Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.
1. Dalili ya kwanza ni maumivu wakati wa kujisaidia.
Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa au tayari mishipa midogo kwenye haja kubwa ishapasuka Mgonjwa uhisi maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa.
2. Kutokwa na damu wakati wa kujisaidia.
Kwa sababu mishipa ya sehemu ya haja kubwa ishapasuka kwa hiyo Mgonjwa anapojisaidia damu utoka wakati wa kujisaidia.
3. Kuwepo kwa miwasho kwenye sehemu ya haja kubwa.
Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa miwasho inakuwepo mingi na kunakuwepo na kishawishi cha kujikuna mara kwa mara hali inayosababisha kuenea kwa magonjwa mengine kama vile minyoo na Typhoid.
4. Kuwepo na uvimbe na kinyama kwenye sehemu za siri,
Hali hiyo Usababishwa na kupasuka kwa mishipa midogo sehemu ya haja kubwa hali inayopelekea kuota vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
5. Haja kubwa kujitokeza kwa mda wowote.
Kuna wakati mwingine haja kubwa uja mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo nafasi ndogo sehemu ya kuhifadhiwa haja kubwa kwa sababu ya kuota kwa vinyama au uvimbe sehemu hizo.
6. Choo juwa kigumu au mara nyingine kukosa kabisa kwa siku tatu na pia uambatana na Maumivu makali ya kiuno na mgongo.
7. Tumbo kujaa gesi mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.
8. Kuhisi njaa mara kwa mara, hali hii utokea kwa sababu ya kutoa haja kubwa mara kwa mara au wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.
9. Baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa matibabu ya mapema ni lazima ili kuepuka madhara makubwa zaidi.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa usafi katika maisha ya mwanadamu au mwili wa binadamu.
Soma Zaidi...Katika post hii utakwend akujifunza kuhusu tatizo la kuwa na vijiwe kwenye ini vijiwe hivi hufahamika kama intrahepatic stones.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na fangasi
Soma Zaidi...Posti hii itakwenda kuelezea mambo machache kuhusu ugonjwa wa kisukari
Soma Zaidi...Makala hii itakwenda kukupa elimu juu ya maradhi haya ya ukimwi, dalili zake, tiba na kinga zake na mengineyo zaidi.
Soma Zaidi...Dermatitis ni hali inayofanya ngozi yako kuwa nyekundu na kuwasha. Ni kawaida kwa watoto, lakini inaweza kutokea katika umri wowote. Hakuna tiba iliyopatikana ya ugonjwa wa Dermatitis
Soma Zaidi...Post hii itakwena kukufundisha kuhusu historia fupi ya Ukimwi na matibabu yake. Ni wapi wapo hatarini kupata maambukizi na ni kitu gani wafanye?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia kuaribika kwa figo, hizi ni njia zinazotumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuaribika kwa figo na hasa wale ambao hawajapata tatizo hili wazitumie ili tuone kama tutaweza kupunguza tatizo hili.
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Swali langu: Ukiwa na areji , afu kupata muwasho korodani unapo jikuna unga kutoka nayo fangasi?
Soma Zaidi...