Faida za kujuwa Quran tajwid

Hapa nitakufindisha faida za kusoma quran kwa Tajwid.

Fadhila na umuhimu wa tajwid.
Kwa hakika tunatambuwa sasa kuwa elimu ya tajwid ina umuhimu mkubwa kwenye umma wetu wa kiislamu. Kwani msomaji kama hatachunga kisomo anaweza kubadilisha maana ya qurani kabisa. Hivyo elimu ya tajwid inaweza kuwa ni msingi wa kuchunga maana ya matamshi ya qurani katika usomaji.



Tunahitajia imamu mwenye kiraa kizuri kwa sauti pia awe anajuwa tajwid na anaitumia ipasavyo. Amesema Mtume (s.a.w): Kutoka kwa Abu Mas’uud Al-Answaariyy ( رضي لله عنه ) amesema: Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) amesema: ((Awaswalishe watu yule mwenye kujua kusoma zaidi Kitabu cha Allaah na wakiwa katika kusoma wako sawa, basi mwenye ujuzi zaidi wa Sunnah, na wakiwa kwenye Sunnah wako sawa, basi aliyetangulia Hijrah, na wakiwa katika hijrah wako sawa, basi mkubwa wao kwa umri, wala asiswalishe mtu (mwengine) katika nyumba yake wala katika mamlaka yake wala asikae mahali pake pa heshima isipokuwa kwa idhini yake))

 

Halikadhalika watu hupenda kusikiliza kiraa cha mtu anayesoma vizuri kwa sauti na kuchunga hukumu za tajwid. Na hivi pia ndivyo Mtume (s.a.w0 anvyotuambia:Kutoka kwa Abu Muwsaa Al-’Ash’arriy ( رضي لله عنه ) kwamba Mtume kamwambia: ((Ungeliniona jana nilivyokuwa nakusikiliza kisomo chako. Hakika umepewea mizumari miongoni mwa mizumari ya aila ya (Daawuwd)


Msomaji wa qurani atakukuwa pamoja na malika wema wenye kuandika. Imetoka kwa ‘Aaishah ( رضي لله عنها ) kwamba Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) amesema: ((Yule aliyekuwa hodari wa kusoma Qur-aan atakuwa pamoja na Malaika Waandishi [wa Allaah] watukufu wema, na yule ambaye anaisoma Qur-aan kwa mashaka na huku anajitahidi kwa kudodosa atapata ujira mara mbili)).

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1290

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Quran Tafsiri kwa Kiswahili

Tafsiri ya quran kw akiswahili, imeandikw ana Shekh Ali Muhsin al-Barwani

Soma Zaidi...
Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.

Soma Zaidi...
Sababu za kshuka surat al Asr

Sura hii ni katika sura za kitawhidi sana. Maulamaa wanasema inatosha sura hii kuwa ni mawaidha. Imamu sharifu anasema kuwa sura hii inatosha kuwa muongozo…

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat Ikhlas

Surat Ikhlas ni katika sura za kitawhid ambazo zilishuka miaka siku za mwanzoni mwa utume. Sura hii imekuja kujibu maswali mengi kuhusu Allah ikiwemo, Allah ni nani?

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al qadir

Asbab nuzul surat al qadi. Hii ni sura ya 97 katika mpangilio wa mashaf. Surat al qadir imeteremshwa Madina na ina aya 5.

Soma Zaidi...