Quran na sayansi

3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran??

uran na sayansi

3; Mchujo wa maji dhalili
Katika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha ya kuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalili na pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran

‘ ’Ambaye ametengeneza umbo la kila kitu, na akaanzisha umbo la mwanadamukwa udongo. Na kisha akakifanya kizazi chake kwa mchujo wa maji yaliyo madhalili ’ ’[32:7-8]
‘je ! hatukukuumbeni kwa maji yaliyo madhalili? ’ ’ [77:20]

kwa ufupi matumizi ya neno sulala kwenye aya hii yanatupa picha hilisi kuwa sio maji yote yalitumika katika utungaji wa mimba bali kulifanyika mchujo wa majimaji hayo. Yaani ni sawa na kusema kuwa sio mbegu zote zilizomo kwenye majimaji ya manii zilitumika katika utungaji wa mimba bali mmajimaji haya ya manii yalichujwa na mengine kutumika na mengine kuachwa. Mchujo huu tukakuja uona vizuri hapo chini.

Uthibitisho wa sayansi
Sayansi inathibitisha kuwa sio kiasi chote cha mbegu za kiume yaan sperm hutumika katika utungaji wa mimba bali kiwango kidogo sana ndo hutumika kama tutakavyoona;-

1; sayansi inathibitisha kuwa manii ni mchanganyiko wa majimaji yapatikanayo katika tezi na mbegu za kiume zinazopatikana kwenye korodani. 95% ya manii ni majimaji hayo na 2% ni mbegu yaani sperm. Lakini katika utungaji wa mimba mbegu pekeyake ndo hutumika yaani katika kukutana kwa mbegu na yai majimaji mengine yanabakia pembeni na mbegu pekee ndo huhitajika katika utungaji wa mimba. Hivyo huu ni mchujo wa majimaji hayo

2; sayansi imegunduwa pia katika ejaculationmoja mwanaume hutoa mbegu zifikazo milioni 250- 300 lakini katika utungaji wa mimba mbegu moja tuu ndo hutumika vinginevyo chance ya kutumika mbili ipo lakini ni ndogo sana kwa baadhi ya mimba za mapacha. Huu bila shaka nao ni mchujo wa majimaji hayo.

3; katika tumbo la mama sehemu inayohusika katika utungaji wa mimba huwa na hali ya asidi hivyo hali hii huzifanya zile mbegu zilizo dhoofika kufa na kubakia zile zenye nguvu ambazo ndo zitakwenda kuminyana katika utungaji wa mimba. Hivyo hali hii pia inatupa picha jinsi mchujo huu unavyozidi kufanyika.

4; wakati mamilioni ya mbegu za kiume spermatozoansyanapokutana na yai huminyanakulilainisha na kupata nafasi ya kuingia ndani ili nuclear ya mbegu ikakutane na ile ya yai yaan ovum. Katika kiminyano hiki mbegu ya kwanza ikibahatika kuingia yai linatengeneza utando mgumu ambao utazuia mbegu nyingine kuingia. Hivyo hapa tunazidi kupatapicha zaidi jinsi mchujo huu unavyoendelea kufanyika.

Kwa kumalizia matumizi ya neno la kiarabu sulala limesaidia kutupa picha halisi ya kuwa majimaji haya yalichujwa kwa namna mbalimbali na kupata sample moja.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 678

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

HUKUMU ZA QALQALA

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.

Soma Zaidi...
Kwa nini quran ilishuka kidogo kidogo?

Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo

Soma Zaidi...
Maana ya Idgham na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Aina za idgham ni idgham al mutamathilain, na idgham al mutajanisain

Soma Zaidi...
sura ya 11

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Makundi ya Id-ghamu katika usomaji wa Quran Tajwid

Kama tulivyoona kuwa id-ghamu ipo katika aina kuu mbili ambazo ni id-ghamu bighunnah na id-ghamu bighair ghumnah. Sasa hapa tutajifunza makundi mengine ya idhgamu.

Soma Zaidi...
Tofauti kat ya sura za Maka na Madina

Sura za Makka na Madina Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina.

Soma Zaidi...
Ni ipi aya ya mwisho kushuka katika Quran?

Maulamaa katika elimu ya Quran wametofautiana juu ya aya ya mwisho kushuka. Hata hivyo hapa nitakutajia ambayo imependekezwa zaidi

Soma Zaidi...