picha

Dalili za ugonjwa wa Bawasili

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.

Dalili za ugonjwa wa Bawasili.

1. Dalili ya kwanza ni maumivu wakati wa kujisaidia.

Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa au tayari mishipa midogo kwenye haja kubwa ishapasuka Mgonjwa uhisi maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa.

 

2. Kutokwa na damu wakati wa kujisaidia.

Kwa sababu mishipa ya sehemu ya haja kubwa ishapasuka kwa hiyo Mgonjwa anapojisaidia damu utoka wakati wa kujisaidia.

 

3. Kuwepo kwa miwasho kwenye sehemu ya haja kubwa.

Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa miwasho inakuwepo mingi na kunakuwepo na kishawishi cha kujikuna mara kwa mara hali inayosababisha kuenea kwa magonjwa mengine kama vile minyoo na Typhoid.

 

4. Kuwepo na uvimbe na kinyama kwenye sehemu za siri,

Hali hiyo Usababishwa na kupasuka kwa mishipa midogo sehemu ya haja kubwa hali inayopelekea kuota vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.

 

5. Haja kubwa kujitokeza kwa mda wowote.

Kuna wakati mwingine haja kubwa uja mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo nafasi ndogo sehemu ya kuhifadhiwa haja kubwa kwa sababu ya kuota kwa vinyama au uvimbe sehemu hizo.

 

6. Choo juwa kigumu au mara nyingine kukosa kabisa kwa siku tatu na pia uambatana na Maumivu makali ya kiuno na mgongo.

 

7. Tumbo kujaa gesi mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.

 

8. Kuhisi njaa mara kwa mara, hali hii utokea kwa sababu ya kutoa haja kubwa mara kwa mara au wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.

 

9. Baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa matibabu ya mapema ni lazima ili kuepuka madhara makubwa zaidi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3530

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Dalili za vidonda vya tumbo, matibabu na dawa zake, sababu za kutokea kwake

Utajifunza chanzo cha vidonda vya tumbo, dalili zake, dawa na matibabu yake pamoja na njia za kujilinda na vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi: Ni hatari?

Kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi, kitaalamu kama Menorrhagia, ni hali inayowapata wanawake wengi. Ingawa si kila mara ni ishara ya ugonjwa mbaya, damu nyingi kupita kiasi inaweza kusababisha upungufu wa damu mwilini (anemia) na kuathiri kwa kiasi kikubwa maisha ya kila siku. Makala hii inaelezea nini kinachozingatiwa kuwa "damu nyingi," sababu zake, na wakati muafaka wa kutafuta msaada wa kitaalamu.

Soma Zaidi...
Dalili za kifua kikuu (tuberculosis)

Kifua kikuu ni ugonjwa sugu wa kuambukiza na anuwai ya magonjwa ya kiafya yanayosababishwa na Mycobacterium tuberculosis complex. Kwa binadamu sababu ya kawaida ni Mycobacterium tuberculosis.

Soma Zaidi...
Dalili za fangasi Mdomoni.

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za fangasi Mdomoni kwa watoto, vijana, watu wazima na mama wanaonyonyeshwa.

Soma Zaidi...
Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Vyakula Vinavyoongeza Kinga ya Mwili.

​Blogu hii inaangazia umuhimu wa lishe bora katika kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili. Tutajadili vyakula mahususi vyenye virutubisho muhimu, umuhimu wa vitamini na madini, pamoja na ukweli wa kisayansi kuhusu jinsi lishe inavyochangia afya yako kwa ujumla.

Soma Zaidi...