9. Swala ya Kukidhi Haja



Muislamu anatakiwa amtegemee Allah (s.w) katika kila hali. Kila anapokuwa na tatizo au anapohitajia jambo lolote, anatakiwa amuelekee Allah (s.w) na aombe msaada kutoka kwake.



Abdur-Raham ibn Awfi (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Yeyote atakayekuwa na haja ambayo anataka itoshelezwe na Allah (s.w) au na mwanaadamu na atawadhe inavyostahiki, kisha aswali (rakaa mbili) amhimidi Allah na kumtakia Mtume Rehma na amani kisha aseme:
“Hapana Mola (apasaye kuabudiwa) ila Mwenyezi Mungu. Mwingi wa huruma, Mkarimu. Utukufu ni wa Allah, Mfalme wa Arshi Tukufu, Shukurani zote ni za Mwenyezi Mungu Mola (Bwana) wa walimwengu.


Nakuomba unr'laalie njia ya kupata rehtna Zako na sababu ya kupata msanwha wako: Ninaomba hifadhi Yako kutokuna na kila oru. Usiniache na kosa (dhanrbi) lnlote bila vu kunisatnehe na (usiniache na) na wasi wasi wowote bila ra kuniondolea, na usiniache na haft' vovore venue radhi Zako bila ya kunikidhia. Ewe Mwingi wa Rehnui Mrehentevu ". (Tirmidh, Ibn Majah).