picha

Quran si maneno ya shetani

Quran si maneno ya shetani

(v) Dai kuwa Qur-an ni aya za Shetani



Katika mwaka 1988 Salman Rushdie, Muingereza mwenye asili ya kihindi, aliandika kitabu chake alichokiita "Satanic Verses" (yaani aya za Shetani) ambamo amemtukana Mtume (s.a.w), Uislamu na Qur-an kwa kuiita "aya za Shetani."



Katika kitabu chake hicho, Rushdie amedai kuwa hapakuwa na wahy wowote uliomshukia Muhammad (s.a.w) bali alikuwa akidai tu kuwa anashushiwa Wahy. Aidha Rushdie anadai kuwa Muhammad (s.a.w) alikuwa ni mtu aliyekuwa akifuata matashi yake mwenyewe akiongozwa na shetani na kwa hiyo yote yaliyomo ndani ya Qur-an ni maneno ya shetani.



Pia Rushdie katika kitabu chake hicho amedai kuwa Mtume (s.a.w) hakuwa na uwezo wa kutofautisha wahy kutoka kwa Malaika au wahy kutoka kwa shetani.

Vile vile Salman Rushdie amedai kuwa Mtume (s.a.w) hakuwa na kumbukumbu ya kile alichowasomea waandishi wake na wala hakuweza kutambua hata kile ambacho waandishi hao wamekiongeza kichini-chini. Amepiga mfano wa mwandishi mmoja wa Kifursi kuwa alisomewa na Mtume aandike "Mwenye kusikia, mwenye kujua kila kitu" lakini yeye akaandika "Mwenye kujua na Mwenye hikma" na Mtume hakung'amua mabadiliko hayo!



Udhaifu wa madai ya Salman Rushdie
Kwanza,
ujumbe wa Qur-an umeteremshwa ili kumtoa binaadamu kutokana na hadaa zote za shetani. Shetani katika Qur-an ameelezwa wazi pamoja na vitimbi vyake na watu anaowatumia ili wanaadamu wasiweze kupotezwa naye. Hebu turejee aya chache zifuatazo:


"Na namna hii tumemfanyia kila Nabii maadui, (nao ni) mashetani katika watu na (mashetani) katika majini. Baadhi yao wanawafunulia wenzao maneno ya kupamba pamba ili kuwadanganya. Na Mola wako angelipenda wasingelifanya hayo. Basi waache na uongo wao." (6:112)


"Enyi wanaadamu! Shetani (Iblisi) asikutieni katika matata, kama alivyowatoa wazee wenu katika Pepo akawavua nguo zao ili kuwaonesha tupu zao. Hakika yeye pamoja na kabila yake wanakuoneni na hali ya kuwa hamuwaoni." Bila shaka sisi tumewajaalia mashetani kuwa marafiki wa wale wasioamini." (7:2 7)



"Kwa yakini Shetani ni adui yenu, basi mfanyeni adui (yenu; kwa hivyo msimtii) kwani anaita (analiita) kundi lake liwe katika watu wa Motoni." (35:6)
Kama Qur-an ni maneno ya Shetani, inakuwaje tena shetani mwenyewe ajidhihirishe kiasi hicho ili watu wamkimbie?



Pili, Allah (s.w) anasema kuwa laiti ingelikuwa hii Qur-an inatoka kwa mwingine asiye kuwa Yeye au kama ingekuwa ina waandishi wawili tofauti ambao wana malengo yanayopingana mmoja anavutia kwenye mema na mwingine kwenye uovu pangelikuwa na khitilafu nyingi (Qur-an 4:82). Je, uko mgongano wowote katika maneno ya Qur-an? Haupo, bali maneno yote ya Qur-an ni yenye kusadikishana. Hivyo haiwezekani Qur-an kuwa na mchanganyiko wa maneno ya shetani na ya Allah (s.w) kwa pamoja.



Tatu, Qur-an yenyewe imekataa kuwa Qur-an si maneno ya shetani."Wala hii si kauli ya shetani aliyefukuzwa (katika rehma za Mwenyezi Mungu.) (81:25)



Nne, Sote tunamfahamu shetani kuwa ni kiumbe dhaifu pamoja na kuwa hatumuoni. Sasa ikiwa shetani ameleta maneno na ujumbe mzito uliomo ndani ya Qur-an, kwanini na mashetani wengine nao hawakai pamoja kujibu zile changamoto zilizotolewa? "Mahound" kama alivyomwita Rushdie ni shetani mmoja tu, je pamekuwa na uzito gani kwa wanaadamu pamoja na majini wakichanganyika kuleta mfano wa angalau sura moja ya Qur-an? Qur-an imetoa changamoto hiyo tangu kuanza kushuka kwake:


"Sema "Hata wakijikusanya watu (wote) na majini kuleta mfano wa hii Qur-an basi hawangaliweza kuleta mfano wake, hata kama watasaidiana (vipi) wao kwa wao." (17:88)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2246

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 ai web app   

Post zinazofanana:

Sababu za kushuka surat al qadir

Asbab nuzul surat al qadi. Hii ni sura ya 97 katika mpangilio wa mashaf. Surat al qadir imeteremshwa Madina na ina aya 5.

Soma Zaidi...
MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al alaqa

Asbsb nuzul surat al alaqa, sababu za kushuka surat alaqa. Sura hii imeshuka Makka na ina aya 19. Ni sura ya 96 katika mpangilio wa Quran.

Soma Zaidi...
Asbab nuzul surat at Tin, Sababu za kushuka surat at Tin (watin wazaitun)

Post hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa surat at Tin (watin wazaitun).

Soma Zaidi...
quran na sayansi

YALIYOMONENO LA AWALI1.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MADD YAANI KUVUTA HERUFI KWENYE USOMAJI WA QURAN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Je, mtu anaweza kusoma quran akiwa amelala?

Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet

Soma Zaidi...