PHP - somo la 1: Maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi

MAFUNZO YA PHP SOMO LA KWANZA

Mahitaji ya course:
1.Uwe na kompyuta ama smartphone
2.Uwe na uelewa wa html
3.Uwe mjanga, wa kuweza kutumia simu ama kompyuta yako vyema
4.Ujuwe kusoma na kuandika
5.Kuwa na hamu ya kutaka kujuwa.


Utangulizi:
PHP ni katika lugha za kikompyuta inayotumika kwenye server. Php hutumika katika kutengeneza kurasa za wavuti kama ilivyo html. Php pia inaweza kutumika katika kutengeneza software. Php ni moja katika lugha zinazotumika sana katika blog kama wordpress na katika social media kama facebook. Php ni free kibiashara na hata binafsi.

Php ilianzishwa mwaka 1994 na mmarekani aliyejulikana kwa jina la Rasmus Lerdorf, ikiwa kama home project. Nika katika luga za kikompuata zilizo rahisi kujifunza, hata hivyo syntax yake inaweza kuwa ngumu kuliko javascript na lugha nyingine.

PHP ni nini?
Php ni kifupisho cha maneno Hypertext Preprocessor. Php hutengeneza kurasa za wavuti kama html, pia huweza kutumiwa ndani ya html ama html ikatumiwa ndani ya php. Kwa pamoja tukaweza kuhama kutokakurasa kwenda kurasa ndio maana php ikawa nayo ipo katika hypertext kama ilivyo html. Tofauti ni kuwa php kwanza code hufanyiwa processing kwenye server, kisha ndipo server hutuma matokeo kwenye browser kama html code ama plain text kwa maana hii ndipo tunapata preprocessor kwa maana kwana code zinachakatwa kwenye server kisha matokeo ndipo hutolewa kama html ama plain text kwenye browser.

 

NINI PHP HUFANYA:
1.Hutengeneza dynamic web page
2.Hutengeneza static webpage
3.Huwengeneza web App

 

Kwa ufupi php ina uweza kufanya mambo haya:-
1.Inaweza kuedit data kwenye database
2.Kuongeza na kupunguza data kwenye database
3.Kujaza fomu za madodoso
4.Kupokea taarifa kutoka katika madodoso (form)
5.Kufunga na kufunguwa database
6.Kufunguwa na kufunga mafaili
7.Kutengeneza dynamic na static web page
8.Kutengeneza system za web App

 

PHP inafanyaje kazi?
Kwanza browser inapokutana na code za php, code hizi hutumwa kwenda kwenye server. Server inachakata code za php na kurudisha matokeo kwenye browser kama plain text, na hapo html huchukuwa nafasi yake, hatimaye maudhui yanaonekana kwenye browser kama html.

Server ni nini?
Server ni kompyuta inayohudumia kompyuta nyingine. Zipo kompyuta maalumu zinafanya kazi ya kuhudumia kompyuta nyingine, lakini kompyuta yako mwenyewe pia unaweza kuifanya iwe server na kuhudumia kompyuta nyingine. Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia sikuhisi hata simu inaweza kuwa server na kuhudumia kompyuta.

Browseer yako kama chrome, firefox na opera zinaelewa html, javascript, xml, css lakini haziwezi kuelewa php. Hivyo ili code za php uweze kuzirun kwenye browser ni lazima uwe na server ambayo inachakata php na kurudisha majibu kama plain text.

 

KUIANDAA SIMU NA KOMPYUTA YAKO KUTUMIA PHP
Kama nilivyokueleza kuwa php inahitaji server. Hivyo unatakiwa uwe na App ambazo zitaweza kufanya simu yako iwe localhost server. Fuata hatuwa zifuatazo:-

1. Kwa watumiaji wa Simu

Kama wewe unatumia simu basi fuata maelekezo haya ili kuweza kuandaa simu yako kwa ajili ya mafunzo. Hapa nitakuletea list za App ambazo inatakiwa uwe nazo. List hii nimeiweka katiuka vifungu viwili ambavyo ni:-

A. Text editor: Hakikisha una moja kati ya App hizi, kama si u yako itagoma utacheki nyingine.

1. Acode - code editor | FOSS (nakushauri uchukuwe hii)

2. DroidEdit (free code editor)

3. Code Editor- Program on Mobile

 

B. Local host server Hakikisha una moja kati ya server zifuatazo:- Ila ninakushauri uwe na hiyi ya kwanza hapo.

1. AWebServer ( Http Web Server  (nakushauri uchukuwe hii)

2. ...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 1071

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

PHP somo la 90: Jinsi ya kutumia json data kama blog post

Katika somo hili utaweza kujifunza ni kwa nambna gani utaweza kutengeneza blog post na kuisoma kwa kutumia data za json

Soma Zaidi...
PHP - somo la 10: Jinsi ya kundika condition statement if, ifelse na switch case

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu condition statements if, ifelse na switch case. Hata utajifunza jnsi ya kuziandika na zinavyofanya kazi

Soma Zaidi...
PHP - somo la 38: Jinsi ya ku upload mafaili zaidi ya moja kwa kutumia PHP

katika somo hili utajifunza jinsi ya ku upload multiple file yaani mafaili mengi kwa wakati mmoja kwa kutumia PHP

Soma Zaidi...
PHP somo la 71: Jinsi ya kutengeneza PDF kwa kutumia PHP na library ya tcpdf

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku generate PDF automatik kutoka kwenye php code , html, javascript na css.

Soma Zaidi...
PHP somo la 50: Jinsi ya kutengeneza CLASS na OBJECT kwenye PHP OOP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza class na object. Tunakwenda kutumia mfano wetu wa hapo juu kwa ajili ya kukamilisha somo hili.

Soma Zaidi...
PHP somo la 96: Jinsi ya kutengeneza ORM inayofanya CDRUDE operation

Katika somo hili utakwenda Jinsi ya kutengeneza ORM inayofanya CDRUDE operation.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 46: Nini maana ya cronjob na matumizi yake

Katika somo hili utajifunza kuhusu cronjob na matumizi yake kwenye PHP

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 6: Jinsi ya kutengeneza dashboard kwa ajili ya blog

katika post hii utajifunza jinsi ya kutengeneza ukurasa wa dashboard kwa ajili ya kutibti post

Soma Zaidi...
PHP somo la 58: static method kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu static method na inavtotumika kwenye OOP

Soma Zaidi...
PHP - somo la 25: Jinsi ya kukusanya taarifa kutoka kwenye html form kwa kutumia php

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kukusanya taarifa ambazo watu wamezijaza kwa kutumia fomu ya html. Kisha utajifunza jinsi ya kuzisoma hizo taarifa.

Soma Zaidi...