hizi ndio nguzo za swala, swala za faradhi na suna

hizi ndio nguzo za swala, swala za faradhi na suna

Nguzo za Swala



Utekelezaji wa nguzo za swala ni hatua ya pili katika harakati za kusimamisha Swala. Baada ya kutekeleza kwa ukamilifu sharti za swala, Muislamu huwa tayari kumkabili Mola wake na kuzungumza naye katika swala.Vipi tuzungumze na Mola wetu katika swala, tumeonyeshwa kinadharia na matendo na Mtume Muhammad (s.a.w) ambaye ametuusia: 'Swalini kama mlivyoniona mimi nikiswali'. Tunafahamu Mtume (s.a.w) aliswali vipi kwa kurejea Hadith zifuatazo:



Aysha (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) alikuwa akianza swala kwa takbira na kusoma Qur-an - Alhamdullilaahi Rabil-alamiina (Suratul Fatiha). Alipoinama (kurukuu) hakuwa anaweka kichwa chake juu wala hakuwa anakiinamisha sana bali alikuwa akikiweka katikati ya hali hizo mbili, na alipoinuka kutoka kwenye rukuu hakuwa anakwenda


kwenye sijda mpaka asimame kwanza wima na alipoinua kichwa chake kutoka kwenye sijda, hakusujudu mpaka baada ya kukaa wima; na alikuwa akisoma tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili, na (katika hiyo tahiyyatu) alikuwa anakaa kwa kuulaza mguu wa kushoto na kuusimamisha wima mguu wa kulia. Alikataza kukaa mkao wa shetani (kunyoosha miguu) na kunyoosha mikono kama mnyama, na alikuwa akifunga (akimaliza) Swala kwa Salaam'. (Muslim)



Abu Humid Sayid(r.a) aliwaambia Masw ahaba wa Mtume (s.a.w) alitaka kuwakumbusha jinsi Mtume wa Mwenyezi alivyokuwa akisw ali. Alisema (Abu Humaid) kwamba wakati alipokuwa akisoma takbira Mtume alikuwa akiweka mikono yake mkabala na mabega yake na alipokuw a akirukuu, aliweka viganja vya mikono yake juu ya magoti na kuupinda mgongo wake; wakati alipoinua kichwa (alipoinuka) alijinyoosha (alinyoosha shingo yake) wima mpaka kila kiungo kinarudia nafasi yake; wakati alipokwenda Sijda (aliposujudu) mikono yake ilikuwa kati na kati (haikuwa mbali sana wala haikuwa pamoja), na vidole vyake (ncha za vidole vyake) vya miguu vilielekea (alivielekeza) Ka 'aba, alipokaa baada ya rakaa mbili alikuwa akiukalia mguu wake wa kushoto na kusimamisha mguu wa kulia. Wakati alipokaa katika rakaa ya mwisho aliutanguliza (hakuukalia) mguu w a kushoto na kuusimamisha w a kulia, alikaa kwa makalio. (Bukhari).



Abu Hamaid Sayid aliwaambia Maswahaba kumi wa Mtume(s.a.w), kwamba yeye anajua vizuri zaidi jinsi Mtume (s.a.w) alivyokuwa akiswali. Alisema (Abu Hamid) kwamba: Wakati Mtume (s.a.w) aliposimama kuswali, aliinua mikono yake juu mpaka ilipokuwa mkabala na mabega yake. Halafu alisoma takbira na baadaye alisoma Qur-an. Halafu alisoma takbira na kuinua tena mikono yake hadi kufikia mkabala na mabega yake.Halafu aliinama (alirukuu) akiweka viganja vya mikono yake juu ya magoti na kujiweka mwenyewe sawa sawa (bila ya kuinamisha kichwa wala kukiinua juu). Baadaye aliinua kichwa chake (aliinuka kutoka rukuu) na kusema: 'Mwenyezi Mungu anamsikia (humsikia) yule anayemsifu '. Halafu aliinua tena mikono yake hadi kufikia mkabala na mabega yake akiwa wima sawa sawa na kusema:'Mwenyezi Mungu ni mkubwa '. Baadaye alikw enda (chini alikw enda sijda) akiw eka mikono yake mbali na usawa wake na mwili na kupinda vidole vyake vya miguu. Aliinua kichwa chake na aliukunja mguu wake wa kushoto na kuukalia. Alikaa sawasawa (wima) mpaka kila kiungo cha mwili kimerudia mahali pake, na alikwenda tena sijda na kusema:'Mwenyezi Mungu ni mkubwa '. Aliinuka (alijiinua) kutoka Sijda na kukalia mguu wake wa kushoto. Alikaa sawa sawa mpaka kila kiungo cha mwili kikarudia nafasi yake (mahali pake). Baadaye alisimama juu (wima) na kufanya yote kama alivyofanya


katika rakaa ya kwanza. Mw is ho wa rakaa hizi mbili alisimama na kusoma takbira.ya kwanza na aliinua mikono yake hadi ikawa mkabala na mabega yake kama alivyosoma takbira ya kufungulia swala na baadaye alifanya hivyo hivyo katika sehemu ya swala iliyobakia mpaka kufikia Sijda ambamo mlikuwa na (Taslimu). Aliondoa mguu wake wa kushoto (hakuukalia). Alikaa kwa makalio zaidi upande wa kushoto (alikalia mfupa wa kalio la upande wa kushoto) baadaye alitoa Salaam (Taslim). Maswahaba wote `walikubali kuwa Abu Hamid amesema ukweli. (Abu Daud).



Hadithi hizi zinatufahamisha kuwa swala ya Mtume(s.a.w) ambaye ametuamrisha tumuigize ina vipengele vilivyogawanyika katika mafungu makubwa mawili. Nguzo za Swala na Sunnah za Swala.



Nguzo za Swala



Nguzo za swala ni vile vipengele vya swala ambavyo lazima mtu avitekeleze ndio swala yake iweze kukamilika. Nguzo moja tu ikikosekana swala haisihi (haikamiliki). Hivyo ili mwenye kuswali awe na matarajio ya kupata matunda ya Swala hana budi kutekeleza nguzo zake zote kwa ukamilifu. Zifuatazo ni nguzo za Swala:



1. Nia - dhamira moyoni.
2. Takbira ya kuhirimia (au Takbira ya kufungulia Swala).
3. Kusoma suratul-Fatiha.
4.Kurukuu.
5.Kujituliza katika rukuu.
6.Kuitidali (kusimama kutoka katika rukuu).
7.Kujituliza katika itidali.
8.Kusujudu.
9.Kujituliza katika sijda.
10.Kukaa kati ya sijda mbili.
11.Kujituliza katika kikao cha kati ya sijda mbili.
12Kusujudu mara ya pili.
13.Kujituliza katika sijda ya pili.
14.Kukaa Tahiyyatu.
15.Kusoma Tahiyyatu.
16.Kumswalia na kumtakia rehema Mtume (s.a.w) na Waislamu.
17.Kutoa Salaam.
18.Kuswali kwa kufuata utaratibu huu (1 - 17).



hizi za swala tunaweza kuzigawanya kwenye makundi
(a)Nia.
(b)Nguzo za matamshi (visomo)
(c)Nguzo za vitendo.
(d)Kufuata utaratibu.



Katika nguzo 18, nguzo za matamshi ni hizi tano zifuatazo:
(i)Takbira ya kuhirimia swala.
(ii)Ku soma suratul-Fatiha (Al-hamdu).
(iii)Kusoma Tahiyyatu.
(iv)Kumswalia Mtume.
(v)Kutoa Salaam.



Nguzo zote zilizobakia, ukiacha nia na kufuata utaratibu ni nguzo za vitendo.




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 356


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

SHUGHULI ZA KILA SIKU
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

DUA ZA WAKATI WA HASIRA
DUA ZA WAKATI UNAPOKUWA NA HASIRA. Soma Zaidi...

quran na sayansi
Soma Zaidi...

Historia ya Kuzuka Imani ya Kishia waliodai kuwa ni wafuasi wa Ally
Soma Zaidi...

Njia za kudhibiti riba
Ufumbuzi wa tatizo la ribaRiba imeenea na kuzoeleka duniani kwa kiasi ambacho watu wengi wanadhani kuwa bila riba hakuna shughuli yoyote ya uchumi inayowezekana. Soma Zaidi...

Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)
Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an. Soma Zaidi...

kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii
11. Soma Zaidi...

Sifa na majina ya siku ya mwisho siku ya kiyama
Soma Zaidi...

KUMUAMINI MWENYEZI MUNGU
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...

Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Soma Zaidi...

Namna ya kujitwaharisha Najisi ndogo
Soma Zaidi...

KUINGIA KWA WAGENI
Download kitabu Hiki Bofya hapa KUINGIA KWA WAGENI Amina na Sadie walimuonea huruma wakamuomba Zubeid amruhusu abakie. Soma Zaidi...