Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu class inheritance kwenye object oriented programming.
Inheritance ni nini?
Hiki ni kitendo kuwa class moja inarithi property na method kutoka class nyingine. Hii inayorithi itaitwa child class yaani class toto. Katika kurithi huku tutazingatia access modifier, hivyo basi tutarithi method na property ambazo ni public au protected. Class ambayo inayorithi (inherited) huongezewa keyword extends wakati wa kuitengeneza.
Mfano:
<?php
class Gari {
}
class prado extends Gari {
}
?>
Hapo class Gari huitwa parent class na hiyo class prado huitwa child class. Sasa ngoja tuone namna ambavyo tunaweza kurithi method na property ambazo ni public ama protected.
<?php
class Gari
{
public $jina;
protected $speed;
public function __construct($jina, $speed)
{
$this->jina = $jina;
$this->speed = $speed;
}
protected function tangazo()
{
echo "Tunauza {$this->jina} yenye speed ya {$this->speed}.";
}
}
class Prado extends Gari
{
public function tangazo_jipya()
{
//method tangazo ni protected
$this->tangazo();
}
}
$Toyota = new Prado("Toyota", "180 km/h");
$Toyota->tangazo_jipya();
?>
Hapo utaona method tangazo() ni protected lakini tumeweza kuitumia kwenye child class prado(). Hii ni kwa sababu class Prado() imerithi property na method kutoka kwenye parent class Gari().
Kwa kutumia mfabo huo hata property ikiwa ni protected unaweza kuitumia ndani ya child class bila ya wasi wasi wowote.
Hapo kuna kitu kipya umekiona {$this->jina} umeona hapo tumetumia mabano {} haya hapo yametumika ili tuweze kutumia hizo property kwenye string. Hii kitaalamu inaitwa string interpolation. Angalia mfano mmoja hapo chini
<?php
$x = 4;
$b = 6;
$z = $x +$b;
echo "jumala ya {$x} na {$b} ni {$z}";
jumala ya ">...
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku generate PDF automatik kutoka kwenye php code , html, javascript na css.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu cronjob na matumizi yake kwenye PHP
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya traits kwenye OOP. hii itakusaidia ku solve baadhi ya changamoto zinazotokana na inheritance
Soma Zaidi...Somo hili litakwenda kukutajia baadhi ya library za php ambazo hutumika kwa matumizi ya ORM
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya sqlite kwa kutumia PHP.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya iteration kwenye PHP OOP hapa tutakwenda kuiona jinsi inavyofanya kazi pamoja na foreach loop
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kukusanya taarifa za watumiaji kwa kutumia html form.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia taarifa ambazo zimekusanywa kutoka kwa mtumiaji ili kuweka kutatuwa hoja mbalimbali
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifnza jinsi ya ku upload file kwenye database. Kisha utajifunza jinsi ya kulisoma faili hilo kwa kutumia php
Soma Zaidi...