Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.
1. Dalili ya kwanza ni maumivu wakati wa kujisaidia.
Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa au tayari mishipa midogo kwenye haja kubwa ishapasuka Mgonjwa uhisi maumivu makali wakati wa kujisaidia haja kubwa.
2. Kutokwa na damu wakati wa kujisaidia.
Kwa sababu mishipa ya sehemu ya haja kubwa ishapasuka kwa hiyo Mgonjwa anapojisaidia damu utoka wakati wa kujisaidia.
3. Kuwepo kwa miwasho kwenye sehemu ya haja kubwa.
Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye sehemu ya haja kubwa miwasho inakuwepo mingi na kunakuwepo na kishawishi cha kujikuna mara kwa mara hali inayosababisha kuenea kwa magonjwa mengine kama vile minyoo na Typhoid.
4. Kuwepo na uvimbe na kinyama kwenye sehemu za siri,
Hali hiyo Usababishwa na kupasuka kwa mishipa midogo sehemu ya haja kubwa hali inayopelekea kuota vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
5. Haja kubwa kujitokeza kwa mda wowote.
Kuna wakati mwingine haja kubwa uja mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo nafasi ndogo sehemu ya kuhifadhiwa haja kubwa kwa sababu ya kuota kwa vinyama au uvimbe sehemu hizo.
6. Choo juwa kigumu au mara nyingine kukosa kabisa kwa siku tatu na pia uambatana na Maumivu makali ya kiuno na mgongo.
7. Tumbo kujaa gesi mara kwa mara kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.
8. Kuhisi njaa mara kwa mara, hali hii utokea kwa sababu ya kutoa haja kubwa mara kwa mara au wakati mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi.
9. Baada ya kuona dalili kama hizi ni vizuri kabisa kuhakikisha kuwa matibabu ya mapema ni lazima ili kuepuka madhara makubwa zaidi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Saratani ya Utumbo ni Saratani ya utumbo mpana (koloni), sehemu ya chini ya mfumo wako wa usagaji chakula. Kwa pamoja, mara nyingi hujulikana kama Saratani ya utumbo mpana. Visa vingi vya Saratani ya utumbo mpana huanza
Soma Zaidi...SABABU ZA KUTOKEA KWA VIDONDA VYA TUMBO Sababu za kawaida za vidonda vya tumbo ni maambukizo na bakteria Helicobacter pylori (H.
Soma Zaidi...Presha ya kushuka ama kitaalamu huitwa hypotension, presha ya kushuka ni hatari kwa afya kama ilivyo presha ya kupanda, maana mwili unakosa nguvu kabisa.
Soma Zaidi...Huwenda ukawa ni moja kati ya watu wanaotaka kujuwa juu ya dalili za ukimwi. Kama wewe ni katika watu hawa tambuwa kuwa kuna dalili za VVU (hiv) na dalili za ukimwi. Makala hii itakwenda kukuletea dalili kuu za mwanzo za VVU na HIV kuanzia wiki tatu za mw
Soma Zaidi...Posti hii inahusu sababu za mwanamke kuumwa tumbo chini ya kitovu, ni tatizo ambalo limewapata wanawake wengi na pengine sababu ni vigumu kupata au pengine zinapatikana lakini kwa kuchelewa hali ambayo usababisha madhara mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye uume, maambukizi hata utokea kwenye kichwa Cha uume kwa kitaalamu huitwa Balanitis, zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa macho, ni ugonjwa ambao ushambulia zaidi sehemu za nje za macho ambazo kwa kawaida uitwa conjunctiva na cornea hizi sehemu zikipata maambukizi zisipotibiwa mapema uweza kusababisha upofu kwa mgonjwa.
Soma Zaidi...posti hii inahusu dalili za ugonjwa wa mapafu.ambapo kitaalamu hujulikana Kama Ugonjwa wa Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS) hutokea wakati Majimaji yanapojaa kwenye vifuko vidogo vya hewa nyororo (alveoli) kwenye mapafu yako. Majimaji mengi kw
Soma Zaidi...Hili ni swali lililowahi kuulizwa na moja ya wasomaji wetu
Soma Zaidi...