Damu, majimaji na uteute unaotoka kwenye uke wa Mjamzito, sababu zake na dalili zake

Unataka kujuwa sababu za mjamzito kutokwa na damu, utelezi ama majimaji kwenye uke wake. Na dalili gani zinaashiriwa na majimaji haya

Damu, majimaji na uteute unaotoka kwenye uke wa Mjamzito, sababu zake na dalili zake



DAMU NA UTEUTE NA MAJIMAJI YANAYOTOKA UKENI WAKATI WA UJAUZITO:




Majimaji yanayotoka ukeni wakati wa ujauzito (Damu na uteute)
Ni kawaida kwa mjamzito kushuhudia kwenye uke wake kutokwa na kama uteute na huongezeka kila mimba inapoendelea kukomaa. Wakatiflani anaweza kuona nguo zake zina madoa ya damu, ama akashuhudia matone kadhaa ya damu. Wapo pia wanaingia hedhi kwa damu chache. Sasa hebu tuangalie kwa ufupi hali hizi:-



1.Baada ya kutoka hedhi uke wa mwanamke unakuwa mkavu bila ya kuwa na utelezi telezi. Hiki ni kipindi ambacho mwanamke hawezi kubeba ujauzito. Katika kipindi hiki hata akitia kidole hakitoki na utelezitelezi. Kipindi hiki kinaweza kuchukuwa takribani siki tano hadi 10 inategemea na mzunguruko wa mwanamke. Huu ni kuda mzuri wa kushiriki tendo kwa wale ambao hawahitaji kulea ujauzito.



2.Zitakapoanza kuingia siku hatari mwanamke ataanza kuhisi uwepo wa uteute kwenye uke wake anapotia kidole kwa ndani. Siku hizi pia zinatofautiana kulingana na idadi ya mzunguruko. Ila zinaweza kuazia siku ya 11 hadi 14 inaweza pia kuwa chini ya papo lwa baadhi ya wanawake ama juu ya hapo.



3.Siku moja kabla ya kukomaa kwa yai na kuwa tayari kwenye mirija ya falopian tayari kutungisha mimba, uteute huu huongezeka zaidi. Sifa za uteute huu ni kuwa ni wenye kuteleza sana ila sio mzito na wenye kunatanata ama kuvutikana. Kwa wanaotumia njia za uzazi wa mpango hasa zile za homoni uteute wao upo muda wowote kwa hiyo ni ngumu sana kwao kuiona hali hii.



4.Siku ya hatario zaidi mwanamke atapata mabadiliko ya hamu ya kutaka kushiriki tendo la ndoa. Yaani hamu itaongezeka zaidi siku hii kuliko siku iliyotangulia. Hapa kwa wale ambao hawataki ujauzito sio siku salama kwao kushiriki tendo landoa.



5.Uteute huu katika siku hizi kuandaliwa kwa ajili ya kusaidia mbegu za kiume ziweze kusafiri vyema, kuogelea vyema na kulifikia yai. Pia kuhakikisha kuwa mbegu za kiume haziathiriwi na asidi ya tumboni kwa mama kwa kiasi kikubwa. Hivyo uteute huu katika kipindi hiki ni muhimu sana.



6.Kali hii inaweza kudumu kwa masiku kadhaa toka 14 hadi 17 kwa makadirio inaweza kupungua ama kuongezeka kulingana na mzunguruko wa mwanamke. Baada ya hapo kama mwanamke alibeba ujauzito majimaji haya yanaongezeka uzito saa na kuwa yenye kunata na kufanana na utelezi wa yai pindi unapolibanja. Baada ya mimba majimaji haya yataendelea kutoka na kuongezeka na kuwa mazito zaidi hadi atakapojifungua.



Katika ujauzito majimaji haya yanakazi ya kulinda njia ya kuingilia kwenye mji wa mimba dhidi ya mashambulizi na aambukizi ya bakteria. Yaani kuhakikisha kuwa hakuba bakteria ama fangasi atakayeweza kuingia na kumzuru mtoto tumboni.



7.Kama hakuna ujauzito uliobebwa majimaji yataanza kurudi kutoka hali yake ya kawaida na kuwa safi, yenye harufu kwa mbali ila si harufu ya kukera, pia yanaweza kuwa na rangi ya maziwa hivi.



Majimaji haya pia nayaweza kuashiria shida kwenye afya endapo yatakuwa na sifa hizi:-
A.Yana rangi ya njao, kijani ama buluu
B.Yana harufu kali mbaya
C.Yanakusababishia muwasho kwenye uke na mashavu ya uke
D.Yanakusababishia kuvimba kwa uke na mashavu ya uke



8.Ama kuhusu kutokwa na damu, ikiwa chache ni kawaida. Ikiwa unaambatana na maumivu makali ya tumbo, ama maumivi makali ya kichwa na homa, basi vyema kumuona daktari kwa ushauri zaidi. Kama nilivtotangulia kusema kuna wanawake wanapata hedhi wakiwa wajawazito. Wenyewe wanaita kupunguzia, kwa ufupi hii si hedhi na pia haiashirii kama kuna tatizo. Ila kama inatoka nyingi na kuambatana na maumivu yasiyo ya kawaida ni vyema kumuona daktari.



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 14782

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Sababu za maumivu wakati wa tendo la ndoa

Kama unapata maumivu wakati wa tendo la ndoa, suluhisho lako lipo kwenye makala hii

Soma Zaidi...
Njia za kupunguza tatizo la kutanuka kwa tezi dume.

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo tunaweza kutumia ili kuweza kupunguza tatizo hili la kutanuka kwa tezi dume, kwa hiyo tunaweza kutumia njia zifuatazo ili kuweza kupunguza tatizo hili kwenye jamii kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kunyonyesha mtoto

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kunyonyesha mtoto, kunyonyesha ni kitendo cha Mama kutumia titi lake Ili kuweza kumpatia mtoto lishe kwa kipindi chote ambacho Mama upaswa kutumia kwa kunyonyesha mtoto wake kwa hiyo Kuna faida ambazo mama uzipata kutoka

Soma Zaidi...
Je dalili ya kuuma tumbo huanza baada ya wiki ngapi Toka mwanamke apate ujauzito?

Maumivu ya tumbo ni moja katika dalili za ujauzito. Maumivu wanawake wengi hushindwa kujuwa kuwa ni ujauzito ama laa. Na hii ni kwa sababu kwa wanawake wengi maumivu ya tumbo ama changu ni jalivya kawaida kwao.

Soma Zaidi...
je mwana mke ana weza kubeba mimba kama hayupo kwenye siku zake za hatali ama

Mimba haipatikani kila siku, na pia mimba huingia kwa siku moja na katika muda mmoja. Baada ya mimba kutungwa hakuna tena nafasi ya kutungwa mimba nyingine.

Soma Zaidi...
Sababu za uke kuwa na harufu mbaya.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa harufu mbaya kwenye uke ukizingatia usafi huwa unafanyika mara kwa mara ila harufu bado inaendelea kuwa mbaya kwa hiyo tutaona sababu hapo chini.

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria

Post hii inahusu zaidi dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria,ni mojawapo ya antibiotics au anti bacteria ambayo upambana na bakteria kama tutakavyoona hapo mbeleni.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa maji yaliyomo kwenye mfuko wa mtoto akiwa tumboni mwa mama

Post hii inahusu zaidi umuhimu wa maji yaliyomo kwenye mfuko wa mtoto akiwa tumboni. Ni maji ambayo kwa kitaalamu huitwa (Amniotic fluid)

Soma Zaidi...
Fahamu matatizo yanayowapata watoto waliozaliwa kabla ya wakati au mapema (premature)

Kuzaa kabla ya wakati ni kuzaliwa ambayo hufanyika zaidi ya wiki tatu kabla ya kuzaliwa kwa mtoto au kuzaliwa mapema ni moja ambayo hutokea kabla ya mwanzo wa wiki ya 37 ya ujauzito. Kawaida, ujauzito hudumu kama wiki 40.

Soma Zaidi...
Kwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?

Je unaweza kunielezaKwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?

Soma Zaidi...