Kwa nini Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kufuatwa

Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.

Kwanini Uislamu Ndio Dini Pekee Inayostahiki Kufuatwa na Watu?

 

 

Hakika dini mbele ya Allah ni Uislamu...” (3:19)

 

“Basi uelekeze uso wako katika Dini iliyo ya haki kabla ya kufika hiyo siku isiyozuilika, inayotoka kwa Mwenyezi Mungu; siku hiyo watatengana (Waumini wende Peponi na Makafiri wende Motoni).” (30:43)
Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa pamoja na kuwepo dini nyingi (mifumo mingi ya maisha) hapa ulimwenguni dini ya Haki anayoiridhia Allah (s.w) ni Uislamu.

 

Hivyo Uislamu ndio dini pekee inayostahiki kufuatwa na watu kwa sababu zifuatazo:


Kwanza, ndio dini ya kweli na ya uhakika kwa sababu imefumwa na Allah (s.w) aliye mjuzi wa kila kitu. Allah (s.w) ndiye aliyemuumba binaadamu kwa lengo maalumu, na hivyo ndiye pekee anayestahiki kumuwekea utaratibu wa maisha utakaomuwezesha kufikia lengo la kuumbwa kwake kwa wepesi.

 

Tunakumbushwa katika Qur-an:

“Litukuze jina la Mola w ako aliye Mtukufu. Aliyeumba (kila kitu na) kukitengeneza na akakikadiria (kila kimoja lengo lake) na akakiongoza (kufikia lengo hilo).” (87:1-3)


Dini nyingine zote wanazofuata watu ni dini za upotofu kwa sababu zinabuniwa na wanaadamu wasio na ujuzi wala uwezo wa kazi hiyo.

 

Mifumo yao ya maisha imefumwa kwa dhana wakiongozwa na matashi ya nafsi zao.

 

Tujihadhari na wazushi hawa wa dini kama Allah (s.w) anavyotuasa:

 

“Na kama ukiwatii wengi katika (hawa) waliomo ulimwenguni watakupoteza na njia ya Mwenyezi Mungu.

 

Hawafuati ila dhana tu, na hawakuwa ila ni wenye kuzua (tu basi).” (6:116).


Pili, Uislamu ndio mfumo wa maisha pekee unaolandana na umbile la binaadamu na maumbile yote yaliyomzunguka.

 

Yaani kanuni na sheria zilizowekwa na Uislamu zinakwenda sambamba na kanuni na sheria zinazofuatwa na maumbile yote, kwani mtunzi wake ni yule yule mmoja, Allah (s.w). Ni kwa msingi huu, Allah (s.w) anatanabahisha watu:

 


“Je, (watu) wanataka dini isiyokuwa ya Mwenyezi Mungu na hali kila kilichomo mbinguni na ardhini kimejisalimisha kwake kipende kisipende?...” (3:83)

 

“Basi uelekeze uso wako katika dini iliyo sawa saw a ndilo umbile Mwenyezi Mungu alilowaumbia watu.Hakuna mabadiliko katika maumbile ya viumbe vya Mw enyezi Mungu.

 

Hiyo ndio dini iliyo ya Haki lakini watu wengi hawajui. ” (30:30).

 


Hivyo kwa kuwa Uislamu ni dini ya maumbile, ndio pekee inayoweza kuiongoza jamii kwa uadilifu na kuleta furaha na amani ya kweli.

 


Tatu, ndio dini pekee inayofuatwa na walimwengu wote wa sehemu zote na wa nyakati zote. Mitume wote wa Mwenyezi Mungu kuanzia Adam (a.s) mpaka kuishia kwa Muhammad (s.a.w), wamefundisha na kufuata dini moja- Uislamu-kama tunavyokumbu shwa katika aya zifuatazo:

 

“Amekupeni sheria ya dini ile ile aliyomuusia Nuhu, na Tuliyokufunulia wewe na Tuliyowausia Ibra him na Mussa na Issa, kwamba simamisheni dini (Uislamu) wala msifarikiane kwayo...” (42:13)

 


“Na ipiganieni dini ya Mwenyezi Mungu kama inavyostahiki (kupiganiw a). Yeye amekuchagueni (muwe umma ulio bora). Wala hakuweka juu yenu mambo mazito katika dini

 

. (Nayo dini hii) ni mila ya baba yenu Ibrahimu; yeye (Mw enyezi Mungu) alikuiteni Waislamu tangu (katika vitabu vya zamani) huko; na ka tika (Qur-an) h ii p ia (mum eitw a jin a h ilo) ili awe Mtume shahidi juu yenu na nyinyi muwe mashahidi juu ya watu (waliotangulia)...” (22:78).

 


Pia Uislamu ni dini isiyoruhusu ubaguzi wa aina yoyote kama tunavyokumbushwa katika aya ifuatayo:

 

“Enyi w atu! Kwa hakika tumekuumbeni (nyote) kw a
(yule) mwanamume (mmoja, Adam) na (yule yule)
mwanamke (mmoja, Hawwa). Na tumekufanyieni
mataifa na makabila (mbali mbali) ili mjuane (tu basi).
Hakika aheshimiw aye sana miongoni mwenu mbele
ya Mwenyezi Mungu ni yule amchaye Mungu zaidi katika nyinyi. Kwa yakini Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye ha bari (za mambo yote).” (49:1 3)

 

Nne, Uislamu ni utaratibu wa maisha uliokamilika.

Uislamu unamuelekeza binaadamu namna ya kuendesha kila kipengele cha maisha yake ya kibinafsi na ya kijamii. Uislamu umeweka utaratibu unaozingatia watu kama walivyo. Kwa kutambua kuwa mtu anakamilika kwa kuwa na mwili na roho, Uislamu umeweka utaratibu wa kuustawisha mwili na roho.

 

Uislamu umetuwekea kanuni na sheria zinazotuwezesha kujenga afya zetu na kukuza utu (ucha Mungu) wetu.

 

Pia, kwa kutambua kuwa watu ni viumbe wanaotakiwa waishi kijamii (social beings) na kutegemeana, Uislamu umetoa mwongozo na kuweka kanuni na sheria ambazo humuwezesha kila mtu binafsi na jamii kwa ujumla kuishi maisha ya furaha na amani.

 

Uislamu umeweka mifumo ya kijamii kama vile siasa, uchumi, utamaduni, na kadhalika juu ya misingi ya haki na Uadilifu.


Tano, ni dini pekee inayomuongoza binaadamu namna ya kumiliki hisia zake.

 

Uislamu unatuelekeza, tufanyeje tunapokuwa katika furaha kubwa.

 

Kwa mfano Uislamu unatuelekeza kuwa tunapokuwa na sherehe, tule na kunywa vilivyo vizuri na halali lakini tusifanye israfu na tumtaje na kumsifu Allah (s.w) kwa wingi.

 

Pia Uislamu unatuelekeza la kufanya pindi tunapofikwa na jambo la kutuhuzunisha sana. Kwa mfano, Uislamu unatuelekeza kuwa tunapofikwa na msiba wa aina yoyote, tusubiri na tuone kuwa,hilo lililotokea ni katika Qadar ya Allah (s.w), kama tunavyokumbu shwa katika aya zifuatazo:

 

“Na Tutakutieni katika msuko suko wa hofu na njaa na upungufu wa mali na wa watu na wa matunda. Na wapashe habari njema wanaosubiri (2 :155)

 


Ambao uwapatapo msiba husema: Hakika Sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye tutarejea”.(2:155-156)

 

“Hautokei msiba katika ardhi wala katika nafsi zenu ila umekwisha andikwa katika Kitabu kabla hatujaumba. Kwa yakini hilo ni sahali kwa Mwenyezi Mungu.

 

Ili msihuzunike sana juu ya kitu kilichokupoteeni, w ala msifurahi sana kwa alichokupeni. Na Mwenyezi Mungu hampendi kila ajivunaye, ajifaharishaye” (57:22-23)
Sita, Uislamu ni dini ya haki kama inavyobainika katika Qu r-an.

 

“Yeye (Allah (s.w) ndiye aliyemleta Mtume wake kwa uongofu na dini ya haki ili aijaalie (dini hii) kushinda dini zote ijapokuwa watachukia washirikina” (9:33)
Dini ya haki hapa ina maana kuu mbili; maana ya kwanza ni kuwa Uislamu ni dini ya Allah (s.w), mjuzi na mwenye Hikima.

 

Allah (s.w) ndiye anayestahiki kuwaundia binaadamu dini kwa kuwa ndiye aliyewaumba kwa lengo maalumu na kwa hiyo ndiye mwenye haki pekee ya kuwawekea wanaadamu utaratibu wa maisha na kuuambatanisha na mwongozo utakaowawezesha kufikia kwa ufanisi lengo hilo.

 


Maana ya pili ni kuwa Uislamu ni dini ya kusimamia haki za binaadamu katika jamii kwa uadilifu kuliko dini yoyote ile. Mitume na Vitabu vya Allah (s.w) vimeshushwa ili kuwafundisha watu uadilifu na kuwaamuru wasimamishe uadilifu kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:

 

“Kwa hakika tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukaviteremsha vitabu na uadilifu pamoja nao, ili watu wasimamie uadilifu. Na tumekiteremsha (tumekiumba) chuma chenye nguvu nyingi na manufaa kwa watu, na ili Mwenyezi Mungu ajulishe anayemnusuru na Mitume yake na hali ya kuwa hawamuoni Mwenyezi Mungu. Kwa yakini Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu mwenye kushinda.” (5 7:25).

 

Katika aya hii tunajifunza kuwa silaha zinatokana na chuma na aina nyingine za madini, nani zana zinazotakaiwa zitumiwe na waumini ili kusimamisha haki na uadilifu katika jamii. Katika aya nyingi za Qur-an waumini wa Kiislamu wameamrishwa kupigana na madhalimu ili kuhakikisha haki inapatikana katika jamii kwa kila raia kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:

 

Basi nawapigane katika njia ya Mwenyezi Mungu wale wanaouza maisha (yao) ya dunia kwa (kununua) ya Akhera. Na anayepigana katika njia ya Mwenyezi Mungu kisha akauawa au akashinda, tutampa ujira mkuu (4:74).

 

Na mna nini hampigani katika njia ya Mwenyezi Mungu na (katika kuwaokoa) wale walio dhaifu - katika wanaume na wanawake na watoto - ambao husema: “Mola wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhalimu, na tujaalie tuwe tuna mlinzi anaetoka kwako. ” (4:75)

 


Wale walioamini wanapigana katika njia ya Mw enyezi Mungu, lakini waliokufuru wanapigana katika njia ya ( Twaghuut). Basi piganeni na marafiki w a Shetani. Hakika hila za Shetani ni dhaifu. (4:76)
Saba, Uislamu ni mfumo wa maisha pekee ulioweka utaratibu wa kumbakisha binaadamu katika maadili ya utu.

 

Uislamu umemuwekea binaadamu ibada maalumu zenye lengo la kumtakasa na kumuwezesha kuwa na maadili mema yatakayopelekea kujenga mazingira ya furaha na amani katika jamii.

 

Ibada hizi maalumu ni Swala, Zakat, Saum, Hija, n.k. Namna ibada hizi zinavyofanya kazi katika kumbakisha binaadamu katika maadili ya utu imefafanuliwa vyema katika kitabu cha pili (Nguzo za Uislamu).

 


Sababu hizi tano za msingi, zatosha kuwa vigezo vya kumfanya mtu achague Uislamu kuwa utaratibu pekee wa maisha wa kufuata katika kuendea kila kipengele cha maisha yake. Dini zote zilizoundwa na watu, zimekosa kabisa sifa hizi na ni zenye kumhasirisha binaadamu katika maisha ya dunia na akhera.

 

Na hata mazingira yetu yanathibisha hili.

 

“Na anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitakubaliwa kwake.Naye akhera atakuwa katika wenye khasara (kubwa kabisa) (3:85).


 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/12/14/Wednesday - 06:19:43 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 649


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-