Lugha ya Qur-an:
Lugha iliyotumika katika Qur-an ni Kiarabu sanifu kama tu navyoj ifu nza katika Qur-an yenyewe:
"Na namna hii tumekufunulia Qur-an kwa Kiarabu ili uwaonye watu wa Makka na walio pembezoni mwake. Na uwaonye siku ya mkutano, siku isiyo na shaka. Kundi moja litakuwa Peponi na kundi jingine Motoni " (42:7)
Kwa nini Qur-an Imeshushwa kwa Lugha ya Kiarabu?
Walimwengu walio wengi wakiwemo baadhi ya Waislamu wanaitakidi kuwa lugha ya Kiislamu ni Kiarabu na Uislamu ni dini ya Waarabu. Bila shaka mawazo haya yamejitokeza kutokana na kutoujua Uislamu kwa upeo wake. Uislamu ni Dini ya Walimwengu wote wa nyakati zote na ni Dini iliyofundishwa na Mitume wote. Je, Mitume wote walikuwa Waarabu au watu wote waliolinganiwa na Mitume hao na kuwafuata walikuwa Waarabu? Bila shaka jibu litakuwa "hapana". Bali tunajifunza katika Qur-an yenyewe kuwa Allah (s.w) amewajaalia walimwengu kuzungumza lugha mbali mbali na ni katika ishara ya Uungu wake na utukufu wake.
"Na katika Ishara zake (zinazoonyesha uwezo wake) ni kuumba mbingu na ardhi, na kuhitilafiana lugha zetu na rangi zenu. Kwa yakini katika haya zimo ishara kwa wenye ujuzi." (3 0:22)
Kwa nini Qur-an imeshushwa kwa lugha ya Kiarabu? Jibu lake linapatikana ndani ya Qur-an yenyewe:
"Na hatukumpeleka Mtume yeyote isipokuwa kwa lugha ya watu wake ili apate kuwabainishia. Kisha, Mwenyezi Mungu anamuacha kupotea amtakaye (kwa kuwa hataki kufuata ujumbe uliomfikia wazi wazi) na humuongoza amtakaye. Naye ni Mwenye nguvu na Mwenye Hekima." (14:4)
Aya hii inatufahamisha kuwa kila Mtume alishushiwa Wahyi kwa lugha ya watu wake ili yeye mwenyewe apate kuwabainishia vizuri na wao wapate kumuelewa vizuri. Kwa kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa Mwarabu wa kabila la Kiquraishi na kwa kuwa Maquraish na Waarabu kwa ujumla ndio watu wake wa mwanzo kuwalingania Uislamu ili wamsaidie kuufikisha ulimwengu mzima. Qur-an ilibidi ishushwe kwa lugha ya Kiarabu cha Kiquraish kilichokuwa fasaha kuliko vilugha vyote vya Kiarabu. Watu wake wasingemuelewa kabisa kama Mtume (s.a.w) angewalignania kwa lugha isiyokuwa ya Kiarabu:
"Na lau kama tungaliifanya Qur-an lugha isiyo ya Kiarabu wangelisema: Kwa nini aya zake hazikupambanuliwa? Lo! Lugha isiyokuwa ya Kiarabu na (Mtume) Mwarabu! (Mambo gani hayo)? " (41:44).
"Na lau tungaliiteremsha juu ya mmoja wa wasiokuwa Waarabu, na akawasomea (kwa ufasaha) wasingalikuwa wenye kuamini." (26:198-199)
Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa:
(i)Ni desturi ya Allah (s.w) kumtuma mjumbe wake kwa lugha ya watu wake anaowafikishia.
(ii)Qur-an imeteremshwa kwa lugha ya Kiarabu kwa kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa Mwarabu na wale aliowalingania mara ya kwanza walikuwa ni Waarabu.
(iii)Waarabu wa mwanzo kulinganiwa Uislamu na Mtume (s.a.w) wasingeliukubali ujumbe kama Mtume asingelikuwa Mwarabu na kama angelingania kwa lugha nyingine isiyokuwa ya Kiarabu.
(iv)Kama Mtume (s.a.w) angelingania kwa lugha nyingine isiyokuwa Kiarabu, ujumbe wake usingelifahamika na watu wake wasingelazimika kuufuata kwa kuwa hawauelewi.
Umeionaje Makala hii.. ?
ASBAB NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN Quran imeteremka kwa muda wa miaka 23 kidogokido.
Soma Zaidi...Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo
Soma Zaidi...Hapa utajifunza kuhusu maana ya id-ghamu na aina zake.
Soma Zaidi...Asbab nuzul surat al qadi. Hii ni sura ya 97 katika mpangilio wa mashaf. Surat al qadir imeteremshwa Madina na ina aya 5.
Soma Zaidi...Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...(vii)Dai kuwa Muhammad (s.
Soma Zaidi...