image

Taratibu za kumuona mchumba

Taratibu za kumuona mchumba

Ruhusa ya Wachumba Kuonana Kabla ya Ndoa



Pamoja na sifa ya ucha-Mungu na wema, tunatakiwa tuwaoe wanawake tunaowapenda kwa sura na umbo; hivyo hivyo wanawake nao wachague wanaume wanaowapenda kwa sura na umbo ili kuzidisha mapenzi na upendo baina yao katika familia. Kwa mantiki hii Mtume (s.a.w) ameruhusu wachumba kuonana kabla ya kufunga ndoa kama tunavyojifunza katika hadithi zifuatazo:



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa mwanamume mmoja alikuja kwa Mtume (s.a.w) akasema: "Ninakusudia kumuoa mwanamke miongoni mwa answari." Akasema Mtume


(s.a.w), 'Mwangalie kwanza kwa sababu kuna dosari katika macho ya Answari." (Muslim)



Jabir (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w) amesema: "Mmoja wenu atakapochumbia, na akawa na uwezo wa kumtazama yule anayemchumbia na afanye hivyo." (Bukhari na Muslim)



Pamoja na ruhusa hii, bado waislamu wanalazimika kuendelea kuzingatia mipaka ya "Hijaab", kwamba hawaruhusiwi kukaa faragha au kutembea faragha mwanamke na mwanamume wasio maharimu.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 274


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-