Kwa nini imefaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani

Unaweza kijiuliza ni kwa nini hasa kimepelekea kufaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani.

Kwa nini Funga imefaradhishwa Mwezi wa Ramadhani

Japo tumefahamishwa katika Qur-an kuwa, faradhi ya funga ni kwa umma zote hatufahamu umma zilizotangulia zilifaradhishiwa kufunga miezi gani au wakati gani wa mwaka. Umma huu umefaradhishiwa kufunga katika mwezi wa Ramadhani kwa sababu ndio mwezi ilipoanza kushuka Qur-an kama tunavyofahamishwa katika aya ifu atayo:

 

“(Mw ezi huo mliofaradhishw a kufunga) ni mw ezi w a Ramadhani ambao ndani yake imeshuka hii Qur-an ili iwe uongozi kwa watu na hoja zilizowazi

 

za uongozi na upambanuzi. Atakayeshuhudia mwezi huu miongoni mwenu na afunge ....” (2:185).
Hivyo, Waislamu wameamrishwa kufunga katika mwezi wa Ramadhani ili pamoja na kutekeleza amri hii wafikie lengo lililoku su diwa, vile vle iwe ni kumbukumbu ya kushuka Qur-an, Mwongozo wa Allah (s.w) wa mwisho kwa wanaadamu. Ni kwa msingi huu kusoma Qur-an kwa wingi katika mwezi huu kumesisitizwa zaidi. Qur-an ilianza kumshukia Mtume (.s.a.w) alipokuwa Jabal-Hira, usiku wa manane katika usiku mmoja wa Mwezi wa Ramadhani. Usiku huo mtakatifu ni “Lailatul’qadri” (Usiku Wenye Cheo) kama tunavyojifunza katika Suratul-Qadr.

 

Hakika Tumeiteremsha (Qur’an) katika usiku w a Laylatul Qadri. Na jambo gani litakalokujulisha ni nini huo usiku wa Laylatul Qadri? Huo usiku wa heshima ni bora kuliko miezi elfu. Huteremka Malaika na roho katika (usiku) huo kwa idhini ya Mola wao kwa kila jambo. Ni amani (usiku) huo mpaka mapambazuko ya alfajiri(97:1-5)

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1622

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Baada ya kumzika maiti nini kifanyike kumsaidia marehemu

Tumesha mzika maiti sasa imebakia mali yae nyumbani, watoto, wake na menginyeo.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake

Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Zijuwe nguzo tano za uislamu na maana zake katika sheria ya uislamu

Hili ni somo letu la kwanza kwenye mtiririko huu wa darsa za fiqh. Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya uislamu na nguzo zake.

Soma Zaidi...
NI ZIPI NGUZO NA SHARTI KUU ZA SWALA ILI IKUBALIWE

Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuelekea qibla katika swala.

Je unadhani ni kwa nini waislamu wanaelekea kibla, na jinsi gani utaweza kukipata kibla.

Soma Zaidi...
Zijuwe funga za kafara na jinsi ya kuzigunga

Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga.

Soma Zaidi...