picha

Dalili za ugonjwa wa Bawasili

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.

Dalili za ugonjwa wa Bawasili.

1. Dalili ya kwanza ni maumivu wakati wa kujisaidia.

Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa au tayari mishipa midogo kwenye haja kubwa ishapasuka Mgonjwa uhisi maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa.

 

2. Kutokwa na damu wakati wa kujisaidia.

Kwa sababu mishipa ya sehemu ya haja kubwa ishapasuka kwa hiyo Mgonjwa anapojisaidia damu utoka wakati wa kujisaidia.

 

3. Kuwepo kwa miwasho kwenye sehemu ya haja kubwa.

Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa miwasho inakuwepo mingi na kunakuwepo na kishawishi cha kujikuna mara kwa mara hali inayosababisha kuenea kwa magonjwa mengine kama vile minyoo na Typhoid.

 

4. Kuwepo na uvimbe na kinyama kwenye sehemu za siri,

Hali hiyo Usababishwa na kupasuka kwa mishipa midogo sehemu ya haja kubwa hali inayopelekea kuota vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.

 

5. Haja kubwa kujitokeza kwa mda wowote.

Kuna wakati mwingine haja kubwa uja mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo nafasi ndogo sehemu ya kuhifadhiwa haja kubwa kwa sababu ya kuota kwa vinyama au uvimbe sehemu hizo.

 

6. Choo juwa kigumu au mara nyingine kukosa kabisa kwa siku tatu na pia uambatana na Maumivu makali ya kiuno na mgongo.

 

7. Tumbo kujaa gesi mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.

 

8. Kuhisi njaa mara kwa mara, hali hii utokea kwa sababu ya kutoa haja kubwa mara kwa mara au wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.

 

9. Baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa matibabu ya mapema ni lazima ili kuepuka madhara makubwa zaidi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3454

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰3 ai web app     πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuishi na mtu mwenye matatizo ya afya ya akili.

​Kuishi na mtu anayekabiliwa na changamoto za afya ya akili ni safari inayohitaji subira, elimu, na mipaka ya kijamii iliyo thabiti. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu namna ya kutoa msaada bila kupoteza ustawi wako mwenyewe. Tunachambua mbinu za mawasiliano, umuhimu wa kutoa nafasi, na jinsi ya kuunda mazingira ya kuaminiana, huku tukisisitiza umuhimu wa msaada wa kitaalamu na utunzaji binafsi kwa walezi (caregivers

Soma Zaidi...
Tufanyeje ili kuepuka kuaribika kwa figo?

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia kuaribika kwa figo, hizi ni njia zinazotumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuaribika kwa figo na hasa wale ambao hawajapata tatizo hili wazitumie ili tuone kama tutaweza kupunguza tatizo hili.

Soma Zaidi...
Je minyoo inaweza kusababisha mmeng'enyo wa chakula kuwa dhaifu?

Mfumo wa chakula unaweza kuwa dhaifu kwa sababu nyingi ikiwepo vyakula vyenyewe, vinywaji ama maradhi. Vipi kuhusu minyoo? Endelea na makala hii utajifunza zaidi.

Soma Zaidi...
Maumivu ya nyonga kwa wanawake: Je, yanamaanisha nini?

Maumivu ya nyonga (pelvic pain) ni changamoto inayowakabili wanawake wengi, yakijitokeza katika maeneo ya chini ya kitovu hadi kwenye mapaja. Makala haya yanachunguza visababishi mbalimbali vya maumivu haya, kuanzia sababu za kawaida za mfumo wa uzazi hadi matatizo ya mfumo wa mmeng'enyo wa chakula na misuli, huku yakisisitiza umuhimu wa utambuzi sahihi wa kitabibu.

Soma Zaidi...