Uthibitisho kuwa quran ni maneno ya Allah kutokana na Historia (Hadith)

Uthibitisho kuwa quran ni maneno ya Allah kutokana na Historia (Hadith)

(b)Uthibitisho kutokana na Historia (Hadith)



Historia ya kushuka Qur-an na namna Mtume (s.a.w) alivyoipokea ni ushahidi mwingine unaotuthibitishia kuwa Qur-an si kitabu alichokitunga Muhammad (s.a.w). Kuna maelezo kadhaa ya kihistoria tunayojifunza katika Hadith juu ya namna Mtume (s.a.w) alivyoipokea Qur-an. Hebu turejee hadithi zifuatazo:



(1)Hadithi ya bibi Aysha (r.a) iliyopokelewa na Imamu Bukhari inatufahamisha namna Mtume (s.a.w) alivyopokea wahyi wa kwanza wa Qur-an alipokuwa katika pango la Jabal Hira. Kama tulivyojifunza katika hadithi hiyo Mtume (s.a.w) alistushwa sana na tukio lile la kujiwa na Malaika Jibril (a.s) na kumuamrisha kusoma kinyume na uwezo wake. Tukio lile lilimhofisha sana Mtume (s.a.w) na kumfanya arejee nyumbani kwake akiwa anatetemeka. Tukio la Jabal Hira ni ushahidi mwingine tosha kuwa Qur-an si maneno ya Muhammad (s.a.w) bali ni ujumbe kutoka kwa Allah (s.w) uliofikishwa kwake kwa njia ya wahyi kupitia kwa Malaika Jibril.



(2)Mtume (s.a.w) alikuwa akibadilika haiba yake na kutokwa na jasho wakati wa kupokea wahyi kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:
Bibi aysha (r.a) amesimulia: Kwa hakika nimemuona Mtume akiteremshiwa wahyi siku ya baridi kali na baada ya kumaliza kile kipindi cha kuteremshiwa wahyi alimininikwa na jasho jingi kichwani mwake." (Malik)



Amesimulia Aysha (r.a), "Al-Harith bin Hisham (r.a) alimuuliza Mtume wa Allah, 'Ee mtume wa Allah! Ni vipi wahyi unakuja?' Mtume wa Allah alijibu, "Wakati mwingine ulifunuliwa kwangu kwa sauti mithili ya mlio wa kengele, wahyi ulioletwa kwa namna hii ulikuwa mgumu sana kuliko aina nyingine zote (za wahyi), kisha hali hii ilikwisha baada ya kukidhibiti kile kilichofunuliwa. Wakati mwingine Malaika


(Jibril) alikuja katika umbile la binaadamu na kuzungumza nami, ambapo nilikidhibiti (nilikichukua) chochote kile alichosema." Aysha (r.a) aliendelea kusema: Hakika nilimuona Mtume (s.a.w) wakati anateremshiwa wahyi siku ya baridi kali na kuona jasho likitiririka usoni mwake." (Bukhari)
Hadithi hizi nazo zinatuthibitishia kuwa Qur-an si utunzi wa Muhammad (s.a.w) kabisa,bali ni ujumbe wa Allah (s.w) uliopitia kwake kwa njia ya wahy.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2326

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 web hosting    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

WAQFU WAL-IBTIDAAI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al bayyinah

Asbab nuzul surat al bayyinh. Sura hii imeteremka Madina na ina aya nane.

Soma Zaidi...
Kwa nini quran ilishuka kidogo kidogo?

Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo

Soma Zaidi...
ASBAB-NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN

ASBAB NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN Quran imeteremka kwa muda wa miaka 23 kidogokido.

Soma Zaidi...
IDGHAAM KATIKA LAAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za Quran kuwa mwongozo sahihi wa maisha ya mwanadamu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al Mauun

Sura hii ni katika sura ambazo zinahitaji kusomwa kwa mazingatio sana. Wanaoswali bila ya kuzingatia swala zao, wameonywa vikali sana. Wanaowatesa na kuwanyanyasa mayatima wameonywa vikali. Wanaowanyima wenye haja na masikini huku wakiwakaripia nakuwasem

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa surat al-Fiil

SURAT AL-FIILSura hii imeteremshwa Makkah na ina Aya Sita pamoja na Basmallah.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa surat al qariah

Surat Al qariah, ni moja katika sura zilizochuka miaka ya mwanzoni mwa utume.

Soma Zaidi...