Quran si maneno ya mwenye kifafa

Quran si maneno ya mwenye kifafa

(iv)Dai kuwa Qur-an ni zao la Mwenye Kifafa na Aliyepagawa na Shetani:



Waandishi kadhaa wa kikafiri katika maandishi yao wamedai bila kutoa ushahidi wowote unaotokana na historia kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa mwenye kifafa na mwenye kupagawa na Shetani na maneno yake alipokuwa katika hali ya ugonjwa ndiyo yaliyonukuliwa na kuunda Kitabu cha Qur-an!



Udhaifu:
Udhaifu wa dai hili tunaweza kuuona kwa kujiuliza maswali yafuatayo: Je, kifafa, ugonjwa mbaya kama tunavyoufahamu, umewahi kumtokea mtu katika historia ya mwanaadamu na bado akawa mtu mwenye kutoa sheria za kufuatwa na umati wa watu wengi zaidi ya robo ya dunia? Je, historia ya mwanaadamu imewahi kumshuhudia mgonjwa wa kifafa au mwenye kupagawa na shetani kuwa na hadhi na uwezo mkubwa kuliko mtu yeyote ulimwenguni kama ilivyokuwa kwa Mtume Muhammad (s.a.w)? Kama mgonjwa wa kifafa ndiye aliyeandika Qur-an, inakuwaje waandishi hodari wenye akili timamu na wanafalsafa wakubwa washindwe kuandika kitabu mithili ya angalau sura moja ya Qur-an na kukabili changa moto iliyotolewa na Qur-an karne nyingi zilizopita:



"Je! Ndiyo wanasema ameitunga? Sema: "Hebu (tungeni na nyie) mlete sura moja mfano wake na waiteni muwezao (kuwapata waje).- isipokuwa Mwenyezi Mungu - (wa kuwasaidieni) kama nyinyi mnasema kweli (kuwa haya ameyazua Muhammad)." (10:38)



Kitaalam inafahamika kuwa ugonjwa wa kifafa baada ya muda humfanya mgonjwa kuwa taahira (punguani). Pia ugonjwa wa kifafa humdhoofisha mgonjwa na hutisha wauguzaji na wenye kumuangalia mgonjwa wakati ameshikwa na kifafa. Hapana ushahidi wowote katika historia ya Mtume (s.a.w) ambayo iko bayana mno kuliko historia ya mtu yeyote, kuwa alikuwa mwenye kifafa au mwenye kupagawa na shetani.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 111

Post zifazofanana:-

Ni mali ipi inatakiwa kutolewa zaka?
Soma Zaidi...

HADITHI YA MVUVI NA JINI
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MVUVI NA JINI Hapao zamani kulikuwepo na mvuvi aliyekuwa masikini wenye watoto watatu na mke mmoja. Soma Zaidi...

KIJUWE KISUKARI CHANZO CHAKE, DALILI ZAKE NA KUKABILIANA NACHO
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Vituo vya kunuia ibada ya hija
Soma Zaidi...

DARSA ZA QURAN
Soma Zaidi...

uwanja wa burudani
Jifunze mengi kuhusu Afya, kuwa nasi kwenye makala hii hadi mwisho. Soma Zaidi...

dua ya kuomba jambo ufanikiwe
hii ni damna ya kuomba dua ukubaliwe, dua ya kuomba jambo ufanikiwe Soma Zaidi...

Hadithi ya kinyozi
Soma Zaidi...

vocabulary
Soma Zaidi...

VYAKULA VYA VITAMIN NA MAJI
Zitambue aina zote za vyakule na ufanye maamuzi yaliyo kuwa sahihi katika uandaaji wa chakula chako Soma Zaidi...

Vyakula vya vitamini C na faida zake
Soma Zaidi...

KAZI ZA MALAIKA
Malaika wamepewa kazi ya kumtumikia Allah(SW) kwa kumtukuza na kumtakasa, kama wanavyosema wenyewe:Hakuna yoyote miongoni mwetu ila anapo mahali pake mahususi. Soma Zaidi...