Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu class inheritance kwenye object oriented programming.
Inheritance ni nini?
Hiki ni kitendo kuwa class moja inarithi property na method kutoka class nyingine. Hii inayorithi itaitwa child class yaani class toto. Katika kurithi huku tutazingatia access modifier, hivyo basi tutarithi method na property ambazo ni public au protected. Class ambayo inayorithi (inherited) huongezewa keyword extends wakati wa kuitengeneza.
Mfano:
<?php
class Gari {
}
class prado extends Gari {
}
?>
Hapo class Gari huitwa parent class na hiyo class prado huitwa child class. Sasa ngoja tuone namna ambavyo tunaweza kurithi method na property ambazo ni public ama protected.
<?php
class Gari
{
public $jina;
protected $speed;
public function __construct($jina, $speed)
{
$this->jina = $jina;
$this->speed = $speed;
}
protected function tangazo()
{
echo "Tunauza {$this->jina} yenye speed ya {$this->speed}.";
}
}
class Prado extends Gari
{
public function tangazo_jipya()
{
//method tangazo ni protected
$this->tangazo();
}
}
$Toyota = new Prado("Toyota", "180 km/h");
$Toyota->tangazo_jipya();
?>
Hapo utaona method tangazo() ni protected lakini tumeweza kuitumia kwenye child class prado(). Hii ni kwa sababu class Prado() imerithi property na method kutoka kwenye parent class Gari().
Kwa kutumia mfabo huo hata property ikiwa ni protected unaweza kuitumia ndani ya child class bila ya wasi wasi wowote.
Hapo kuna kitu kipya umekiona {$this->jina} umeona hapo tumetumia mabano {} haya hapo yametumika ili tuweze kutumia hizo property kwenye string. Hii kitaalamu inaitwa string interpolation. Angalia mfano mmoja hapo chini
<?php
$x = 4;
$b = 6;
$z = $x +$b;
echo "jumala ya {$x} na {$b} ni {$z}";
jumala ya ">...
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku upload mafaili kwenye server kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...Katika soko hili takwenda kujufunza jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP. Hii itasaidia kama unataka kutuma OTP yaqni Onetime password
Soma Zaidi...Katika somo hil utawenda kujifunza jinsi ya ku edit post kwenye databse
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunzo kuhusu teknolojia ya ORM na inavyotumika kulinda usalama wa database
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya ku connect database, kwa kutumia php
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia constatnt kwenye class.
Soma Zaidi...Haya ni mabo ya kuzingatia unapo encode ama ku decode data za json
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jisni ya kudhibiti error ambazo zinaweza kutokea wakati wa ku encode na ku decoe json data
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika constant kwenye PHP. Pia utajifunza utofauti wake na variable
Soma Zaidi...atika somo hli tutakwenda kujifunza kuhusu kitu kinachitwa cron job. ni moja ya teknolojia zinazotumika kufanya kazi zinazofanyika automatic
Soma Zaidi...