Dalili za ugonjwa wa Bawasili
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.
Dalili za ugonjwa wa Bawasili.
1. Dalili ya kwanza ni maumivu wakati wa kujisaidia.
Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa au tayari mishipa midogo kwenye haja kubwa ishapasuka Mgonjwa uhisi maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa.
2. Kutokwa na damu wakati wa kujisaidia.
Kwa sababu mishipa ya sehemu ya haja kubwa ishapasuka kwa hiyo Mgonjwa anapojisaidia damu utoka wakati wa kujisaidia.
3. Kuwepo kwa miwasho kwenye sehemu ya haja kubwa.
Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa miwasho inakuwepo mingi na kunakuwepo na kishawishi cha kujikuna mara kwa mara hali inayosababisha kuenea kwa magonjwa mengine kama vile minyoo na Typhoid.
4. Kuwepo na uvimbe na kinyama kwenye sehemu za siri,
Hali hiyo Usababishwa na kupasuka kwa mishipa midogo sehemu ya haja kubwa hali inayopelekea kuota vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
5. Haja kubwa kujitokeza kwa mda wowote.
Kuna wakati mwingine haja kubwa uja mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo nafasi ndogo sehemu ya kuhifadhiwa haja kubwa kwa sababu ya kuota kwa vinyama au uvimbe sehemu hizo.
6. Choo juwa kigumu au mara nyingine kukosa kabisa kwa siku tatu na pia uambatana na Maumivu makali ya kiuno na mgongo.
7. Tumbo kujaa gesi mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.
8. Kuhisi njaa mara kwa mara, hali hii utokea kwa sababu ya kutoa haja kubwa mara kwa mara au wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.
9. Baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa matibabu ya mapema ni lazima ili kuepuka madhara makubwa zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 ai web app 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
ninaisi kma kunakitu kwenye koo alafu kuna ali ya weupe kwenye ulimi na Mashavu kwa ndan
Weupe kwenye ulimi unaweza kuwa ni hali ya kawaida. Weupe huu ukichanganyika na utandu huwenda ikaashiria uwepo wa hali fulani za kiafya.
Soma Zaidi...Figo ni nini, ni yapi maradhi yake na nitajiepusha vipi na maradhi ya figo
Makala hii itakwenda kukueleza ni nini hasa hizi figo, na ni yapi maradhi yake na ni kwa namna ggani utaweza kujilinda na maradhi ya figo.
Soma Zaidi...Homa ya dengue: Dalili na jinsi inavyoenezwa na mbu.
Homa ya Dengue ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyoambukizwa kwa binadamu kupitia kuumwa na mbu aina ya Aedes aegypti. Ugonjwa huu ni tishio kubwa katika maeneo ya kitropiki na mikoa yenye joto. Ingawa visa vingi ni vya wastani, baadhi ya watu wanaweza kupata Dengue kali (Dengue Hemorrhagic Fever) ambayo inahitaji uangalizi wa haraka wa kimatibabu. Makala hii inaelezea mzunguko wa uenezaji wa virusi hivi na umuhimu wa usafi wa mazingira katika kudhibiti mbu.
Soma Zaidi...Je, kuna vyakula vya kuepuka wakati wa ujauzito?
Lishe bora ni msingi wa ukuaji wa mtoto mwenye afya na ustawi wa mama mjamzito. Hata hivyo, kuna baadhi ya vyakula ambavyo vinaweza kuwa na vimelea hatari, sumu, au kemikali zinazoweza kusababisha madhara makubwa kama vile maambukizi ya bakteria, kuharibika kwa mimba, au matatizo ya ukuaji wa mtoto. Makala hii inaorodhesha vyakula unavyopaswa kuepuka ili kulinda afya yako na ya kiumbe ulichobeba.
Soma Zaidi...Dalili za Homa ya uti wa mgongo (meningitis)
Posti hii inahusu zaidi dalili za Homa ya uti wa mgongo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye maambukizi kwenye uti wa mgongo.
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kitovuni
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya tumbo kitovuni
Soma Zaidi...