Mtume Muhammad hakujuwa kusoma wala kuandika ni hoja na kuna hekima zake

(i)Mtume Muhammad (s.

Mtume Muhammad hakujuwa kusoma wala kuandika ni hoja na kuna hekima zake

(i)Mtume Muhammad (s.a.w) Kutojua Kusoma na Kuandika:
Iwazi mno katika historia yake kuwa Mtume (s.a.w) hakujua kusoma wala kuandika. Ukweli huu wa historia unathibitishwa na aya za Qur-an zifuatazo:


"Sema (Wewe Nabii Muhammad): Enyi watu! Hakika mimi ni Mtume wa Allah kwenu nyinyi nyote, (Allah) ambaye ana ufalme wa mbingu na ardhi, hapana aabudiwaye (kwa haki) ila Yeye, Ndiye ahuishaye na ndiye afishaye.Basi mwaminini Allah na Mtume wake, aliye Nabii Ummy, (asiyejua kusoma wala kuandika), ambaye humwamini Allah na maneno yake na mfuateni yeye ili mpate kuongoka." (7:158)


"Na hukuwa mwenye kusoma kitabu chochote kabla ya hiki, wala hukukiandika kwa mkono wako wa kuume, ingekuwa hivyo wangefanya shaka wale wanaotaka kubadilisha (haki)." (29:48)



Sababu ya Mtume (s.a.w) kutojua kusoma wala kuandika imebainishwa wazi katika aya hii ya (29:48) kuwa angelijua kusoma na kuandika watu wakaidi wasio tayari kumwamini Mtume na kuamini Qu-ran kwa sababu si maneno ya Allah(s.w) bali ni maneno aliyoyatunga Mtume (s.a.w) au ni maneno aliyoyanakili kutoka kwenye vitabu vya kale au ni maneno aliyofundishwa na watunga mashairi mashuhuri na kuyanukuu kwenye kitabu. Mtume (s.a.w) angalijua kusoma na kuandika ingalikuwa vigumu sana kuonesha udhaifu wa madai haya.


Lakini kutojua kusoma wala kuandika kwa Mtume (s.a.w) kumewafanya wapinzani wengi wakose hoja ya uwazi ya kukataa kuwa Qur-an si Kitabu cha Allah (s.w).Hata hivyo, pamoja na ukweli wa historia kuwa Mtume (s.a.w) hakuwa ni mwenye kujua kusoma wala kuandika, walitokea watu waliojitia upofu na kudai kuwa Qur-an ni maneno ya Muhammad (s.a.w). Ili kuwahuzunisha na kuwaonesha kuwa ni waongo katika madai yao hayo, Allah (s.w) aliwawekea watu hao na walimwengu kwa ujumla changa moto ambayo tutaiona katika kipengele cha (ix).



Kwa hiyo Mtume Muhammad (s.a.w) kutojua kwake kusoma wala kuandika na bado akawasilisha kwa watu ujumbe mzito wenye hekima kubwa na wenye kumuongoza mwanaadamu kwa usahihi katika kila kipengele cha maisha yake, ujumbe ambao hapana yeyote anayeweza kuleta mfano wake ni ushahidi mkubwa kuwa Qur-an yote kama ilivyo ni maneno ya Allah (s.w).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2537

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Ni nini maana ya id-gham katika hukumu za tajwid

Hapa utajifunza kuhusu maana ya id-ghamu na aina zake.

Soma Zaidi...
Quran Tafsiri kwa Kiswahili

Tafsiri ya quran kw akiswahili, imeandikw ana Shekh Ali Muhsin al-Barwani

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al humazah

Sura hii inaonya vikali tabia ya kusengenya na kusambaza habari za uongo. Wameonywa vikali wenye tabia ya kujisifu kwa mali, kukusanya mali bila ya kuitolea zaka.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA (MIIM SAKINA)

HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA : Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( Ω…Ω’).

Soma Zaidi...
Maana ya Idgham na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Aina za idgham ni idgham al mutamathilain, na idgham al mutajanisain

Soma Zaidi...
Aina za Madda twabiy kwenye usomaji wa Quran

Madda zimegawanyika katika maeneo makuu mawili ambayo ni madda twabiy na madda fariy

Soma Zaidi...
Fadhila za kusoma surat al Kahaf siku ya Ijumaa

Je unajuwa ni kwa nini unatakiwa usikose kusoma surat al Kahaf siku ya ijumaa. Makala hii itakujibu swali hili

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat at Takaathur

Kuwa na tamaa huhitaji vitu vya watu si jambo jema. Ila kama tamaa hii itakuhamasisha na wewe kutafuta kitu hicho, kwa uwezo ambao Allah amekupa bila ha kuvuka mipaka yake, hili sio tatizo. Sura hii itakufundisha mengi

Soma Zaidi...