PHP somo la 53: class inheritance kwenye PHP Object Oriented Programming
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu class inheritance kwenye object oriented programming.
Inheritance ni nini?
Hiki ni kitendo kuwa class moja inarithi property na method kutoka class nyingine. Hii inayorithi itaitwa child class yaani class toto. Katika kurithi huku tutazingatia access modifier, hivyo basi tutarithi method na property ambazo ni public au protected. Class ambayo inayorithi (inherited) huongezewa keyword extends wakati wa kuitengeneza.
Mfano:
<?php
class Gari {
}
class prado extends Gari {
}
?>
Hapo class Gari huitwa parent class na hiyo class prado huitwa child class. Sasa ngoja tuone namna ambavyo tunaweza kurithi method na property ambazo ni public ama protected.
<?php
class Gari
{
public $jina;
protected $speed;
public function __construct($jina, $speed)
{
$this->jina = $jina;
$this->speed = $speed;
}
protected function tangazo()
{
echo "Tunauza {$this->jina} yenye speed ya {$this->speed}.";
}
}
class Prado extends Gari
{
public function tangazo_jipya()
{
//method tangazo ni protected
$this->tangazo();
}
}
$Toyota = new Prado("Toyota", "180 km/h");
$Toyota->tangazo_jipya();
?>
Hapo utaona method tangazo() ni protected lakini tumeweza kuitumia kwenye child class prado(). Hii ni kwa sababu class Prado() imerithi property na method kutoka kwenye parent class Gari().
Kwa kutumia mfabo huo hata property ikiwa ni protected unaweza kuitumia ndani ya child class bila ya wasi wasi wowote.
Hapo kuna kitu kipya umekiona {$this->jina} umeona hapo tumetumia mabano {} haya hapo yametumika ili tuweze kutumia hizo property kwenye string. Hii kitaalamu inaitwa string interpolation. Angalia mfano mmoja hapo chini
<?php
$x = 4;
$b = 6;
$z = $x +$b;
echo "jumala ya {$x} na {$b} ni {$z}";
jumala ya 4 na 6 ni 10
Overriding inherited method
Sasa kuna hii concept hapa tunapasa kuijuwa. Ni kuwa endapo method utaitenegeza upya kwenye child class basi method ya mwanzo itakuwa imebadilishwa. Hapo ndio tunaita overriding method.
Angalia mfa...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 ai web app 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
PHP somo la 81: Cross - Orgn Resource Sharing - CORSE header
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Cross - Orgn Resource Sharing ama inafupishwa kama CORSE header
Soma Zaidi...PHP somo la 64: Jinsi ya kutengeneza database na kuingiza data kwa kuumia PDO
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia PDO kutengeneza database, kuteneneza table na kuingiza data moja na zaidi ya moja.
Soma Zaidi...PHP - somo la 7: Jinsi ya kaundika function yakwako
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe yaani user defined function
Soma Zaidi...PHP - somo la 17: Jinsi ya kuingiza data kwenye database kwa kutumia PHP
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuingiza data kwenye dtabase kwa kutumia PHP.
Soma Zaidi...PHP -somo la 33: Matumizi ya while loop kwenye PHP
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP
Soma Zaidi...PHP -somo la 31: Matumizi ya include() na require() function kwenye php
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function za PHP kama require() na iclude()
Soma Zaidi...