image

PHP - somo la 1: Maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi

MAFUNZO YA PHP SOMO LA KWANZA

Mahitaji ya course:
1.Uwe na kompyuta ama smartphone
2.Uwe na uelewa wa html
3.Uwe mjanga, wa kuweza kutumia simu ama kompyuta yako vyema
4.Ujuwe kusoma na kuandika
5.Kuwa na hamu ya kutaka kujuwa.


Utangulizi:
PHP ni katika lugha za kikompyuta inayotumika kwenye server. Php hutumika katika kutengeneza kurasa za wavuti kama ilivyo html. Php pia inaweza kutumika katika kutengeneza software. Php ni moja katika lugha zinazotumika sana katika blog kama wordpress na katika social media kama facebook. Php ni free kibiashara na hata binafsi.

Php ilianzishwa mwaka 1994 na mmarekani aliyejulikana kwa jina la Rasmus Lerdorf, ikiwa kama home project. Nika katika luga za kikompuata zilizo rahisi kujifunza, hata hivyo syntax yake inaweza kuwa ngumu kuliko javascript na lugha nyingine.

PHP ni nini?
Php ni kifupisho cha maneno Hypertext Preprocessor. Php hutengeneza kurasa za wavuti kama html, pia huweza kutumiwa ndani ya html ama html ikatumiwa ndani ya php. Kwa pamoja tukaweza kuhama kutokakurasa kwenda kurasa ndio maana php ikawa nayo ipo katika hypertext kama ilivyo html. Tofauti ni kuwa php kwanza code hufanyiwa processing kwenye server, kisha ndipo server hutuma matokeo kwenye browser kama html code ama plain text kwa maana hii ndipo tunapata preprocessor kwa maana kwana code zinachakatwa kwenye server kisha matokeo ndipo hutolewa kama html ama plain text kwenye browser.

 

NINI PHP HUFANYA:
1.Hutengeneza dynamic web page
2.Hutengeneza static webpage
3.Huwengeneza web App

 

Kwa ufupi php ina uweza kufanya mambo haya:-
1.Inaweza kuedit data kwenye database
2.Kuongeza na kupunguza data kwenye database
3.Kujaza fomu za madodoso
4.Kupokea taarifa kutoka katika madodoso (form)
5.Kufunga na kufunguwa database
6.Kufunguwa na kufunga mafaili
7.Kutengeneza dynamic na static web page
8.Kutengeneza system za web App

 

PHP inafanyaje kazi?
Kwanza browser inapokutana na code za php, code hizi hutumwa kwenda kwenye server. Server inachakata code za php na kurudisha matokeo kwenye browser kama plain text, na hapo html huchukuwa nafasi yake, hatimaye maudhui yanaonekana kwenye browser kama html.

Server ni nini?
Server ni kompyuta inayohudumia kompyuta nyingine. Zipo kompyuta maalumu zinafanya kazi ya kuhudumia kompyuta nyingine, lakini kompyuta yako mwenyewe pia unaweza kuifanya iwe server na kuhudumia kompyuta nyingine. Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia sikuhisi hata simu inaweza kuwa server na kuhudumia kompyuta.

Browseer yako kama chrome, firefox na opera zinaelewa html, javascript, xml, css lakini haziwezi kuelewa php. Hivyo ili code za php uweze kuzirun kwenye browser ni lazima uwe na server ambayo inachakata php na kurudisha majibu kama plain text.

 

KUIANDAA SIMU NA KOMPYUTA YAKO KUTUMIA PHP
Kama nilivyokueleza kuwa php inahitaji server. Hivyo unatakiwa uwe na App ambazo zitaweza kufanya simu yako iwe localhost server. Fuata hatuwa zifuatazo:-

1. Kwa watumiaji wa Simu

Kama wewe unatumia simu basi fuata maelekezo haya ili kuweza kuandaa simu yako kwa ajili ya mafunzo. Hapa nitakuletea list za App ambazo inatakiwa uwe nazo. List hii nimeiweka katiuka vifungu viwili ambavyo ni:-

A. Text editor: Hakikisha una moja kati ya App hizi, kama si u yako itagoma utacheki nyingine.

1. Acode - code editor | FOSS (nakushauri uchukuwe hii)

2. DroidEdit (free code editor)

3. Code Editor- Program on Mobile

 

B. Local host server Hakikisha una moja kati ya server zifuatazo:- Ila ninakushauri uwe na hiyi ya kwanza hapo.

1. AWebServer ( Http Web Server  (nakushauri uchukuwe hii)

2. KSWEB: web developer kit...



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 437


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

PHP somol la 55: PHP Abstract Class na abstract method
Katika somo hili utakwenda kujifunza concept mpya ya abstract class na abstract method kwenye OOP. Soma Zaidi...

PHP - somo la 47: Jifunze kuhusu sql injection na kuizuia
Katika somo hili utajwenda kujifunza jinsi ya kuzuia hacking kwenye website yako Soma Zaidi...

PHP somo la 56:class interface na polymorphism kwenye PHP OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya interface na concept ya polymorphism kwenye PHP OOP. Soma Zaidi...

PHP - somo la 41: Jinsi ya kufanya hashing kwenye PHP
Katika somo hili utajifunza jinsiya kufanya hashing taarifa muhimu kama password. Kufanya hashing kunaongeza usalama wa taarifa za waumiaji kwenye blog yako. Soma Zaidi...

PHP somo la 75: Content-Type Header
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu content-type header. Soma Zaidi...

PHP - somo la 45: Jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP
Katika soko hili takwenda kujufunza jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP. Hii itasaidia kama unataka kutuma OTP yaqni Onetime password Soma Zaidi...

PHP somo la 71: Jinsi ya kutengeneza PDF kwa kutumia PHP na library ya tcpdf
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku generate PDF automatik kutoka kwenye php code , html, javascript na css. Soma Zaidi...

PHP somo la 65: Jinsi ya kusoma data kwenye database kwa kutumia PDO
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma data kwenye database kwa kutumia PDO. Soma Zaidi...

PHP somo la 49: utangulizi wa Object Oriented Programming katika PHP
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya PHP na hapa tunaaza rasmi advanced PHP. tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye PHP. Ni vyema kabla ya kuanza course hii ya advanced PHP uwe una uelewa wa kutosha kuhusu mafunzo yetu ya PHP. Soma Zaidi...

PHP somo la 59: static property kwenye PHP
Katika somo hili utakwend kujifunza kuhusu static property na jnsi inavyotumika Soma Zaidi...

PHP somo la 54: class constant kwenye php
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia constatnt kwenye class. Soma Zaidi...

PHP BLOG - somo la 8: Jinsi ya kufuta post kwenye database
katika post hii utajifunza jinsi ya kufuta post kwenye database. pia utajifunza jinsi ya kufuta picha kwenye server Soma Zaidi...