(iii)Jinsi Mtume Muhammad (s.
(iii)Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:
Tumejifunza kuwa Allah (s.w) huwasiliana na wanaadamu kwa njia ya Wahyi (ufunuo) kwa kutumia njia za mawasiliano zifuatazo:
- Il-hamu.
- Kutumwa Malaika.
- Kuongeleshwa nyuma ya pazia.
- Maandishi (yaliyoandikwa tayari)
- Ndoto za kweli.
Qur-an ilishushwa kwa Mtume (s.a.w) kwa njia hii ya wahyi kupitia kwa Malaika Jibril.
Kuonesha kuwa Qur-an ni neno la Allah (s.w) na wala si tungo za Mtume Muhammad (s.a.w) ni ile hali aliyokuwa nayo wakati wa kupokea wahyi. Wakati wa mwanzo mwanzo wa kuanza kushushiwa wahyi Mtume (s.a.w) alikuwa akiyarudia haraka haraka yale aliyokuwa anasomewa na Malaika Jibril kwa wasi wasi kuwa atasahau. Ndipo Allah (s.w) akamtoa wasi wasi huo kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:
Usiutikise ulimi wako kwa (kuufanyia haraka) wahyi (unapoteremka. Wewe sikiliza tu. Usiseme kitu). Kwa hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha (kukukusanyia na kukusomesha). Wakati tunapokusomea, basi fuata kusomwa kwake. Kisha ni juu yetu kuubainisha (kukubainishia). (75:16-19)
Tutakusomesha (tutakusomea) wala hutasahau. Ila Akipenda Mwenyezi Mungu; Yeye anajua yaliyodhahiri na yaliyofichikana. (87:6-7)
Kwa hiyo kutokana na aya hizi Qur-an si maneno ya Mtume Muhammad (s.a.w) aliyoyatoa kichwani mwake. Kwani yangelitoka kichwani mwake asingelikuwa na wasi wasi wowote kuwa atakuja yasahau. Alikuwa na wasi wasi kwa sababu yeye akiwa ni Mtume wa Allah(s.w) alijua fika kuwa jukumu lake kubwa ni kuufikisha ujumbe wa Allah kwa watu kama ulivyo bila ya kupunguza au kuzidisha hata chembe.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Zijuwe sababu kuu za kushuka surat Al-Humazah katika quran
Soma Zaidi...(ii)Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza kuhusu hukumu ya Idh-har katika usomaji wa Quran.
Soma Zaidi...Al fiyl ni neno la Kiarabu lenye maana ya tembo. Sura hii inazungumziakisa cha jeshi lenye tembo. Jeshi hili lilikuwa na nia ya kuvunja al qaaba
Soma Zaidi...Kwa kuwa hakuna sababu mwalumu ikiyonukuliwa kuwa ndio chanzo cha kushushwa suravhii. Basi post hii itakujuza mambo ambayo huwenda hukuyajuwa kuhusu fadhika za surabhii na mengineyo.
Soma Zaidi...