Navigation Menu



ihram na nia ya Hija na Umra

1.

ihram na nia ya Hija na Umra

1.Ihram na Nia ya Hija au ‘Umra
Matendo ya Hija au ‘Umra huanza rasmi kwa kuvalia vazi la Ihram. Kama tulivyoona Ihram huvaliwa nyumbani au katika vituo maalum -


Mawaaqiit - vilivyowekwa na Mtume (s.a.w) kabla ya kuingia kwenye uwanja Mtakatifu wa Makka. Wakazi wa Makka huvalia Ihram nyumbani kwa o.
Utaratibu unaofuatwa ni kwamba Hajj, kabla ya kuvaa Ihram, ni sunna kunyoa nywele za makwapani na sehemu nyingine za mwili, kupunguza nywele za kichwani, kunyoa ndevu na kukata kucha. Kisha ni sunnah kukoga, kutawadha na kupaka manukato ndipo uvalie Ihram. Ni vyema kuvaa Ihram wakati wa swala mojawapo ya faradhi. Mtume (s.a.w) katika Hija ya kuaga alivaa Ihram wakati wa swala ya Adhuhuri.



Kabla ya kutia nia ya aina ya Hija au ‘Umra, Haji ataswali rakaa mbili za sunnah, kisha mara tu baada ya kutoa salaam atanuia aina ya Hija anayokusudia kuifanya, na ataitikia wito wa Allah (s.w) kulingana na nia yake.Kama nia yake ni ya kufanya ’Umra (At-Tamattu) ataitika:



Ee Allah nakutikia kwa ‘Umra.
Allahumma labbaikal ’Umrata



Kama nia yake ni ya kufanya Hija na ‘Umra (Al-Qiran) ataitika:


Ee Mola. Naitika kwa Hija na ‘Umra. Allahumma labbaikal hajji wa Umrata


Kama nia yake ni ya kufanya Hija tu (Al-Ifraad) ataitikia: Ee Mola, Naitika kwa Hija Allahumma labbaikal hajji




                   


           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 303


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Namna ya kutufu, na masharti ya mwenye kutufu
3. Soma Zaidi...

Muda wa kuhiji na mwenendo wa mwenye kuhiji
Soma Zaidi...

maana ya swala kilugha na kisheria
Soma Zaidi...

TAFSIRI (TARJIMA) YA QURAN KWA LUGHA YA KISWAHILI
Tafsiri ya Quran kwa iswahili iliyotafsiriwa na Sheikh Ali Muhsin Al-BArwani Soma Zaidi...

Kiwango cha mahari katika uislamu
Kiasi gani Kinachojuzu kutolewa Mahari? Soma Zaidi...

Hutuba ya ndoa wakati wa kuoa
Soma Zaidi...

MAFUNZO YA QURAN: QURAN NA SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Soma Zaidi...

Swala za tahajud na namna ya kuziswali
4. Soma Zaidi...

Sababu Ya Uislamu Kuwa Ndiyo Dini Sahihi Pekee
1. Soma Zaidi...

Zijuwe suna (sunnah) za Udhu ama Kutawadha
Soma Zaidi...