PHP - somo la 1: Maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi
Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi
MAFUNZO YA PHP SOMO LA KWANZA
Mahitaji ya course:
1.Uwe na kompyuta ama smartphone
2.Uwe na uelewa wa html
3.Uwe mjanga, wa kuweza kutumia simu ama kompyuta yako vyema
4.Ujuwe kusoma na kuandika
5.Kuwa na hamu ya kutaka kujuwa.
Utangulizi:
PHP ni katika lugha za kikompyuta inayotumika kwenye server. Php hutumika katika kutengeneza kurasa za wavuti kama ilivyo html. Php pia inaweza kutumika katika kutengeneza software. Php ni moja katika lugha zinazotumika sana katika blog kama wordpress na katika social media kama facebook. Php ni free kibiashara na hata binafsi.
Php ilianzishwa mwaka 1994 na mmarekani aliyejulikana kwa jina la Rasmus Lerdorf, ikiwa kama home project. Nika katika luga za kikompuata zilizo rahisi kujifunza, hata hivyo syntax yake inaweza kuwa ngumu kuliko javascript na lugha nyingine.
PHP ni nini?
Php ni kifupisho cha maneno Hypertext Preprocessor. Php hutengeneza kurasa za wavuti kama html, pia huweza kutumiwa ndani ya html ama html ikatumiwa ndani ya php. Kwa pamoja tukaweza kuhama kutokakurasa kwenda kurasa ndio maana php ikawa nayo ipo katika hypertext kama ilivyo html. Tofauti ni kuwa php kwanza code hufanyiwa processing kwenye server, kisha ndipo server hutuma matokeo kwenye browser kama html code ama plain text kwa maana hii ndipo tunapata preprocessor kwa maana kwana code zinachakatwa kwenye server kisha matokeo ndipo hutolewa kama html ama plain text kwenye browser.
NINI PHP HUFANYA:
1.Hutengeneza dynamic web page
2.Hutengeneza static webpage
3.Huwengeneza web App
Kwa ufupi php ina uweza kufanya mambo haya:-
1.Inaweza kuedit data kwenye database
2.Kuongeza na kupunguza data kwenye database
3.Kujaza fomu za madodoso
4.Kupokea taarifa kutoka katika madodoso (form)
5.Kufunga na kufunguwa database
6.Kufunguwa na kufunga mafaili
7.Kutengeneza dynamic na static web page
8.Kutengeneza system za web App
PHP inafanyaje kazi?
Kwanza browser inapokutana na code za php, code hizi hutumwa kwenda kwenye server. Server inachakata code za php na kurudisha matokeo kwenye browser kama plain text, na hapo html huchukuwa nafasi yake, hatimaye maudhui yanaonekana kwenye browser kama html.
Server ni nini?
Server ni kompyuta inayohudumia kompyuta nyingine. Zipo kompyuta maalumu zinafanya kazi ya kuhudumia kompyuta nyingine, lakini kompyuta yako mwenyewe pia unaweza kuifanya iwe server na kuhudumia kompyuta nyingine. Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia sikuhisi hata simu inaweza kuwa server na kuhudumia kompyuta.
Browseer yako kama chrome, firefox na opera zinaelewa html, javascript, xml, css lakini haziwezi kuelewa php. Hivyo ili code za php uweze kuzirun kwenye browser ni lazima uwe na server ambayo inachakata php na kurudisha majibu kama plain text.
KUIANDAA SIMU NA KOMPYUTA YAKO KUTUMIA PHP
Kama nilivyokueleza kuwa php inahitaji server. Hivyo unatakiwa uwe na App ambazo zitaweza kufanya simu yako iwe localhost server. Fuata hatuwa zifuatazo:-
1. Kwa watumiaji wa Simu
Kama wewe unatumia simu basi fuata maelekezo haya ili kuweza kuandaa simu yako kwa ajili ya mafunzo. Hapa nitakuletea list za App ambazo inatakiwa uwe nazo. List hii nimeiweka katiuka vifungu viwili ambavyo ni:-
A. Text editor: Hakikisha una moja kati ya App hizi, kama si u yako itagoma utacheki nyingine.
1. Acode - code editor | FOSS (nakushauri uchukuwe hii)
2. DroidEdit (free code editor)
3. Code Editor- Program on Mobile
B. Local host server Hakikisha una moja kati ya server zifuatazo:- Ila ninakushauri uwe na hiyi ya kwanza hapo.
1. AWebServer ( Http Web Server (nakushauri uchukuwe hii)
3. Web Server PHP/MyAdmin/MySQL
JINSI YA KUANZA KUTUMIA:
1. Kwenye simu yako tengeneza fol...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Faida za kiafya za kula Viazi mbatata
Viazi mbatata ni katika vyakula ambavyo hupatikana karibia dunia yote. Viazi hivi vimekuwa ni lishe kubwa sana. Ila je unajuwa hasa ni faida gani za kiafya hupatikana kwenye viazi hivi?
Soma Zaidi...PHP - somo la 22: Kutafuta jumla, wastani na idani ya vitu kwenye database kw akutumia PHP
Katika somo hili utakwenda jifunza jinsi ya kuhesabu row kwenye database, kutafuta wastani wa taarifa kwenye database na kutafuta idadi yake.
Soma Zaidi...PHP somo la 49: utangulizi wa Object Oriented Programming katika PHP
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya PHP na hapa tunaaza rasmi advanced PHP. tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye PHP. Ni vyema kabla ya kuanza course hii ya advanced PHP uwe una uelewa wa kutosha kuhusu mafunzo yetu ya PHP.
Soma Zaidi...PHP somo la 74: aina za http headerna server variable
Katika somo hii utakwenda kujifunza aina za http header na server variable. Hapa tutakwenda kuchambuwa mgawanyiko wa httpheader na kazi zake.
Soma Zaidi...PHP BLOG - somo la 12: Jinsi ya kutumia prepared statement kwenye kusoma post za blog
Katika somo hili tutakwenda kutumia prepared ststement kwenye ku fetch data kutoka kwenye database.
Soma Zaidi...PHP somo la 90: Jinsi ya kutumia json data kama blog post
Katika somo hili utaweza kujifunza ni kwa nambna gani utaweza kutengeneza blog post na kuisoma kwa kutumia data za json
Soma Zaidi...