image

Mtume Muhammad hakujuwa kusoma wala kuandika ni hoja na kuna hekima zake

(i)Mtume Muhammad (s.

Mtume Muhammad hakujuwa kusoma wala kuandika ni hoja na kuna hekima zake

(i)Mtume Muhammad (s.a.w) Kutojua Kusoma na Kuandika:
Iwazi mno katika historia yake kuwa Mtume (s.a.w) hakujua kusoma wala kuandika. Ukweli huu wa historia unathibitishwa na aya za Qur-an zifuatazo:


"Sema (Wewe Nabii Muhammad): Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Allah kwenu nyinyi nyote, (Allah) ambaye ana ufalme wa mbingu na ardhi, hapana aabudiwaye (kwa haki) ila Yeye, Ndiye ahuishaye na ndiye afishaye.Basi mwaminini Allah na Mtume wake, aliye Nabii Ummy, (asiyejua kusoma wala kuandika), ambaye humwamini Allah na maneno yake na mfuateni yeye ili mpate kuongoka." (7:158)


"Na hukuwa mwenye kusoma kitabu chochote kabla ya hiki, wala hukukiandika kwa mkono wako wa kuume, ingekuwa hivyo wangefanya shaka wale wanaotaka kubadilisha (haki)." (29:48)



Sababu ya Mtume (s.a.w) kutojua kusoma wala kuandika imebainishwa wazi katika aya hii ya (29:48) kuwa angelijua kusoma na kuandika watu wakaidi wasio tayari kumwamini Mtume na kuamini Qu-ran kwa sababu si maneno ya Allah(s.w) bali ni maneno aliyoyatunga Mtume (s.a.w) au ni maneno aliyoyanakili kutoka kwenye vitabu vya kale au ni maneno aliyofundishwa na watunga mashairi mashuhuri na kuyanukuu kwenye kitabu. Mtume (s.a.w) angalijua kusoma na kuandika ingalikuwa vigumu sana kuonesha udhaifu wa madai haya.


Lakini kutojua kusoma wala kuandika kwa Mtume (s.a.w) kumewafanya wapinzani wengi wakose hoja ya uwazi ya kukataa kuwa Qur-an si Kitabu cha Allah (s.w).Hata hivyo, pamoja na ukweli wa historia kuwa Mtume (s.a.w) hakuwa ni mwenye kujua kusoma wala kuandika, walitokea watu waliojitia upofu na kudai kuwa Qur-an ni maneno ya Muhammad (s.a.w). Ili kuwahuzunisha na kuwaonesha kuwa ni waongo katika madai yao hayo, Allah (s.w) aliwawekea watu hao na walimwengu kwa ujumla changa moto ambayo tutaiona katika kipengele cha (ix).



Kwa hiyo Mtume Muhammad (s.a.w) kutojua kwake kusoma wala kuandika na bado akawasilisha kwa watu ujumbe mzito wenye hekima kubwa na wenye kumuongoza mwanaadamu kwa usahihi katika kila kipengele cha maisha yake, ujumbe ambao hapana yeyote anayeweza kuleta mfano wake ni ushahidi mkubwa kuwa Qur-an yote kama ilivyo ni maneno ya Allah (s.w).




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 633


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Sababu za kushuka Surat al fatiha (Alhamdu)
Kwa kuwa hakuna sababu mwalumu ikiyonukuliwa kuwa ndio chanzo cha kushushwa suravhii. Basi post hii itakujuza mambo ambayo huwenda hukuyajuwa kuhusu fadhika za surabhii na mengineyo. Soma Zaidi...

sura ya 11
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Fadhila za kusoma surat al Kahaf siku ya Ijumaa
Je unajuwa ni kwa nini unatakiwa usikose kusoma surat al Kahaf siku ya ijumaa. Makala hii itakujibu swali hili Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al-Fiyl
Al fiyl ni neno la Kiarabu lenye maana ya tembo. Sura hii inazungumziakisa cha jeshi lenye tembo. Jeshi hili lilikuwa na nia ya kuvunja al qaaba Soma Zaidi...

Aasbab Nuzul surat Ash sharh: sababu za kushuka alam nashrah (surat Ash sharh)
Makala hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa alam nasharah yaani Surat Ash sharh. Soma Zaidi...

Sababu za Kushuka Surat Al-Masad (tabat yadaa) na fadhila zake
4. Soma Zaidi...

Kwa nini quran ilishuka kidogo kidogo?
Kuna sababu nyingi za kuonyesha umuhimu wa Quran kushuka kwa mfumo wa kidogo kidogo Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al qadir
Asbab nuzul surat al qadi. Hii ni sura ya 97 katika mpangilio wa mashaf. Surat al qadir imeteremshwa Madina na ina aya 5. Soma Zaidi...

Fadhila za kusoma surat al Imran
Post hii itakufundisha fadhila na faida za kusoma surat al Imran Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat Al-Humazah
Zijuwe sababu kuu za kushuka surat Al-Humazah katika quran Soma Zaidi...

Kutokea Kweli Matukio yaliyotabiriwa katika Qur-an
Soma Zaidi...

Maswali yanayohusu quran
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...