Wanaadamu kushindwa Kuandika Kitabu Mithili ya Qur-an:

Wanaadamu kushindwa Kuandika Kitabu Mithili ya Qur-an:

(ix)Wanaadamu kushindwa Kuandika Kitabu Mithili ya Qur-an:



Ushahidi mkubwa na wa uwazi zaidi ni hii changa moto iliyonadiwa kwa wanaadamu wote katika Qur-an yenyewe. Ni kwamba, watu waliokufuru wa nyakati zote za historia ya Qur-an wanadai kuwa Qur-an si kitabu cha Allah(s.w) bali ni kitabu kinachotokana na kazi ya mwanaadamu, hususan Mtume Muhammad (s.a.w). Baadhi ya madai yao tumeshayaona katika kurasa za nyuma.


Baada ya kutoa madai yao haya yasiyo na ushahidi wowote au fununu yoyote ya ukweli, Allah (s.w), aliye Mjuzi na Mwingi wa hekima, Alitoa changamoto si kwa hawa wapinzani tu bali kwa wanaadamu wote ili baada ya hapo kila mwenye akili timamu ashuhudie kuwa Qur-an ni Kitabu cha Allah (s.w). Allah (s.w) alitoa wito kwa wapinzani wote wa Qur-an kuwa wakusanyike pamoja na washirikiane na wataalamu wote wa ulimwengu walio na uzoefu na uhodari katika sanaa ya uandishi kisha katika ushirikiano wao huo watoe kitabu mfano wa Qur-an. Historia nzima inatuonesha kuwa hakuna aliyefua dafu. Hebu turejee changa moto hii katika aya ifuatayo:


Sema: "Hata wakijikusanya watu (wote) na majini ili kuleta mfano wa hii Qur-an basi hawangaliweza kuleta mfano wake, hata kama watasaidiana (vipi) wao kwa wao." (17:88)



Baada ya kushindwa kutoa kitabu mfano wa Qur-an, Allah (s.w) aliwapa makafiri tahfifu ili wazidi kutanabahi na kuhuzunika kwa kuwanadia kuwa waandike mfano wa sura kumi tu za Qur-an badala ya sura 114, kama tunavyofahamishwa katika aya ifuatayo:



Ndiyo kweli wanasema kuwa: "Ameitunga mwenyewe (Muhammad hii Qur-an)?" Sema: "Basi leteni sura kumi za uwongo zilizotungwa mfano wa hii, na waiteni muwawezao (kuwaita) badala ya Allah (waje wakusaidieni kutunga hivyo) ikiwa mnasema kweli." (11:13)'



Hakuna aliyethubutu kutoa sura hizo kumi mfano wa Sura za Qur-an kwa wakati wote wa historia ya Qur-an. Allah (s.w) Mwingi wa Rehema na Mwingi wa Ujuzi na Hekima, alitoa tena tahfifu nyingine kwa kuwataka wale wote wanaodai kuwa Qur-an ni kitabu cha Mtume Muhammad (s.a.w) nao waandike angalau sura moja tu mfano wa sura za Qur-an kwa ufasaha wa lugha, mantiki, mtiririko wa maudhui na ukamilifu wa ujumbe. Hebu turejee aya zifuatazo:


"Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyomteremshia mtumwa wetu, (kuwa hakuteremshiwa na Allah), basi leteni sura moja iliyofanywa na (mtu) aliye mfano wake, na muwaite miungu yenu bighairi ya Allah (wakusaidieni) ikiwa mnasema kweli." (2:23)


Je, ndiyo wanasema ameitunga? Sema: "Hebu (tungeni na nyie) mlete sura moja mfano wake na waiteni muwezao (kuwapata waje) isipokuwa Allah (wa kuwasaidieni) kama nyinyi mnasema kweli (kuwa haya ameyazua Muhammad)" (10:38)


Kama Muhammad (s.a.w) ndiye mwandishi wa Qur-an angelithubutu kweli kutoa changa moto hii kwa walimwengu wote wa nyakati zote? Mtume (s.a.w) angaliwezaje kutamka kwa uhakika kiasi hicho kuwa walimwengu wote hata wakishirkiana pamoja hawawezi kuandika kitabu mithili ya Qur-an uhakika ambao umebakia mpaka hivi leo? Kwa hiyo kushindwa kwa wanaadamu wa enzi zote za historia ya Qur-an kuleta mfano wa Qur-an angalau sura moja ni hoja tosha kuwa Qur-an ni Kitabu cha Allah (s.w).



Aidha Qur-an pia imewajibu wale watu wanaosema kuwa Muhammad (s.a.w) ndiye aliyeandika Qur-an kwa kuwataka watu hao wazingatie mawili: Kwanza Muhammad aliishi nao kwa muda wa miaka 40 na hakuonesha dalili zozote za kuwa mwandishi wala mshairi. Imekuwaje ghafla mtu huyo akaweza kuandika aya ambazo hakuna awezaye kuleta mfano wake? Pili, Muhammad angewezaje kuandika Qur-an na ilhali hakujua kusoma wala kuandika? Hoja hizo zinapatikana katika aya zifuatazo za Qur-an:


"Sema: Kama Allah angelitaka nisingalikusomeeni hii (Qur-an), wala asingalikujulisheni (hiyo Qur-an). Nalikaa baina yenu umri (mwingi) kabla ya haya; (hamkunisikia kusema kitu). Basi hamfahamu (kuwa haya si yangu mwenyewe kwa nafsi yangu)? (10:16)


"Na hukuwa mwenye kusoma chochote kabla ya hiki, wala hukukiandika kwa mkono wako wa kuume, (ingekuwa hivyo) wangefanya shaka wale wanaotaka kubadilisha (haki). (29:48)




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 146


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Umuhimu wa ndoa na kuoa ama kuolwa katika jamii
Matamanio ya jimai ni katika maumbile na hayaepukiki. Soma Zaidi...

DUA ZA WAKATI WA HASIRA
DUA ZA WAKATI UNAPOKUWA NA HASIRA. Soma Zaidi...

Mbinu Alizozitumia Nabii Shu'ayb(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe Wake
Soma Zaidi...

NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA
NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA. Soma Zaidi...

Nadharia ya uchumi kiislamu
1. Soma Zaidi...

Swala ya jamaa na mnamna ya kuswali swala ya jamaa, nyumbni, msikitini na kwa wanawake
Soma Zaidi...

Shahada nguzo ya kwanza ya uislamu, sifa zake na umuhimu wake.
Soma Zaidi...

Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?
Mwezi ukionekana sehemu moja, Waislamu wote ulimwenguni watalazimika kufunga? Soma Zaidi...

Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani
2. Soma Zaidi...

TOFAUTI KATI YA MAKATOZO NA MAAMRISHO KATIKA SUNNAH
' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ': ' ' ' ' ' ' ' ' ': "'... Soma Zaidi...

Ukarimu na Sifa za kuwa Mkarimu na faida zake
30. Soma Zaidi...

Imam Bukhari na Sahihul Bukhari
Soma Zaidi...