elimu yenye manufaa

Elimu yenye Manufaa



Elimu yenye manufaa ni ile ambayo: Kwanza, humuwezesha mja kufikia lengo la kuumbwa kwake. Tumeona kuwa elimu imekuwa faradhi ya kwanza kwa waumini kwa kuwa elimu ndio nyenzo kuu ya kuwawezesha binaadamu kufikia lengo la kuumbwa kwao ambalo ni kumuabudu Allah (s.w), ipasavyo


katika kila kipengele cha maisha yao. (Qur-an 51:56). Pia elimu ndio nyenzo kuu ya kuwawezesha waumini kuwa viongozi wa jamii (makhalifa wa Allah) katika ardhi. (Qur-an 2:30 - 31).


Elimu itakayotafutwa kinyume na kumuwezesha mtu kumuabudu Mola wake ipasavyo na kusimamisha ukhalifa wa Allah (s.w) katika ardhi itakuwa si elimu yenye manufaa bali elimu yenye kuhasirisha kama tunavyojifunza katika hadithi zifuatazo:



Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w)
amesema: “Anayetafuta elimu isiyokuwa kwa ajili ya
kutafuta radhi za Allah (s.w), hasomi kwa lengo lolote
lile ila la kupata maslahi ya hapa duniani tu. Huyo
siku ya kiyama hatapata hata harufu ya Pepo.”
(Ahmad, Abu Daud, Ibn Majah).



Pia Mtume (s.a.w) ametuasa kuwa mwenye kutafuta elimu ili awazidi wasomi wengine au ili kuitumia katika biashara za kijahili au ili kujionesha kwa watu kuwa naye ni msomi, Mwenyezi Mungu atamuingiza motoni. (Tirmidh).



Pili, elimu yenye manufaa kwa binaadamu hapa ulimwenguni na huko akhera ni ile ambayo pamoja na mtu binafsi kuitumia katika kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo katika maisha yake ya kila siku, huifundisha au huifikisha kwa wengine pia kwa ajili ya kutafuta radhi za Allah (s.w).


Ni vibaya mno mbele ya Allah (s.w) mtu kukataa au kuacha kufikisha kwa wengine kila anachokijua kama tunavyojifunza katika hadithi ifu atayo:
“Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Atakayeulizwa juu ya jambo alilojifunza kisha akaficha (akakataa kutoa elimu ile) atavalishwa mshipi wa moto katika siku ya Kiyama”. (Ahmad, Ibn Majah, Tirmidh na Abu Daud).



Katika hadith nyingine iliyosimuliwa na Abu Hurairah Mtume (s.a.w) amesema:
“Mfano wa elimu isiyonufaisha ni sawa na mfano wa mali iliyokusanywa bila ya kutumiwa katika njia ya Allah ”. (Ahmad, Darini).


Kutokana na hadith hizi tunajifunza kuwa elimu yenye kunufaisha ni ile iliyofundishwa kwa wengine kinadharia na kiutendaji. Kwa kufundisha watu unachokijua bila ya wewe mwenyewe kutenda ni mfano mbaya mno kwa wale wanaofundisha na chukizo kubwa mno mbele ya Allah (s.a.w):


“Enyi mlioamini mbona mnasema msiyoyatenda?) Ni chukizo kubwa mbele ya Allah (s.w) kusema msiyoyatenda.” (61:2-3)
******************************




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 320

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dhana ya ibada kwa mtazamo wa uislamu..

Mtazamo wa uislamu juu ya ibada (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nguzo za imani

Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)

Soma Zaidi...
mitume

Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamh juu ya ibada

Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada

Soma Zaidi...
Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia

Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.

Soma Zaidi...
Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.

Soma Zaidi...