picha

Namna ya kutoa huduma kwa mgonjwa wa Dengue.

Posti hii inahusu zaidi huduma anayopaswa kupata mgonjwa wa ndengue, kwa sababu tunafahamu wazi Ugonjwa huu hauna dawa ila kuna huduma muhimu ambayo anaweza kupata na akaendelea vizuri.

Huduma kwa mgonjwa wa Dengue.

1.Kwa hali ya kawaida Ugonjwa ambao unasababishwa na virusi huwa hauna dawa lakini kuna huduma mbalimbali ambazo utolewa na mgonjwa anaweza kupona na kuendelea na hali yake ya kawaida na pengine huwa tiba inayotolewa kuendana na dalili iliyopo kama Mgonjwa anaumwa kichwa dawa ya maumivu utolewa au kama anaharisha dawa ya kuzuia kuharisha utolewa na mambo kama hayo hatimaye Mgonjwa anapata nafuu na kuendelea na shughuli zake kama kawaida.

 

2. Kwa sababu mgonjwa wa Dengue anakuwa na maumivu makali ya kichwa kwa kawaida anapewa dawa ya maumivu na kwa wakati mwingine anapewa maji ambayo yamependekezwa na wizara ya afya ni lingers na pengine Mgonjwa kama ana uwezo wa kunywa maji ya kawaida anaweza kunywa na pia kuna wakati mwingine hali ikiwa imefikia pabaya mgonjwa huwa anatoa damu kwa hiyo kuna hatari ya kupungukiwa damu kwa hiyo anaongezea damu na anapewa dawa ya kusaidia damu iache kutoka mara kwa mara.

 

3. Vile vile Tunapaswa kuzuia Ugonjwa huu kwa kwa kuwapatia watu elimu kuhusu kuwepo kwa ugonjwa huu na kuwapatia mbinu za kujikinga na ugonjwa huu kwa kutumia neti wakati wa usiku kukata vichaka na mazalia ya mbu na kwa wakati mwingine kutumia dawa za kujipaka ili kuweza kupunguza kiwango cha kuenea kwa mbu.

 

4. Kwa hiyo baada ya kujua Ugonjwa huu jamii pia inapaswa ielezwe wazi pale Ugonjwa huu unapotokea ili kuweza kuwafahamisha watu wajue namna ya kujikinga na hasa kuwakinga watoto wadogo na wazee ambao wapo kwenye hatari kubwa ya kupata matatizo zaidi, kwa hiyo na mila na desturi potovu zinapaswa kuepukwa wakati wa kipindi hiki cha Ugonjwa huu ili kuepuka madhara na matatizo yatokanayo na Ugonjwa ambao hauna dawa

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2408

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Maumivu ya meno na ufizi: Tiba za asili na hospitalini.

Maumivu ya meno na matatizo ya ufizi ni miongoni mwa changamoto za kiafya zinazokumba watu wengi duniani. Hali hizi si tu kwamba huleta maumivu makali, bali pia huathiri uwezo wa kula, kuzungumza, na hata ubora wa maisha kwa ujumla. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu sababu za maumivu haya, mbinu za kutuliza maumivu nyumbani, na kwa nini ni muhimu kumuona daktari wa meno (dentist) ili kupata tiba ya kudumu.

Soma Zaidi...
Dalili za madonda ya koo

Posti hii inahusu zaidi magonjwa ya koo, ni ugonjwa unaoshambulia sana sehemu ya koo la hewa, na na huwa na dalili zake kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa ,kwa kawaida Ugonjwa huu utokea kuanzia kwenye wiki ya pili mpaka mwaka mmoja na hapo Ugonjwa unakuwa bado haujaonesha Dalili na Dalili zikishaonekana ni vigumu kutibika.

Soma Zaidi...
Kufunga uzazi (Tubal Ligation): Je, inaweza kurudishwa?

Kufunga uzazi kwa wanawake (Tubal Ligation) ni utaratibu wa upasuaji unaokusudiwa kuwa wa kudumu. Hata hivyo, mabadiliko ya kimaisha, kupoteza mtoto, au mabadiliko ya mazingira ya kifamilia huwafanya wanawake wengi kujiuliza kama utaratibu huu unaweza kubadilishwa. Makala haya yanachunguza kitaalamu uwezekano wa kurudisha uzazi (Tubal Reversal), viwango vya mafanikio, hatari zake, na mbadala mwingine kama In Vitro Fertilization (IVF

Soma Zaidi...
Fahamu Magonjwa yanayowapata watoto chini ya miaka mitano

Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa mbalimbali ambayo watoto chini ya miaka wanaweza kuyapata kiurahi.

Soma Zaidi...
tatizo la kushindwa kujaza misuli ya mwilini na kusinyaa kwa misuli mwilini

Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kusinyaa kwa Misuli. Ni maradhi yanayopelekea uzalishwaji hafifu wa misuli, hivyo kupelekea misuli kukosa protini, kushunwa kukuwa na kusinyaa.

Soma Zaidi...