Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu class inheritance kwenye object oriented programming.
Inheritance ni nini?
Hiki ni kitendo kuwa class moja inarithi property na method kutoka class nyingine. Hii inayorithi itaitwa child class yaani class toto. Katika kurithi huku tutazingatia access modifier, hivyo basi tutarithi method na property ambazo ni public au protected. Class ambayo inayorithi (inherited) huongezewa keyword extends wakati wa kuitengeneza.
Mfano:
<?php
class Gari {
}
class prado extends Gari {
}
?>
Hapo class Gari huitwa parent class na hiyo class prado huitwa child class. Sasa ngoja tuone namna ambavyo tunaweza kurithi method na property ambazo ni public ama protected.
<?php
class Gari
{
public $jina;
protected $speed;
public function __construct($jina, $speed)
{
$this->jina = $jina;
$this->speed = $speed;
}
protected function tangazo()
{
echo "Tunauza {$this->jina} yenye speed ya {$this->speed}.";
}
}
class Prado extends Gari
{
public function tangazo_jipya()
{
//method tangazo ni protected
$this->tangazo();
}
}
$Toyota = new Prado("Toyota", "180 km/h");
$Toyota->tangazo_jipya();
?>
Hapo utaona method tangazo() ni protected lakini tumeweza kuitumia kwenye child class prado(). Hii ni kwa sababu class Prado() imerithi property na method kutoka kwenye parent class Gari().
Kwa kutumia mfabo huo hata property ikiwa ni protected unaweza kuitumia ndani ya child class bila ya wasi wasi wowote.
Hapo kuna kitu kipya umekiona {$this->jina} umeona hapo tumetumia mabano {} haya hapo yametumika ili tuweze kutumia hizo property kwenye string. Hii kitaalamu inaitwa string interpolation. Angalia mfano mmoja hapo chini
<?php
$x = 4;
$b = 6;
$z = $x +$b;
echo "jumala ya {$x} na {$b} ni {$z}";
jumala ya ">...
Umeionaje Makala hii.. ?
katika somo hili utajifunza jinsi ya ku upload multiple file yaani mafaili mengi kwa wakati mmoja kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi
Soma Zaidi...Katika somo hili utaweza kujifunza ni kwa nambna gani utaweza kutengeneza blog post na kuisoma kwa kutumia data za json
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu access modifier ili kuweza kuthibiti nama ya kuzitumia properties kwenye class.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutuma email kwa kutumia email() function ya PHP. Hii ni njia rahisi zaidi ya kutuma email. Ila hufanya kazi kwenye hosting.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kuhifunza kuhusu Custom header na aina zake
Soma Zaidi...Katika somo hili utajwenda kujifunza jinsi ya kuzuia hacking kwenye website yako
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia constatnt kwenye class.
Soma Zaidi...Katika somo hilibutajifunza maana ya cURL pamoja na matumini yake
Soma Zaidi...