Hapa nitakufindisha faida za kusoma quran kwa Tajwid.
Fadhila na umuhimu wa tajwid.
Kwa hakika tunatambuwa sasa kuwa elimu ya tajwid ina umuhimu mkubwa kwenye umma wetu wa kiislamu. Kwani msomaji kama hatachunga kisomo anaweza kubadilisha maana ya qurani kabisa. Hivyo elimu ya tajwid inaweza kuwa ni msingi wa kuchunga maana ya matamshi ya qurani katika usomaji.
Tunahitajia imamu mwenye kiraa kizuri kwa sauti pia awe anajuwa tajwid na anaitumia ipasavyo. Amesema Mtume (s.a.w): Kutoka kwa Abu Mas’uud Al-Answaariyy ( رضي لله عنه ) amesema: Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) amesema: ((Awaswalishe watu yule mwenye kujua kusoma zaidi Kitabu cha Allaah na wakiwa katika kusoma wako sawa, basi mwenye ujuzi zaidi wa Sunnah, na wakiwa kwenye Sunnah wako sawa, basi aliyetangulia Hijrah, na wakiwa katika hijrah wako sawa, basi mkubwa wao kwa umri, wala asiswalishe mtu (mwengine) katika nyumba yake wala katika mamlaka yake wala asikae mahali pake pa heshima isipokuwa kwa idhini yake))
Halikadhalika watu hupenda kusikiliza kiraa cha mtu anayesoma vizuri kwa sauti na kuchunga hukumu za tajwid. Na hivi pia ndivyo Mtume (s.a.w0 anvyotuambia:Kutoka kwa Abu Muwsaa Al-’Ash’arriy ( رضي لله عنه ) kwamba Mtume kamwambia: ((Ungeliniona jana nilivyokuwa nakusikiliza kisomo chako. Hakika umepewea mizumari miongoni mwa mizumari ya aila ya (Daawuwd)
Msomaji wa qurani atakukuwa pamoja na malika wema wenye kuandika. Imetoka kwa ‘Aaishah ( رضي لله عنها ) kwamba Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) amesema: ((Yule aliyekuwa hodari wa kusoma Qur-aan atakuwa pamoja na Malaika Waandishi [wa Allaah] watukufu wema, na yule ambaye anaisoma Qur-aan kwa mashaka na huku anajitahidi kwa kudodosa atapata ujira mara mbili)).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
waqfu ni misimamo ambapo msomaji wa Quran anaruhusiwa kusimama, kuhema au kumeza mate. Na ibtidai ni kuanza baada ya kutoka kwenye waqf
Soma Zaidi...Aina za idgham ni idgham al mutamathilain, na idgham al mutajanisain
Soma Zaidi...Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo
Soma Zaidi...SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza kuhusu maana ya id-ghamu na aina zake.
Soma Zaidi...SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( مْ).
Soma Zaidi...