Saratul-asr 103
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
- Suratul-A’sr (103): Imeteremshwa Makkah, Ina Aya Tatu.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.
- Naapa kwa zama (zako Ewe Nabii Muhammad!).
- Kuwa wanaadamu yuko katika hasara.
- Isipokuwa wale walioamini na wakafanya vitendo vizuri na wakausiana (kufuata) haki na wakausiana (kushikamana) na subira.
Mafunzo kwa Ufupi.
- Mwenyezi Mungu huapia kitu au kiumbe chochote kinachofahamika ili kutoa uthibitisho kwa kile anachoapia.
- Muumini haruhusiwi kuapa kwa kiumbe chochote isipokuwa kwa jina la Mwenyezi Mungu peke yake.
- Wakati (muda) ni rasilimali muhimu sana inayotakiwa kutumiwa kwa uangalifu mkubwa.
- Imani ya kweli huthibitishwa katika vitendo vizuri.
- Uislamu sio dini ya ubinafsi, hivyo ni lazima watu wausiane katika kufanya wema na kufuata haki.
- Subra ni nyenzo muhimu sana na ya pekee katika kuweza kuusimamisha Uislamu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 web hosting 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 ai web app
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 web hosting 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
namna quran inavyogawanya mirathi na wanaorithi pamoja na mafungu yao
Qur-an inavyogawa MirathiMgawanyo wa mirathi umebainishwa katika Qur-an kama ifuatavyo:Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Mwanamume apate sawa na sehemu ya wanawake wawili.
Soma Zaidi...As-Sab nuzul
Sababu za kuteremshwa baadhi ya sura Katika darsa hii tutaangalia sababu za kushuka kwa aya na sura ndani ya quran.
Soma Zaidi...Dai kuwa Muhammad (s.a.w) alitunga Qur-an ili kuleta Umoja na Ukombozi wa Waarabu:
(vii)Dai kuwa Muhammad (s.
Soma Zaidi...