- Suratul-A’sr (103): Imeteremshwa Makkah, Ina Aya Tatu.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.
- Naapa kwa zama (zako Ewe Nabii Muhammad!).
- Kuwa wanaadamu yuko katika hasara.
- Isipokuwa wale walioamini na wakafanya vitendo vizuri na wakausiana (kufuata) haki na wakausiana (kushikamana) na subira.
Mafunzo kwa Ufupi.
- Mwenyezi Mungu huapia kitu au kiumbe chochote kinachofahamika ili kutoa uthibitisho kwa kile anachoapia.
- Muumini haruhusiwi kuapa kwa kiumbe chochote isipokuwa kwa jina la Mwenyezi Mungu peke yake.
- Wakati (muda) ni rasilimali muhimu sana inayotakiwa kutumiwa kwa uangalifu mkubwa.
- Imani ya kweli huthibitishwa katika vitendo vizuri.
- Uislamu sio dini ya ubinafsi, hivyo ni lazima watu wausiane katika kufanya wema na kufuata haki.
- Subra ni nyenzo muhimu sana na ya pekee katika kuweza kuusimamisha Uislamu
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0