Quran si Mashairi kama wanavyodai makafiri

Quran si Mashairi kama wanavyodai makafiri

(i)Dai kuwa Qur-an ni Mashairi aliyotunga Muhammad (s.

Quran si Mashairi kama wanavyodai makafiri

(i)Dai kuwa Qur-an ni Mashairi aliyotunga Muhammad (s.a.w):



Dai hili lilitolewa na Makuraishi katika enzi hizo za kushuka kwa Qur-an pia linaendelea kutolewa na makafiri wa karne hizi. Kwa mfano Stober, baada ya kusoma tafsiri ya Qur-an alidai kuwa itakuwa imeandikwa na Mwarabu ambaye ni mweledi wa historia ya Mayahudi na mila za nchi yake ambaye pia ni mshairi mzuri.
Udhaifu:



Wasomaji wa mashairi ya Kiarabu wanafahamu kuwa mashairi hayo yana mizani,beti na vina na yanaimbika kwa kiasi kwamba wakati mwingine inabidi hata maana au sarufi viwekwe pembeni alimradi tu shairi liimbike. Hivi sivyo kabisa ulivyo mfumo wa Qur-an. Qur-an si mashairi bali ni ujumbe wenye maana kamili ulioandikwa katika fasihi ya hali ya juu kwa kuzingatia sarufi na miiko yote ya lugha hai


.
Historia imeshuhudia kuwa Qur-an si mashairi. Ilikuwa kawaida ya washairi wakati ule wa Mtume (s.a.w) kubandika mashairi yao kwenye mlango wa Ka'aba kama changa-moto kwa washairi wengine. Ilitokea siku moja mshairi mashuhuri wa wakati huo, Labbiib ibn Rabiah, akabandika shairi lake kwenye mlango wa Ka'aba ili kutoa changamoto kwa washairi wengine. Shairi lake lilikuwa limetungwa kwa utaalamu mkubwa sana na lilikuwa zuri mno kiasi cha kutothubutu mtu yeyote kupambanisha shairi lake na hilo. Lakini baada ya kubandikwa kipande cha Sura ya Qur-an karibu na shairi lake, Labbiid mwenyewe (ambaye alikuwa Mshirikina) baada ya kusoma mistari michache ya sura hiyo alinaswa na mvuto wake na kuiamini dini iliyofunuliwa kutoka kwa Allah (s.w) na kubandua shairi lake




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1296

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Tofauti kati ya sura za makkah na madinah
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah

Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Quran si njozi za mvurugano alizoota Mtume Muhammad
Quran si njozi za mvurugano alizoota Mtume Muhammad

(ii)Dai kuwa Qur-an ni zao la njozi za Mtume (s.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa surat Al-Humazah
Sababu za kushuka kwa surat Al-Humazah

Zijuwe sababu kuu za kushuka surat Al-Humazah katika quran

Soma Zaidi...
Kukusanywa na kuhifadhiwa kwa quran
Kukusanywa na kuhifadhiwa kwa quran

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al bayyinah
Sababu za kushuka surat al bayyinah

Asbab nuzul surat al bayyinh. Sura hii imeteremka Madina na ina aya nane.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa surat An-Nasr (idhaa jaa)
Sababu za kushuka kwa surat An-Nasr (idhaa jaa)

SURATUN-NASR Sura hii imeteremka wakati Mtume (s.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Aina za usomaji wa Quran
Aina za usomaji wa Quran

Je kuna aina ngapi zabusomaji wa Quran

Soma Zaidi...