picha

Dalili za ugonjwa wa Bawasili

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.

Dalili za ugonjwa wa Bawasili.

1. Dalili ya kwanza ni maumivu wakati wa kujisaidia.

Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa au tayari mishipa midogo kwenye haja kubwa ishapasuka Mgonjwa uhisi maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa.

 

2. Kutokwa na damu wakati wa kujisaidia.

Kwa sababu mishipa ya sehemu ya haja kubwa ishapasuka kwa hiyo Mgonjwa anapojisaidia damu utoka wakati wa kujisaidia.

 

3. Kuwepo kwa miwasho kwenye sehemu ya haja kubwa.

Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa miwasho inakuwepo mingi na kunakuwepo na kishawishi cha kujikuna mara kwa mara hali inayosababisha kuenea kwa magonjwa mengine kama vile minyoo na Typhoid.

 

4. Kuwepo na uvimbe na kinyama kwenye sehemu za siri,

Hali hiyo Usababishwa na kupasuka kwa mishipa midogo sehemu ya haja kubwa hali inayopelekea kuota vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.

 

5. Haja kubwa kujitokeza kwa mda wowote.

Kuna wakati mwingine haja kubwa uja mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo nafasi ndogo sehemu ya kuhifadhiwa haja kubwa kwa sababu ya kuota kwa vinyama au uvimbe sehemu hizo.

 

6. Choo juwa kigumu au mara nyingine kukosa kabisa kwa siku tatu na pia uambatana na Maumivu makali ya kiuno na mgongo.

 

7. Tumbo kujaa gesi mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.

 

8. Kuhisi njaa mara kwa mara, hali hii utokea kwa sababu ya kutoa haja kubwa mara kwa mara au wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.

 

9. Baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa matibabu ya mapema ni lazima ili kuepuka madhara makubwa zaidi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3796

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu ugonjwa wa vidonda vya tumbo (Peptic ulcers)

Vidonda vya tumbo ni vidonda vilivyo wazi vinavyotokea kwenye utando wa ndani wa umio, tumbo na sehemu ya juu ya utumbo wako. Dalili ya kawaida ya Peptic ulcer ni maumivu ya tumbo. Vidonda vya tumbo ni pamoja na: Vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani

Soma Zaidi...
Upele wa vipele (Shingles): Dalili na matibabu.

Upele wa vipele (Shingles), unaojulikana kitaalamu kama Herpes Zoster, ni ugonjwa wa ngozi unaosababishwa na kirusi kilekile kinachosababisha tetekuwanga (Chickenpox). Baada ya mtu kupona tetekuwanga, kirusi hicho hubaki kimejificha katika mfumo wa neva kwa miaka mingi. Kinapochochewa na kupungua kwa kinga ya mwili, uzee, au msongo wa mawazo, kirusi hujitokeza tena kama upele wa vipele. Makala haya yanaelezea dalili zake na jinsi ya kupata matibabu ya haraka.

Soma Zaidi...
Gout (Ugonjwa wa baridi ya yabisi): Dalili na vyakula vya kuepuka.

Gout ni aina ngumu ya ugonjwa wa baridi ya yabisi (arthritis) inayojulikana kwa kusababisha maumivu makali ya ghafla, uvimbe, na wekundu kwenye viungo, hasa kidole gumba cha mguu. Hali hii husababishwa na mrundikano wa asidi ya uric (uric acid) kwenye damu, ambayo huunda fuwele (crystals) ndogo zinazochoma viungo. Makala haya yanakupa mwongozo wa kina kuhusu namna ya kutambua dalili za gout na hatua za lishe za kuchukua ili kudhibiti maumivu na kuzuia mashambulizi ya mara kwa mara.

Soma Zaidi...
Madhara ya maambukizi kwenye tumbo

Posti hii inahusu zaidi madhara ya maambukizi kwenye tumbo,hasa pale ambapo mgonjwa hakutibiwa

Soma Zaidi...
Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.

Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo

Soma Zaidi...
​Njia za Kutatua Migogoro Katika Ndoa

​Migogoro katika ndoa ni jambo lisiloepukika, lakini uwezo wa kuitatua ndiyo siri ya ndoa yenye furaha na kudumu. Posti hii inatoa mwongozo wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kukabiliana na kutoelewana, kukuza mawasiliano bora, na kujenga msingi wa kuaminiana kati ya wanandoa.

Soma Zaidi...