image

Muda wa kuhiji na mwenendo wa mwenye kuhiji

Muda wa kuhiji na mwenendo wa mwenye kuhiji

Muda wa Hijja



Ibada ya Hija hufanywa katika muda maalum wa mwaka kama inavyosisitizwa katika Qur-an:


“Hija ni miezi maalum...” (2:197).



Miezi iliyowekwa kwa ajili ya Muislamu kunuia kuizuru Ka’ba kwa ajili ya Hija ni mwezi wa Shawwal, mwezi wa Dhul-Qaadah (mfungo pili) na siku kumi za mwanzo za mwezi wa Dhul-Hijah. Wakati wowote katika miezi hii mtu anaweza kwenda Makka kwa ajili ya Hija, lakini hataweza kufanya matendo ya Hija mpaka uanzie mwezi wa Dhul-Hija. Siku za Hija ni kuanzia tarehe 8 Dhul-Hija mpaka tarehe 13 Dhul-Hija.



Mwenendo wa mwenye kunuia Hija au ‘Umra


Mwenye kunuia kuhiji katika miezi hiyo iliyotajwa, analazimika ajipambe na tabia nzuri.Ajizuilie na maneno na matendo machafu na maovu. Ajitahidi kuishi na watu kwa wema, awatake radhi kwa yale yote mabaya aliyowatendea na azidishe kuwatendea wema.Allah (s.w) anatuagiza:


... Na anayekusudia kufanya Hija katika miezi hiyo, basi asiseme maneno machafu wala asifanye vitendo vichafu wala asibishane katika hiyo Hija.


Na kheri yoyote mnayoifanya Mwenyezi Mungu huijua ....” (2:197).
Mwenye kuhiji au kufanya ‘Umra anatakiwa ajipambe na tabia hiyo njema kwa kipindi chote atakapokuwa safarini. Yafuatayo ni mambo muhimu anayotakiwa ayazingatie mtu anapokuwa katika safari ya Hija au Umra.



(i)Ajiepushe na maneno maovu na machafu, pia ajiepushe na vitendo viovu na vichafu.



(ii)Azidishe kusoma Qur’an na Kuswali swala za faradhi kwa jamaa, kuswali swala za sunnah, kuomba msamaha na kutubu kikweli kweli kwa Mola wake.



(iii)Ajitahidi kuwa mwema na mpole kwa wasafiri wenzake, kuongea nao vizuri, kuwapa msaada wanaohitajia, kuwasamehe kwa kosa lolote watakalomfanyia, kujizuia na hasira na kuvumilia maudhi mengi yanayotokana na wasafiri wenzake au wenyeji wa sehemu za Hija.



(iv)Ajitahidi kuchanganyika na wasafiri wenzake kutoka sehemu mbalimbali, ajitahidi kujihusisha kwenye mikutano na mazungumzo ya kheri na kujaribu kubadilishana mawazo na wenzake kutoka sehemu mbalimbali ambao wanaelewana lugha, juu ya usimamishaji Uislamu ulimwenguni.



(v)Ajitahidi kuinamisha macho yake katika makundi yenye mchanganyiko wa wanawake na wanaume na kila itakapowezekana ajiepu she kuwa katika mchanganyiko wa wanaume na wanawake.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 318


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-