picha

Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:

(iii)Jinsi Mtume Muhammad (s.

Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:

(iii)Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:



Tumejifunza kuwa Allah (s.w) huwasiliana na wanaadamu kwa njia ya Wahyi (ufunuo) kwa kutumia njia za mawasiliano zifuatazo:
- Il-hamu.
- Kutumwa Malaika.
- Kuongeleshwa nyuma ya pazia.
- Maandishi (yaliyoandikwa tayari)
- Ndoto za kweli.



Qur-an ilishushwa kwa Mtume (s.a.w) kwa njia hii ya wahyi kupitia kwa Malaika Jibril.
Kuonesha kuwa Qur-an ni neno la Allah (s.w) na wala si tungo za Mtume Muhammad (s.a.w) ni ile hali aliyokuwa nayo wakati wa kupokea wahyi. Wakati wa mwanzo mwanzo wa kuanza kushushiwa wahyi Mtume (s.a.w) alikuwa akiyarudia haraka haraka yale aliyokuwa anasomewa na Malaika Jibril kwa wasi wasi kuwa atasahau. Ndipo Allah (s.w) akamtoa wasi wasi huo kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:


Usiutikise ulimi wako kwa (kuufanyia haraka) wahyi (unapoteremka. Wewe sikiliza tu. Usiseme kitu). Kwa hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha (kukukusanyia na kukusomesha). Wakati tunapokusomea, basi fuata kusomwa kwake. Kisha ni juu yetu kuubainisha (kukubainishia). (75:16-19)


Tutakusomesha (tutakusomea) wala hutasahau. Ila Akipenda Mwenyezi Mungu; Yeye anajua yaliyodhahiri na yaliyofichikana. (87:6-7)
Kwa hiyo kutokana na aya hizi Qur-an si maneno ya Mtume Muhammad (s.a.w) aliyoyatoa kichwani mwake. Kwani yangelitoka kichwani mwake asingelikuwa na wasi wasi wowote kuwa atakuja yasahau. Alikuwa na wasi wasi kwa sababu yeye akiwa ni Mtume wa Allah(s.w) alijua fika kuwa jukumu lake kubwa ni kuufikisha ujumbe wa Allah kwa watu kama ulivyo bila ya kupunguza au kuzidisha hata chembe.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 3173

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

surat al mauun

SURATUL-MAM’UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat..

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat Ikhlas

Surat Ikhlas ni katika sura za kitawhid ambazo zilishuka miaka siku za mwanzoni mwa utume. Sura hii imekuja kujibu maswali mengi kuhusu Allah ikiwemo, Allah ni nani?

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa surat al qariah

Surat Al qariah, ni moja katika sura zilizochuka miaka ya mwanzoni mwa utume.

Soma Zaidi...
quran na sayansi

YALIYOMONENO LA AWALI1.

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya Tajwid, na ni ipi nafasi yake kwenye uislamu

Hapa utajifunza maana ya Tajwid kilugha na kisheria. Pia nitakujuza jukumu ya kusoma tajwid.

Soma Zaidi...
Makundi ya Id-ghamu katika usomaji wa Quran Tajwid

Kama tulivyoona kuwa id-ghamu ipo katika aina kuu mbili ambazo ni id-ghamu bighunnah na id-ghamu bighair ghumnah. Sasa hapa tutajifunza makundi mengine ya idhgamu.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al humazah

Sura hii inaonya vikali tabia ya kusengenya na kusambaza habari za uongo. Wameonywa vikali wenye tabia ya kujisifu kwa mali, kukusanya mali bila ya kuitolea zaka.

Soma Zaidi...
Nini maana ya Quran

Post hii inakwenda kukuambia maana ya Quran

Soma Zaidi...