Kubisha hodi katika nyakati za faragha katika familia

β€œEnyi mlioamini!

Kubisha hodi katika nyakati za faragha katika familia

(i) Kubisha hodi katika nyakati za faragha katika familia



β€œEnyi mlioamini! Nawakupigieni hodi wale iliyowamiliki mikono yenu ya kuume, (ya kulia), na wale wasiofikia baleghe miongoni mwenu, mara tatu: kabla ya Sala ya Alfajiri na mnapovua nguo zenu Adhuhuri, na baada ya Sala ya Isha; hizi ni nyakati tatu za faragha kwenu. Si vibaya juu yenu wala juu yao baada ya nyakati hizo (kuingia bila ya kupiga hodi:) mnazungukiana nyinyi kwa nyinyi. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu Anavyokuelezeni Aya (zake); na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye hikima.



β€œNa watoto miongoni mwenu, watakapobaleghe basi nawapige hodi kama walivyopiga hodi wale wa kabla yao. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyokubainishieni aya zake, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye hikima. (24:58-59)



Katika aya hizi tunapewa maelekezo ya kinidhamu na kimaadili juu ya watoto na watumishi kuwatembelea wazazi wakiwa nyumbani mwao kama ifuatavyo:
(i)Waumini wanatakiwa wawaelekeze watoto wao ambao hawajafikia baleghe kuwa wabishe hodi wanapotaka kuingia vyumbani katika nyakati tatu za faragha zilizoainishwa:
1.Kabla ya Swala ya Al-fajiri
2.Kabla ya Swala ya Adhuhuri wakati wa kujitayarisha kwa swala.
3.Baada ya Swala ya Al-Ishaa.
(ii)Mida mingine nje ya hii watoto wanaruhusika kuingia bila ya hodi. Kwa maana nyingine wazazi wawe katika hali ya sitara ambayo haitakuwa ni chukizo watakapokutwa na watoto.
(iii)Watoto waliofikia baleghe hawaruhusiwi kuingia chumbani mwa wazazi wao pasina kubisha hodi katika nyakati zote.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1066

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Kumuamini mwenyezi Mungu..

Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W)

Zifuatazo ni njia nyingi za kumjua Mwenyezi Mungu (EDK form 2:dhana ya elimu katika uislamu)

Soma Zaidi...
Mitume wa uongo

Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s.

Soma Zaidi...
Mgawanyiko wa Elimu kwa mtazamo wa kikafiri

Kwa mtazamo wa kikafiri elimu imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Elimu ya dunia na Elimu ya akhera.

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu

Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu Ni upi? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu)

Soma Zaidi...
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao

Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.

Soma Zaidi...