SURAT AL-QURAYSH Sura hii ina majina mawili.
SURAT AL-QURAYSH
Sura hii ina majina mawili. Inaitwa Qureish na pia inaitwa Li ii laafi. Ibni Abbas anasimulia ya kuwa ilishuka Makka. Qureish ni jina la kabila lililotoka kwa Nadhir bin Kinana (Razi). Wengine wanasema neno Qureish limetoka katika neno Qarsh ambalo ni jina la samaki mkubwa wa bahari anayekula samaki lakini yeye haliwi. Hivyo kwa ukubwa wa kabila lao na kwa kuheshimiwa na watu wote nao wakaitwa Kureish. Makureish walikuwa watu wa Makka na walinzi wa Kaaba, na kwa sababu ya kuilinda Kaaba waliheshimiwa sana.
Sura hii imeshuka kwa maqurayshi kama alivyosema Mtume (s.a.w) βAllah amewapa neema Maquraysh ambayo hajampa yeyote kabla yao na hatampa yeyote baada yao: Ukhalifa umepewa mtu katika wao, uangalizi wa nyumba tukufu ya Allah umepewa mtu miongoni mwao, kazi ya kuwapa maji mahujaji imepewa mtu katika wao, utume umepewa mtu katika wao, wamepewa ushindi dhidi ya jeshi la tembo, walimuabudu Allah kwa miaka saba ambapo hakuna yeyote aliyekuwa akimuabudu Allah, na sura kwenye quran imeshushwa kwa ajili yao na hakuna yeyote aliyetajwa kwenye surahiyo ila wao (kwa kupewa jina la al-quraysh)
Umeionaje Makala hii.. ?
Asbab nuzul surat al bayyinh. Sura hii imeteremka Madina na ina aya nane.
Soma Zaidi...SURAT AL-MUAWIDHATAYN (SURAT AL-FALAQ NA SURATUN-NAS) Inaelezwa kuwa sura mbili hizi zilishuka pamoja, na maulamaa wanaelezea kuwa Mtume (s.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza kanuni za tajwid katika kusoma bismillah au basmalah.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukuorodheshea aina saba za viraka vya usomaji wa Quran.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza usomaji wa Quran pindi utakapokuta nuni yenyebsakina au tanwin
Soma Zaidi...Post hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa surat at Tin (watin wazaitun).
Soma Zaidi...Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet
Soma Zaidi...Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa
Soma Zaidi...