Maadili katika surat luqman
Maadili katika surat luqman
Na kwa yakini Tulimpa Luqmani hikima, tukamwambia Mshukuru Mwenyezi Mungu; na atakayeshukuru, kwa yakini anashukuru kwa ajili ya nafsi yake; na atakaye kufuru,
Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Asifiwaye, (hahitaji kushukuriwa na yeye). (31:12)
Na (wakumbushe), Luqmani alipomwambia Mwanawe; na hali ya kuwa anampa nasaha.Ewe mwanangu! Usimshirikishe Mwenyezi Mungu, maana kushirikisha ndiyo dhulma kubwa. (31:13)
Na tumemuusia mwanaadamu (kuwafanyia ihsani) wazazi wake - mama yake ameichukuwa mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu, na (kumnyonyesha na kuja) kumwachisha kunyonya katika miaka miwili - ya kwamba unishukuru Mimi na wazazi wako; marejeo yenu ni Kwangu. (3 1:14)
Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwendo wao mbaya); shika njia ya wale wanaoelekea Kwangu, kisha marejeo yenu ni Kwangu, hapo Nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda. (31:15)
Ewe mwanangu! Kwa hakika jambo lolote lijapokuwa na uzito wa chembe ya hardali, likawa ndani ya jabali au mbinguni au katika ardhi, Mwenyezi Mungu Atalileta (amlipe aliyefanya); bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo yaliyofichikana, (na) Mjuzi wa mambo yaliyo dhahiri. (31:16)
Ewe mwanangu! Simamisha Sala, na uamrishe mema, na ukataze mabaya, usubiri juu ya yale yatakayokusibu (kwani mwenye kuamrisha mema na kukataza mabaya lazima zitamfika tu taabu); Hakika hayo ni katika mambo yanayostahiki kuazimiwa (na kila mtu). (31:17)
Wala usiwatazame (usiwafanyie watu jeuri), kwa upande mmoja wa uso, wala usende katika nchi kwa maringo; hakika Mwenyezi Mungu Hampendi kila ajivunae, ajifahirishaye. (31:18)
Na ushike mwendo wa katikati, na uteremshe sauti yako; bila shaka sauti ya punda ni mbaya kuliko sauti zote (kwa makelele yake ya bure). (31:19)
Mzazi wa Kiislamu mwenye hekima ni yule atakayekuwa mstari wa mbele kutenda mema na kuwalea watoto wake wafuate nyayo zake pamoja na kuwausia na kujiusia yeye mwenyewe kufanya yafuatayo:
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 kitabu cha Simulizi π2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π3 Kitabu cha Afya π4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π5 Simulizi za Hadithi Audio π6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Kwa nini uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza
Elimu imepewa nafasi kubwa sana katika uislamu.
Soma Zaidi...Mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu
Ni mgawanyo upi wa elimu haukubaliki. Ni ipi elimul akhera na elimu dunia? (Edk form 1 Dhana ya elimu)
Soma Zaidi...Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab
Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu.
Soma Zaidi...Makundi ya dini za wanaadamu
Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu.
Soma Zaidi...