ijuwe maawe maan ya kusimamisha swala

ijuwe maawe maan ya kusimamisha swala

Maana ya Kusimamisha Swala



Kusimamisha swala ni tofauti na kuswali. Kuswali ni kufanya vitendo vya swala kama vile kusimama, kurukuu, kuitidali, kusujudu, n.k. Kusimamisha swala ni kuitekeleza swala kwa kuchunga na kutekeleza kwa ukamilifu yafuatayo:



(i)Sharti zote za swala.
(ii)Nguzo zote za swala.
(iii)Kuwa na khushui (unyenyekevu) wakati wote wa kutekeleza sharti na nguzo za swala.



Mtu akiswali bila ya kuzingatia na kutekeleza kwa ukamilifu mambo haya matatu, ataonekana kuwa kaswali, lakini atakuwa hajasimamisha swala na atastahiki kuadhibiwa vikali na Mola wake kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:



'Basi adhabu kali itawathibitikia wanaoswali, ambao wanapuuza swala zao (kwa kutozisimamisha), ambao hufanya ria '. (107:4-6)
Kupuuza swala ni pamoja na kutotekeleza ipasavyo sharti za swala, nguzo za swala, na kutokuwa na unyenyekevu wakati wa kutekeleza sharti na nguzo za swala.
Hivyo, swala inayokubalika mbele ya Allah (s.w) ni ile iliyosimamishwa kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:


'Hakika wamefuzu w aumini ambao katika swala zao ni wanyenyekevu '. (23:1-2)
'Na ambao swala zao w anazihifadhi' . (23:9)
Kuhifadhi swala ni kutekeleza kwa ukamilifu sharti na nguzo zote za swala.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 152

Post zifazofanana:-

Je! vitu vichachu kama,machungwa twarusiwa kula wagonjwa wa vidonda vya tumbo?
Nashukuru kwa ushauri, Je! Soma Zaidi...

RAJABU ATHUMAN MAHEDE,(MAARUFU KAMA MWALIMU RAJABU ATHUMANI MAHEDE, AU OSTADHI RAJABU ATHUMANI MAHEDE)
Soma Zaidi...

Quran si maneno ya shetani
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII LUTI
Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat As-Sajida
Nao husema (kwa maskhara): "Je, tutakapopotea katika ardhi, (tukageuka mchanga) ndio tutarudishwa katika umbo jipya? Soma Zaidi...

DAWA MBADALA ZA VIDONDA VYA TUMBO
DAWA MBADALA ZA VIDONDA VYA TUMBO Dawa za kukabiliana na zaidi ambazo zina calcium carbonate (Tums, Rolaids), zinaweza kusaidia kutibu vidonda vya tumbo lakini hazipaswi kutumiwa kama matibabu ya msingi. Soma Zaidi...

Vyanzo vitano vya elimu zote duniani: Chanzo cha Elimu ni Allah (s.w)
Kama tunavyojifunza katika surat 'Alaq (96:4-5), chanzo cha elimu au mkufunzi wa binadamu ni Allah (s. Soma Zaidi...

Haki na wajibu wa mke kwa mumewe na familia
Soma Zaidi...

Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil
Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s. Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA KITABU CHA PILI
Soma Zaidi...

MAAJABU YA MBU
7. Soma Zaidi...

ENGLISH FOR PRIMARY SCHOOL, STANDARD FOUR
Soma Zaidi...