Wanazuoni wengi zaidi wanakubaliana ya kuwa sura hii surat At-Takaathur ilishuka Makka, na hizi ndio sababu za kushuka kwa sura hii
SURAT AT-TAKAATHUR
Wanazuoni wengi zaidi wanakubaliana ya kuwa sura hii ilishuka Makka. Imam Bukhari anaeleza ya kuwa ilishuka Madina. Lakini sahaba mmoja, Ibni Abbas, anasema ya kuwa ilishuka Makka. Neno Takaathur anasema Ibn Abbas maana yake ni tamaa nyingi ya mali na watoto (Bukhari). Abu Huraira anasimulia ya kuwa Mtume s.a.w. aliposoma sura hii alisema, "Mwanadamu anasema, hii ni mali yangu, hii ni mali yangu. Kumbe aliyokula na kuvaa ameichakaza, aliyotoa katika njia ya Mwenyezi Mungu, ndiyo kaiweka akiba na iliyobaki si yake ni mali ya watu."
Sababu za kushuka sura hii:-
Muqatil na Al-Kalb wamesema “sura hii ilishuka kutokana na makabila mawili ya Kikurayshi, ambayo ni Banu Abd Manafi na Banu Sahm. Kila kabila lilikuwa likijisifu na kujigamba juu ya lingine. Hivyo ikafikia hadi wakaanza kuheabu ni kabila lipi lina machifu wengi na viongozi wengi kuliko lingine. Banu Abd Manafi walikuwa wakisema “sisi tuna machifu wengi, viongozi wengi na hata kabila letu lina watu wengi”. pia banu Sahm walikuwa wakisema hivyohivyo. Basi baada ya kuhesabu ikaonekana kweli Banu Abd Manafi wana watu wengi kwenye kabila lao. Baada ha yapo wakasema “twendeni tukahesabu makaburi ya watu wetu waliokufa. Hivyo wakayaendea makaburi hapo wakaata jibu kuwa Banu Saham ni wengi waliokufa kuliko Banu Abd Manafi.
Qatada amesema kuwa sura hii ilishuka kuwahusu Mayahudi waliosema “sisi ni wengi ssana kuliko wakina fulani na fulani ….., hivyo walikuwa wakiendelea na madai yao haya na kujisahau, kumuasi mungu hadi mauti anawafikia.
‹ Nyuma
› Endelea
‹ Books
‹ Apps ››
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowSURATUN-NASR Sura hii imeteremka wakati Mtume (s.
Soma Zaidi...Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.
Soma Zaidi...TAHADHARI KWA WASOMAJI WA QURAN Wasomaji wa qurani wawe na tahadhari katika usomaji wao.
Soma Zaidi...2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA
Soma Zaidi...SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( مْ).
Soma Zaidi...