Nini maana ya ndoa katia uislamu na ni upi umuhimu wake

Hapa utajifunza maana ya ndoa kulingana na uislamu na umuhimu wake katika jamiii

Maana ya Ndoa

Ndoa, kwa ujumla, ni mkataba wa kuishi pamoja kati ya mume na mke kwa kufuata utaratibu uliowekwa na jamii. Kwa mfano, hapa Tanzania mume na mke watatambulika kuwa wameoana kisheria, pale watakapokuwa wamefunga mkataba wa kuishi pamoja mbele ya Mkuu wa wilaya au mbele ya walii na mashahidi wawili (ndoa ya kiislamu)au mbele ya Padri (Kanisani).

 


Ndoa ya Kiislamu ni mkataba wa hiari kati ya mume na mke wa kuishi pamoja kwa kuzingatia masharti na taratibu zilizowekwa na sheria ya Kiislamu. Ndoa yoyote iliyofungwa kinyume na masharti na taratibu za Kiislamu, haikubaliki kwa Waislamu.

 


Umuhimu wa Ndoa kwa Mtazamo wa Uislamu
Katika Uislamu ndoa ni jambo lililokokotezwa sana kama tunavyojifunza katika Hadithi zifuatazo:

 


Katika Hadithi iliyopokelewa na Imamu Bukhari Mtume (s.a.w) amesisitiza kuwa ndoa ni katika sunnah yake na akaongeza kusema: "Yeyote anayekataa sunna yangu sipamoja nami ".

 


Anas (r.a) amesema kuwa Mtume wa Allah amesema, 'Mtu anapooa huwa amekamilisha nusu ya dini, kisha amche Allah ili akamilishe nusu iliyobakia." (Bukhari).

 


Ndoa inasisitizwa kutokana na umuhimu wake katika kuijenga na kuiendeleza jamii kwa:
(i)Kuihifadhi jamii na zinaa.
(ii)Kuendeleza kizazi kwa utaratibu mzuri.
(iii)Kujenga mapenzi na huruma katika familia.
(iv)Kukuza uhusiano na Udugu katika jamii.
(v)Kukilea kizazi katika maadili mema.
(vi)Kuwafanya watu wawajibike ipasavyo.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1084

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Siku zilizoharamishwa kufunga Sunnah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Zoezi la 6 kusimamisha swala

Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala.

Soma Zaidi...
Shart kuu nne za swala

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu masharti ya swala.

Soma Zaidi...
Haki za kiuchumi za mwanamke katika uislamu

Haki za UchumiKuwa imara kiuchumi ni sababu mojawapo kubwa ya kumpa mtu hadhi katika jamii.

Soma Zaidi...
Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu

Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa.

Soma Zaidi...
Kwanini funga imefaradhishwa mwezi wa ramadhani

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...