Quran na sayansi

3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran??

uran na sayansi

3; Mchujo wa maji dhalili
Katika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha ya kuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalili na pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran

‘ ’Ambaye ametengeneza umbo la kila kitu, na akaanzisha umbo la mwanadamukwa udongo. Na kisha akakifanya kizazi chake kwa mchujo wa maji yaliyo madhalili ’ ’[32:7-8]
‘je ! hatukukuumbeni kwa maji yaliyo madhalili? ’ ’ [77:20]

kwa ufupi matumizi ya neno sulala kwenye aya hii yanatupa picha hilisi kuwa sio maji yote yalitumika katika utungaji wa mimba bali kulifanyika mchujo wa majimaji hayo. Yaani ni sawa na kusema kuwa sio mbegu zote zilizomo kwenye majimaji ya manii zilitumika katika utungaji wa mimba bali mmajimaji haya ya manii yalichujwa na mengine kutumika na mengine kuachwa. Mchujo huu tukakuja uona vizuri hapo chini.

Uthibitisho wa sayansi
Sayansi inathibitisha kuwa sio kiasi chote cha mbegu za kiume yaan sperm hutumika katika utungaji wa mimba bali kiwango kidogo sana ndo hutumika kama tutakavyoona;-

1; sayansi inathibitisha kuwa manii ni mchanganyiko wa majimaji yapatikanayo katika tezi na mbegu za kiume zinazopatikana kwenye korodani. 95% ya manii ni majimaji hayo na 2% ni mbegu yaani sperm. Lakini katika utungaji wa mimba mbegu pekeyake ndo hutumika yaani katika kukutana kwa mbegu na yai majimaji mengine yanabakia pembeni na mbegu pekee ndo huhitajika katika utungaji wa mimba. Hivyo huu ni mchujo wa majimaji hayo

2; sayansi imegunduwa pia katika ejaculationmoja mwanaume hutoa mbegu zifikazo milioni 250- 300 lakini katika utungaji wa mimba mbegu moja tuu ndo hutumika vinginevyo chance ya kutumika mbili ipo lakini ni ndogo sana kwa baadhi ya mimba za mapacha. Huu bila shaka nao ni mchujo wa majimaji hayo.

3; katika tumbo la mama sehemu inayohusika katika utungaji wa mimba huwa na hali ya asidi hivyo hali hii huzifanya zile mbegu zilizo dhoofika kufa na kubakia zile zenye nguvu ambazo ndo zitakwenda kuminyana katika utungaji wa mimba. Hivyo hali hii pia inatupa picha jinsi mchujo huu unavyozidi kufanyika.

4; wakati mamilioni ya mbegu za kiume spermatozoansyanapokutana na yai huminyanakulilainisha na kupata nafasi ya kuingia ndani ili nuclear ya mbegu ikakutane na ile ya yai yaan ovum. Katika kiminyano hiki mbegu ya kwanza ikibahatika kuingia yai linatengeneza utando mgumu ambao utazuia mbegu nyingine kuingia. Hivyo hapa tunazidi kupatapicha zaidi jinsi mchujo huu unavyoendelea kufanyika.

Kwa kumalizia matumizi ya neno la kiarabu sulala limesaidia kutupa picha halisi ya kuwa majimaji haya yalichujwa kwa namna mbalimbali na kupata sample moja.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 699

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Sababu za kushuka surat Al-Kawthar

Sura hii ni miongoni mwa Sura fupi sanya huwenda ndiosura yenye aya chache kuliko sura zote katika Quran.

Soma Zaidi...
Hukumu ya Ikhfau katika tajwid

Ikh-fau ni moja ya hukumu za nun sakina na tanwin kwenye hukumu za Quran tajwid

Soma Zaidi...
HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Ni zipi hukumu za nuni yenye sakina au tanwin?

Hapa utajifunza usomaji wa Quran pindi utakapokuta nuni yenyebsakina au tanwin

Soma Zaidi...
Faida za kujuwa Quran tajwid

Hapa nitakufindisha faida za kusoma quran kwa Tajwid.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA QALQALA

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
quran na sayansi

YALIYOMONENO LA AWALI1.

Soma Zaidi...
Fadhila za kusoma surat al Kahaf siku ya Ijumaa

Je unajuwa ni kwa nini unatakiwa usikose kusoma surat al Kahaf siku ya ijumaa. Makala hii itakujibu swali hili

Soma Zaidi...