s.a.w) aliyoyatoa kichwani mwake. Kwani yangelitoka kichwani mwake asingelikuwa na wasi wasi wowote kuwa atakuja yasahau. Alikuwa na wasi wasi kwa sababu yeye akiwa ni Mtume wa Allah(s.w) alijua fika kuwa jukumu lake kubwa ni kuufikisha ujumbe wa Allah kwa watu kama ulivyo bila ya kupunguza au kuzidisha hata chembe.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1172


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

mafunzo ya TAJWID na imani ya dini ya kiislamu
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Wanaoongozwa na wasioongozwa na quran
Soma Zaidi...

Muhammad hakufundishwa quran na padri Bahira
Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat Dhuha
Sura hii imetermka Makkah na ina aya 11. Sura hii ni moja ya sura ambazo zimeshuka mwanzoni wakati ambapo Mtume ameanza kazi ya utume. Soma Zaidi...

Qur-an Kushuka Kidogo Kidogo kwa Kipindi cha Miaka 23:
Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MADD YAANI KUVUTA HERUFI KWENYE USOMAJI WA QURAN
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Quran si njozi za mvurugano alizoota Mtume Muhammad
(ii)Dai kuwa Qur-an ni zao la njozi za Mtume (s. Soma Zaidi...

DARSA ZA QURAN
Soma Zaidi...

fadhila za sura kwenye quran
FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka suratul al-quraysh na fadhila zake
SURAT AL-QURAYSH Sura hii ina majina mawili. Soma Zaidi...

quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...

fadhila za sura kwenye quran
FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya. Soma Zaidi...