28.
28. Kudhibiti Hasira
Kujizuia na hasira ni tabia njema inayoambatana na tabia ya kusamehe. Hasira humpata mtu anapoudhiwa. Wakati mwingine huja ghafla na kumnyima mtu wakati wa kufikiri. Hasira zinaongozwa na shetani, hivyo humnyima mtu nafasi ya kutumia akili, hekima na busara. Hivyo humpelekea mtu kufanya matendo ambayo hugeuka kuwa majuto baadaye. Hasira hasara. Kujizuilia na hasira ni kitendo cha ucha Mungu chenye malipo makubwa mbele ya Allah (s.w). Rejea Qur-an (3:133-134) na (42:36-37). Pia ubora wa kujizuilia na hasira unadhihirika katika Hadithi zifuatazo:
Abu Hurairah(r.a) am esim ulia kuw a m tu mm oja alim uom ba Mtum e (s.a.w): โNiwaidhiโ. Mtume akasema: โUsighadhibikeโ. Kisha akarudia mara nyingi akisema: Usighadhibike. (Bukhari)
Abu Hurairah(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema โMtu mwenye nguvu si bingwa wa mieleka bali mtu mwenye nguvu ni yule anayejizuilia na has ira โ. (Bukhari na Muslim).
Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: โHapana mja aliyemeza kidonge kichungu mbele ya Allah (s.w) kuliko kidonge cha hasira alichokimeza, huku akitaraji radhi ya Allah (s.w)โ. (Ahmad).
Mbinu za kujizuia na hasira zimebainishwa katika Qur-an kama ifu atavyo:
โShikamana na kusamehe na amrisha mema na wapuuze majahili (wajinga). Na kama wasi wasi wa shetani ukikusumbua basi (sema: Audhubillah) jikinge kwa Mwenyezi Mungu. Bila shaka yeye ndiye asikiaye na ajuaye.โ (7:199-200).
Kutokana na aya hizi
hasira ni hizi zifuatazo:
(i) Kushikamana
(ii) Kushikamana
(iii) Kuwapuuza m
(iv) Kujikinga kwa tunajifunza kuwa mbinu za kujizuilia na
na kusamehe.
na kuamrisha mema.
ajah ili.
Allah (s.w) na uovu wa shetani.
Pia Mtume (s.a.w) anatupa mbinu nyingine za kupambana na hasira katika Hadithi zifuatazo:
Atiyyah bin Urw ah Ba โid(r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah amesema: โHakika hasira zinatoka kwa Shetani, na Shetani ameumbwa kutokana na moto na hakika moto huzimishwa na maji. Kwa hiyo yoyote miongoni mwenu atakayepandwa na hasira, na atawadheโ. (Abu Daud).
Abu Dharr (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: โWakati wowote mmoja wenu atakapopandwa na hasira akiwa amesimama, na akae chini. Kama (kwa kufanya hivyo) hasira itamtoka ni vyema; lakini kama haitatoka, na alale chiniโ. (Ahmad, Tirmidh).
Kutokana na Hadithi hizi Mtume (s.a.w) anatuelekeza tupunguze hasira zetu kwa:
(i)Kutia udhu.
(ii)Kukaa chini iwapo tumesimama.
(iii)Kulala chini.
Umeionaje Makala hii.. ?
Wajibu wa Wazazi kwa Watoto Wazazi wanawajibu kwa watoto wao.
Soma Zaidi...ุนููู ุงุจููู ุนูู ูุฑู ุฑูุถููู ุงูููููู ุนูููููู ูุงุ ุฃูููู ุฑูุณูููู ุงูููููู ุตูู ุงููู ุนููู ู ุณูู ููุงูู: "ุฃูู ูุฑูุชู ุฃููู ุฃูููุงุชููู ุงููููุงุณู ุญูุชููู ?...
Soma Zaidi...Hapa utajifunza nafasi ya kufuata suna katika Uislamu
Soma Zaidi...ุนููู ุฃูุจูู ุฑููููููุฉู ุชูู ููู ู ุจููู ุฃูููุณู ุงูุฏููุงุฑูููู ุฑูุถููู ุงูููู ุนููููู ุฃูููู ุงููููุจูููู ุตูู ุงููู ุนููู ูุณูู ููุงูู: "ุงูุฏููููู ุงููููุตู?...
Soma Zaidi...