Hapa nitakufindisha faida za kusoma quran kwa Tajwid.
Fadhila na umuhimu wa tajwid.
Kwa hakika tunatambuwa sasa kuwa elimu ya tajwid ina umuhimu mkubwa kwenye umma wetu wa kiislamu. Kwani msomaji kama hatachunga kisomo anaweza kubadilisha maana ya qurani kabisa. Hivyo elimu ya tajwid inaweza kuwa ni msingi wa kuchunga maana ya matamshi ya qurani katika usomaji.
Tunahitajia imamu mwenye kiraa kizuri kwa sauti pia awe anajuwa tajwid na anaitumia ipasavyo. Amesema Mtume (s.a.w): Kutoka kwa Abu Mas’uud Al-Answaariyy ( رضي لله عنه ) amesema: Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) amesema: ((Awaswalishe watu yule mwenye kujua kusoma zaidi Kitabu cha Allaah na wakiwa katika kusoma wako sawa, basi mwenye ujuzi zaidi wa Sunnah, na wakiwa kwenye Sunnah wako sawa, basi aliyetangulia Hijrah, na wakiwa katika hijrah wako sawa, basi mkubwa wao kwa umri, wala asiswalishe mtu (mwengine) katika nyumba yake wala katika mamlaka yake wala asikae mahali pake pa heshima isipokuwa kwa idhini yake))
Halikadhalika watu hupenda kusikiliza kiraa cha mtu anayesoma vizuri kwa sauti na kuchunga hukumu za tajwid. Na hivi pia ndivyo Mtume (s.a.w0 anvyotuambia:Kutoka kwa Abu Muwsaa Al-’Ash’arriy ( رضي لله عنه ) kwamba Mtume kamwambia: ((Ungeliniona jana nilivyokuwa nakusikiliza kisomo chako. Hakika umepewea mizumari miongoni mwa mizumari ya aila ya (Daawuwd)
Msomaji wa qurani atakukuwa pamoja na malika wema wenye kuandika. Imetoka kwa ‘Aaishah ( رضي لله عنها ) kwamba Mtume ( صلى لله عليه وسلم ) amesema: ((Yule aliyekuwa hodari wa kusoma Qur-aan atakuwa pamoja na Malaika Waandishi [wa Allaah] watukufu wema, na yule ambaye anaisoma Qur-aan kwa mashaka na huku anajitahidi kwa kudodosa atapata ujira mara mbili)).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
(i)Mtume Muhammad (s.
Soma Zaidi...Zijuwe sababu kuu za kushuka surat Al-Humazah katika quran
Soma Zaidi...2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kufundisha fadhila na faida za kusoma Alhamdu.
Soma Zaidi...Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa
Soma Zaidi...SURATUL-KAUTHAR Imeteremshwa maka, na sura hii imeshuka kwa sababu al-aAs ibn Waail.
Soma Zaidi...Sura hii ni katika sura za mwisho kushuka, huwendakuwa ndio ya mwisho kabisa. Masahaba waliamini kuwa sura hii imetabiri kifo cha Mtume S.A.W
Soma Zaidi...