Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu class inheritance kwenye object oriented programming.
Inheritance ni nini?
Hiki ni kitendo kuwa class moja inarithi property na method kutoka class nyingine. Hii inayorithi itaitwa child class yaani class toto. Katika kurithi huku tutazingatia access modifier, hivyo basi tutarithi method na property ambazo ni public au protected. Class ambayo inayorithi (inherited) huongezewa keyword extends wakati wa kuitengeneza.
Mfano:
<?php
class Gari {
}
class prado extends Gari {
}
?>
Hapo class Gari huitwa parent class na hiyo class prado huitwa child class. Sasa ngoja tuone namna ambavyo tunaweza kurithi method na property ambazo ni public ama protected.
<?php
class Gari
{
public $jina;
protected $speed;
public function __construct($jina, $speed)
{
$this->jina = $jina;
$this->speed = $speed;
}
protected function tangazo()
{
echo "Tunauza {$this->jina} yenye speed ya {$this->speed}.";
}
}
class Prado extends Gari
{
public function tangazo_jipya()
{
//method tangazo ni protected
$this->tangazo();
}
}
$Toyota = new Prado("Toyota", "180 km/h");
$Toyota->tangazo_jipya();
?>
Hapo utaona method tangazo() ni protected lakini tumeweza kuitumia kwenye child class prado(). Hii ni kwa sababu class Prado() imerithi property na method kutoka kwenye parent class Gari().
Kwa kutumia mfabo huo hata property ikiwa ni protected unaweza kuitumia ndani ya child class bila ya wasi wasi wowote.
Hapo kuna kitu kipya umekiona {$this->jina} umeona hapo tumetumia mabano {} haya hapo yametumika ili tuweze kutumia hizo property kwenye string. Hii kitaalamu inaitwa string interpolation. Angalia mfano mmoja hapo chini
<?php
$x = 4;
$b = 6;
$z = $x +$b;
echo "jumala ya {$x} na {$b} ni {$z}";
jumala ya ">...
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Authentication header, najinsi ya kutuma taarifa hizo na kuzisoma
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia PHP kutengeneza database kwenye mysql database.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya iteration kwenye PHP OOP hapa tutakwenda kuiona jinsi inavyofanya kazi pamoja na foreach loop
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza ukurasa wa kupost kwa kutumia html form
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku update na kufuta data kwenye database kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuingiza data kwenye dtabase kwa kutumia PHP.
Soma Zaidi...Katika soo hili utakwenda kujifunza umuhmu wa kutumia PDO kwenye PHP kwa ajili ya kutumia database.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ambavyo utaweza kutengeneza mfumo wa kuisajiki na ku login, kisha kuangalia usalama wa mfumo kwa kuzuia sql injection.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwendakujifunza concept ya namespaces na jinsi inavyosaidi kwenye OOP
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunzo kuhusu teknolojia ya ORM na inavyotumika kulinda usalama wa database
Soma Zaidi...