Dalili za ugonjwa wa Bawasili
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.
Dalili za ugonjwa wa Bawasili.
1. Dalili ya kwanza ni maumivu wakati wa kujisaidia.
Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa au tayari mishipa midogo kwenye haja kubwa ishapasuka Mgonjwa uhisi maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa.
2. Kutokwa na damu wakati wa kujisaidia.
Kwa sababu mishipa ya sehemu ya haja kubwa ishapasuka kwa hiyo Mgonjwa anapojisaidia damu utoka wakati wa kujisaidia.
3. Kuwepo kwa miwasho kwenye sehemu ya haja kubwa.
Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa miwasho inakuwepo mingi na kunakuwepo na kishawishi cha kujikuna mara kwa mara hali inayosababisha kuenea kwa magonjwa mengine kama vile minyoo na Typhoid.
4. Kuwepo na uvimbe na kinyama kwenye sehemu za siri,
Hali hiyo Usababishwa na kupasuka kwa mishipa midogo sehemu ya haja kubwa hali inayopelekea kuota vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
5. Haja kubwa kujitokeza kwa mda wowote.
Kuna wakati mwingine haja kubwa uja mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo nafasi ndogo sehemu ya kuhifadhiwa haja kubwa kwa sababu ya kuota kwa vinyama au uvimbe sehemu hizo.
6. Choo juwa kigumu au mara nyingine kukosa kabisa kwa siku tatu na pia uambatana na Maumivu makali ya kiuno na mgongo.
7. Tumbo kujaa gesi mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.
8. Kuhisi njaa mara kwa mara, hali hii utokea kwa sababu ya kutoa haja kubwa mara kwa mara au wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.
9. Baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa matibabu ya mapema ni lazima ili kuepuka madhara makubwa zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Mashambulizi ya hofu (Panic Attacks): Hatua za kuchukua yanapotokea.
​Mashambulizi ya hofu (panic attacks) ni hali ya ghafla ya woga mkali inayoweza kuambatana na dalili za kimwili zinazotisha. Makala haya yanafafanua kwa kina nini ni mashambulizi ya hofu, hatua za haraka za kuchukua yanapotokea, na umuhimu wa kutafuta msaada wa kitaalamu ili kudhibiti afya ya akili kwa muda mrefu.
Soma Zaidi...Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa kaswende
Post hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kaswende kwa wajawazito, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa watu wote, kwa sababu ugonjwa huu una dalili ambazo upitia kwa hatua mbalimbali kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume
Suala la nguvu za kiume limekuwa likijadiliwa kwa miaka mingi, mara nyingi likiambatana na ahadi za miujiza na tiba za siri. Makala haya yanachambua ukweli wa kisayansi kuhusu jinsi lishe inavyoweza kuimarisha uwezo wa kiume, yakitaja vyakula halisi vinavyoboresha mzunguko wa damu na homoni, pamoja na kufanya tathmini ya ukweli (fact check) dhidi ya dhana potofu zilizosambaa mitaani.
Soma Zaidi...Namna ya kuangalia Maambukizi kwenye mifupa.
Posti hii inahusu zaidi njia zinazotumika ili kuangalia Maambukizi kwenye mifupa.
Soma Zaidi...Athari za unyanyasaji wa kisaikolojia ndani ya familia.
​Unyanyasaji wa kisaikolojia ndani ya familia ni janga la kimyakimya ambalo huacha makovu yasiyofutika. Tofauti na unyanyasaji wa kimwili, unyanyasaji wa kihisia na kisaikolojia mara nyingi hufichwa nyuma ya kuta za nyumba, ukiathiri afya ya akili, kujiamini, na ustawi wa jumla wa wahanga. Makala haya yanachunguza aina za unyanyasaji huu, athari zake za muda mrefu, na mbinu za kujikomboa ili kujenga mahusiano yenye afya
Soma Zaidi...