Kubisha hodi katika nyakati za faragha katika familia

β€œEnyi mlioamini!

Kubisha hodi katika nyakati za faragha katika familia

(i) Kubisha hodi katika nyakati za faragha katika familia



β€œEnyi mlioamini! Nawakupigieni hodi wale iliyowamiliki mikono yenu ya kuume, (ya kulia), na wale wasiofikia baleghe miongoni mwenu, mara tatu: kabla ya Sala ya Alfajiri na mnapovua nguo zenu Adhuhuri, na baada ya Sala ya Isha; hizi ni nyakati tatu za faragha kwenu. Si vibaya juu yenu wala juu yao baada ya nyakati hizo (kuingia bila ya kupiga hodi:) mnazungukiana nyinyi kwa nyinyi. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu Anavyokuelezeni Aya (zake); na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye hikima.



β€œNa watoto miongoni mwenu, watakapobaleghe basi nawapige hodi kama walivyopiga hodi wale wa kabla yao. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyokubainishieni aya zake, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye hikima. (24:58-59)



Katika aya hizi tunapewa maelekezo ya kinidhamu na kimaadili juu ya watoto na watumishi kuwatembelea wazazi wakiwa nyumbani mwao kama ifuatavyo:
(i)Waumini wanatakiwa wawaelekeze watoto wao ambao hawajafikia baleghe kuwa wabishe hodi wanapotaka kuingia vyumbani katika nyakati tatu za faragha zilizoainishwa:
1.Kabla ya Swala ya Al-fajiri
2.Kabla ya Swala ya Adhuhuri wakati wa kujitayarisha kwa swala.
3.Baada ya Swala ya Al-Ishaa.
(ii)Mida mingine nje ya hii watoto wanaruhusika kuingia bila ya hodi. Kwa maana nyingine wazazi wawe katika hali ya sitara ambayo haitakuwa ni chukizo watakapokutwa na watoto.
(iii)Watoto waliofikia baleghe hawaruhusiwi kuingia chumbani mwa wazazi wao pasina kubisha hodi katika nyakati zote.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1221

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰2 web hosting    πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Umbile la mbingu na ardhi linavyothibitisha uwepo wa Allah

Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio.

Soma Zaidi...
Dhana ya ibada kwa mtazamo wa uislamu..

Mtazamo wa uislamu juu ya ibada (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.

Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu.

Soma Zaidi...
Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.

Soma Zaidi...
Kwa nini uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza

Elimu imepewa nafasi kubwa sana katika uislamu.

Soma Zaidi...
Kumuamini mwenyezi Mungu..

Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu

Mahusiano kati ya elimu ya mwongizo na elimu ya mazingira katika uislamu.

Soma Zaidi...