Jinsi ya kukaa itiqaf na taratibu zake


image


Hapa utajifunza kuhusu taratibu za ibada ya itiqaf yaani kukaa msikitini kwa ajili ya ibada.


Kukaa Itiqaf

Kukaa Itiqaf katika kumi la mwisho la Ramadhani ni sunna iliyokokotezwa. Ki-lugha “Itqaf” ina maana ya kukaa mahali. katika sheria ya Kiislamu “Itiqaf” ni kukaa msikitini kwa ajili tu ya kumkumbuka na kumtukuza Allah (s.w) na kufanya ibada maalum kama vile kuswali, kusoma Qur-an na kufanya amali yoyote njema ambayo inaruhusiwa kufanyika msikitini nje ya shughuli za kawaida za kutafuta rizki. Kwa hiyo mahali pa kukalia “Itiqaf” ni msikitini kama ilivyotajwa katika Qur-an:

 


“... Wala msichanganyike nao, na hali mmekaa Itiqaf misikitini .... ” (2:187).

 


Misikiti inayokaliwa Itiqaf iwe ni ile inayoswaliwa jamaa na Ijumaa ili pasiwe na haja ya kutoka kwa swala za jamaa au kwa swala ya Ijumaa. Wanawake wanaruhusiwa kufanyia Itiqaf zao majumbani mwao katika sehemu zao za kusalia lakini baada ya kupata ruhusa kutoka kwa waume zao. Kwa muda wote mtu atapokuwa katika Itiqaf haruhusiwi kutokatoka msikitini ila kwa dharura kubwa sana kama vile kwenda haja au kwenda kula. Mtu akiwa katika Itiqaf hulazimika kujitenga na shughuli zote za kutafuta maslahi ya maisha na shughuli zote za kijamii kama vile kutembelea wagonjwa, kuhudhuria mazishi, na kadhalika. Mtu anapokuwa katika Itiqaf haruhusiwi kuchanganyika na mkewe.

 

“ ... Na w ala msichanganyike nao na hali mnakaa Itiqaf msikitini. (2:187).
Kwa ujumla katika muda huu wa kukaa Itiqaf, Mu’takif (Mwenye kukaa Itiqaf) anatakiwa ajihusishe tu na ibada maalum kama vile kuswali, kusoma Qur-an, kuleta tasbihi, tahmid, tahalili, takbir, istighfar na maombi mbali mbali.

 


Mu’takif anaruhusiwa kuja na matandiko yake msikitini na kuyaweka mahali pa uficho ambapo hayatawakarahisha watu wakati wa swala ya jamaa. Katika miezi mingine isiyokuwa Ramadhani mtu anaweza kukaa itiqaf kwa muda wowote ule, siku moja au masaa machache. Ni vyema mtu anapokuwa hana shughuli muhimu, anuie kukaa Itiqaf msikitini badala ya kujiingiza kwenye shughuli zisizo muhimu au shughuli za upuuzi zenye kumuingiza katika dhambi na kumpotezea muda ambao ni rasilimali pekee ya maisha yake. Katika mwezi wa Ramadhani Itiqaf imekokotezwa sana katika kumi la mwisho ili kumuwezesha Muumini kuudiriki usiku wa Lailatul-Qadr - akiwa katika hali ya kumkumbuka Allah (s.w). Mtume (s.a.w) alikuwa akikaa Itiqaf katika kumi hili la mwisho kama tunavyojifunza katika hadith zifu atazo:

 


Ames imulia Abdullah bin Umar (r.a) kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa akikaa Itiqaf katika siku kumi za mwisho za mw ezi wa Ram adhani. (Bukhari na Muslim).

 


Aysha (r.a.) amesimulia kuwa Mtume wa Allah alikuwa akikaa Itiqaf katika siku kumi za mwisho za Ramadhani mpaka alipotawafu (Allah alipo mchukua).Kisha wakeze waliendelea kukaa Itiqaf baada yake. (Bukhari na Muslim).



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mambo ambayo hayafunguzi funga
Hii ni orodha ya mambo ambayo hayawezi kuharimu funga yako endapo utayafanya. Soma Zaidi...

image Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu
Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu. Soma Zaidi...

image Mafungu ya urithi katika uislamu
Hspa utajifunza viwango maalumu vya kutithi mirathi ys kiislamu. Soma Zaidi...

image Dhana ya kumiliki raslimali katika uislamu
Ni ipi raslimali ya halali kuimiliki katika uislamu. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuswali swala vitani
Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika ilibkuswalibukiwa vitani. Soma Zaidi...

image Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu
Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha Soma Zaidi...

image Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili
Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake. Soma Zaidi...

image Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali. Soma Zaidi...

image Nini maana ya ndoa katia uislamu na ni upi umuhimu wake
Hapa utajifunza maana ya ndoa kulingana na uislamu na umuhimu wake katika jamiii Soma Zaidi...

image Warithi wasio na mafungu maalumu katika uislamu
Hapa utajifunza watu wanaorithi bila ya kuwekewa mafungu maalumu au viwango maalumi vya kurithi. Soma Zaidi...