PHP - somo la 5: Maana ya function na jinsi inavyotengenezwa kwa ktumia PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye PHP na jinsi ya kuweza kuzitumia
PHP FUNCTIONS:
Katika programming language, php imepata ubora wake kwa kuwa na hiki kipengele cha functions. Katika php kuna functions zaidi ya 1000. pia php inakupa uwezo wa wewe kuandika function yako mwenyewe kulingana na matarajio yako. Hivyo basi zipo funtion ambazo tayari zipo. Hizi zinaitwa built-in PHP functions. Na kuna hizo ambazo unaweka mwenyewe, hizi huitwa user defined functions.
Sasa function ni nini hasa?
Function ya kikundi cha maelekezo (block of statement) katika code za php ambazyo huweza kutumika zaidi na zaidi katika program. Tofauti na statement nyingine kama echo na print, ambazo huleta matokea punde tu ukiran code ama ukurasa ukufunguliwa au kurefresh. Function zenyewe mpaka zitu ziitajwe kwenye code yaani (by calling the functions).
Katika somo hili tutaona baadhi ya mifano ya built-in-function na jinsi zinavyofanya kazi kwa mifano. Hapa tutaangalia hasa kwenye string. Kama tulivyojifunzakatika somo lililopita.
KANUNI ZA FUNCTION (built-in-php functions)
1.Kwanza ni jina la function ila lisianze na namba mfano salamu
2.Kisha linafatiwa na mabano () mfano salamu()
3.Ndani ya mabano kunawekwa ujumbe ama maudhui ya hiyo function mfano salami(hujamb)
4.Kisha coloni ; mfano salamu salami(hujamb);
Tutajifunza kanuni nyingine za function kwenye somo linalofata kuhusu user defined functions.
FUNCTIONS KWENYE STRING:
1.Kujuwa idadi ya character kwenye string. Kama unataka kujuwa je katika string kuna herufi ngapi ama namba ngapi ama character ngapi, basi tunatumia strlen() function. Neno hili ni ufupisho wa maneno string length.
Mfano:
echo strlen (“bongoclass”);
?>
Hii itakupa matokeo 10 kumaanisha kuwa kuna character 10.
2.Kwa kutumia php functions unaweza kubadili ama ku replace baadhi ya maandishi ndani ya string. Function inayotumika ni str_replace (). Kwa mfano katika mfano ufuatao nita replace neno bongoclass na kwa google.
echo str_replace ('karibu', 'bongoclass', 'welcome google');
?>
Hii itakupa matokeo welcome google maneno ya kwanza utaona yamebadilishwa kwa maneno ya pili.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 web hosting 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
PHP - 9: Jinsi ya kuandika array kwenye PHP na kuzifanyia kazi
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array kwenye php, na jinsi zinavyoweza kufanya kazi
Soma Zaidi...PHP - somo la 3: Maana ya variable na inavyoandika kwenye PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza kujusu PHP variable, maana yake na sheria za uandishi wa variable
Soma Zaidi...PHP - somo la 41: Jinsi ya kufanya hashing kwenye PHP
Katika somo hili utajifunza jinsiya kufanya hashing taarifa muhimu kama password. Kufanya hashing kunaongeza usalama wa taarifa za waumiaji kwenye blog yako.
Soma Zaidi...PHP BLOG - somo la 10: Jinsi ya kufanya sanitization
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufanya sanitization kwenye user input ili kuzuia sql injection kwenye database.
Soma Zaidi...PHP - somo la 47: Jifunze kuhusu sql injection na kuizuia
Katika somo hili utajwenda kujifunza jinsi ya kuzuia hacking kwenye website yako
Soma Zaidi...PHP - somo la 32: Jinsi ya kutumia filter_var() function kwenye PHP
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia filter_var() function kwa ajili ya kuchuja code zilizo hatari kwenye PHP file
Soma Zaidi...