Navigation Menu



Mambo gani ni Haramu kwa mwenye janaba?

Hadathi ya kati na kati (Janaba).

Mambo gani ni Haramu kwa mwenye janaba?

Hadathi ya kati na kati (Janaba).



Mtu hupatwa na hadathi ya kati na kati kwa kupatwa na Janaba. Janaba ni hali inayompata mtu baada ya kufanya kitendo cha jimai (kitendo cha ndoa) au kutokwa na manii kwa kuota au kwa namna nyingineyo. Mtu mwenye janaba yuko katika hali chafu kulingana na sharia ya Allah (s.w) na ameharamishiwa kufanya ibada hizi:



(i)Kuswali (rejea Qur-an 4:43, 5:6)
(ii)Kutufu.
(iii)Kukaa Msikitini.



β€œAysha (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Msielekeze milango ya nyumba hizi msikitini kwa sababu si halali msikiti kwa mwanamke mwenye hedhi au kwa mtu mwenye janaba ”. (Abu Daud)


(iv) Ku is oma Qur-an hata kwa moyo.
Ibn Umar ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: β€œWenye hedhi na wenye janaba hawatasoma chochote kutoka kwenye Qur-an ” (Tirmidh)



Si vibaya kwa mtu mwenye janaba kula, kuongea au kugusana na watu. Pia kutokana na mafundisho ya Mtume (s.a.w) si lazima mtu kukoga mara tu baada ya kufanya kitendo cha jimai na mkewe, hasa ikiwa usiku bali anatakiwa aoshe sehemu za siri na atawadhe alale, kisha akiamka ndipo akoge kwa kujitwaharisha kwa ajili ya swala ya Alfajiri. Mafundisho haya tunayapata katika hadithi ifuatayo:



Aysha (r.a) ameeleza kuwa: Mtume (s.a.w) alipotaka kula au kulala akiwa na janaba, alikuwa kwanza akitawadha kama anavyotawadha kwa ajili ya swala. (Bukhari na Muslim).




                   


Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1277


Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

Dhana ya haki na uadilifu katika uislamu
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ni nini maana ya swala
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala. Soma Zaidi...

Nafasi ya serikali katika ugawaji
Serikali ina nafasi katika kufanya mgawanyiko katika uchumi. Soma Zaidi...

Haki na wajibu wa mke kwa mumewe na familia
Soma Zaidi...

Maandalizi ya maiti: kumuosha, kumkafini ama kumvalisha sanda na kumzika
Soma Zaidi...

Usimamizi wa Haki na haki za binadamu Katika Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...

Tathmini ya swala zetu, kwa nini swala zetu hazijibiwi?
Soma Zaidi...

Nini maana ya Kushahadia nguzo ya kwanza ya uislamu
Soma Zaidi...

Nguzo za uislamu
Katika kipengele hiki tutajifunza nguzo za uislamu.aina tano za nguzo za uislamu,dhana ya nguzo za uislamu,lengo na umuhimu wa nguzo za uislamu Soma Zaidi...

namna ya kuswali
11. Soma Zaidi...