Python somo la 56: Kuongeza Data Katika Database kwa Kutumia Django Admin na Django Shell
Katika somo hili tutajifunza njia mbili muhimu za kuongeza data kwenye database katika project yetu ya pybongo (app: menu). Njia hizi ni: Kutumia Django Admin Kutumia Django Shell Utafahamu pia jinsi ya kusajili models kwenye admin, jinsi ya kuingia admin panel, na namna ya kutengeneza entries mpya za MenuItem.
Utangulizi
Baada ya kutengeneza models na kufanya migrations, hatua inayofuata ni kujaza database kwa data. Django hutupatia njia rahisi na salama za kufanya hivyo. Somo hili litakuongoza hatua kwa hatua jinsi ya kuongeza taarifa za vyakula, bei, muda wa upatikanaji na maelezo kwenye database.
Sasa tuingie kwenye somo letu…
1. Kutumia Django Admin
1.1 Kuanza Admin
Django Admin ni paneli ya kusimamia database bila kuandika SQL yoyote. Lakini ili uitumie:
Hatua ya Kwanza: Tengeneza Superuser
Kwenye terminal:
python manage.py createsuperuser
Utaulizwa:
-
Username
-
Email
-
Password
Hizi ndiyo utatumia kuingia admin panel.
1.2 Kusajili Model Katika Admin
Ili model ionekane kwenye Django Admin, lazima usajili ndani ya admin.py.
Faili: menu/admin.py
from django.contrib import admin
from .models import MenuItem
admin.site.register(MenuItem)
Sasa Django Admin itahusisha model yetu ya MenuItem.
1.3 Kuingia kwenye Admin Panel
Endesha server:
python manage.py runserver
Kisha kwenye browser fungua:
http://localhost:8000/admin/
Ingia kwa username na password ulizounda.
Sasa utaona sehemu ya MenuItem ikiwa ndani ya app menu.
1.4 Kuongeza Data Kupitia Admin
-
Bofya Menu Items
-
Chagua Add Menu Item
-
Jaza:
-
jina
-
maelezo
-
muda_upatikanaji
-
bei
-
-
Bofya Save
Data imehifadhiwa moja kwa moja kwenye database.
2. Kutumia Django Shell
Django Shell hukuruhusu kuingiza data moja kwa moja kwa kutumia Python. Tutakuja...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 ai web app π2 Kitau cha Fiqh π3 Madrasa kiganjani π4 Kitabu cha Afya π5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Python somo la 16: Jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop
Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop
Soma Zaidi...Python somo la 34: Kutumia html kwneye python
Katika somo hili utakwend akujifunz ajinsi ya kutumia html kwneye python
Soma Zaidi...Python somo la 49: Jinsi ya ku host project ya Django
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website ya Django. Hapa tutakwenda kutuma plaform ya pythonanywhere.com.
Soma Zaidi...Python somo la 24: Nini maana ya Object Oriented Programming
Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code
Soma Zaidi...Python somo la 32: Jinsi ya kusoma mafaili
Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data
Soma Zaidi...Python somo la 60: Hashing na Encryption kwenye Django
Katika somo hili tutajifunza: Tofauti kati ya hashing na encryption Jinsi ya kufunga packages muhimu Jinsi ya kufanya hashing kwa maneno ya kawaida (mfano βbongoclassβ) Jinsi ya kufanya encryption na decrypt kutumia Fernet Jinsi Django inahash password kupitia User model Mazoezi ya vitendo
Soma Zaidi...