DUA ZA KUONDOA WASIWASI

DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah.

DUA ZA KUONDOA WASIWASI


DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI
Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah. Hakuna haja ya kumeza dawa za kupunguza maumivu kwa mwenye kumuamini Allah. Ila watu wasielewe vibaya maneno haya, maaana Mtume (s.a.w) amesisitiza watu wajitibu, ila pia ieleweke Allah amejaalia kuwa qurani ni dawa na ni ponyo kwa maradhi na mabo mengine. Leo hapa nimewaandalia dawa ya kuondowa maumivu katika sunnah nayo ni dua ambayo mtume (s.a.w) alikuwa akiwafundisha masahaba waombe pindi wakiwa na maumivu na maradhi.

1.Mtume (s.a.w) alimwambia swahaba kuwa: “weka mkono wako pale unaposikia maumivu katika mwili wako kisha sema “BISMILLAHI” mara tatu kisha useme mara saba (maneno haya): “A’UDHU BILLAHI WAQUDRATIHI MIN-SHARI MAA AJIDU WA-UHAADHIRU”. Hadithi hii ni sahihi na amepokea Muslim, Abu Daud na Ibn Maajah kutokana na masimulizi ya ‘Uthman Ibn Abil-”As.

2.Mtume (s.a.w) alimwambia Mainuna bint Abi Ubay kuwa :”weka mkono wako wa kulia pale panapokupatia maudhi (maumivu) kisha sema “BISMILLAHI ALLAHUMMA DAAWINI BIDAWAAIKA WASHFINII BISHAAIKA WAGHANII BIFADHLIKA ‘AN-MAN SIWAAKA WAHDHUR ‘ANII ADHAAKA” (Amepokea Tabrany)

3.Mume (s.a.w) alimwambia Asmaa bint AbuBakar kuwa: “weka mkono wako (pende maumivu) na useme mara tatu “BISMILLAHI ALLAHUMMA ADH-HAB ‘ANNI SHARRA MAA AJIDU BIDA’AWATIKA NABIYYIKA TWAYYIBIL-MUBAARAKIL-MAKIIN ‘INDAKA. BISMILLAHI “ (Amepokea ibn “Asakir)

4.amesimulia Ibn ‘Abas (r.a) kuwa : “alikuwa Mtume (s.a.w) akitufundisha dua kwa ajili ya maradhi na maumivu yote tunayoyapata kuwa Mtu aseme: ‘BISMILLAHI, A’UDHUBILLAHIL-’ADHIIM MINSHARRI KULLI ‘ARQIN-NA’AARI, WAMINSHARRI HARRIN-NAHAARI” (Amepokea Ahmad, tirmidh na Alhaakim).


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 2935

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 web hosting    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

DUA 85 - 93

SWALA YA MTUME 85.

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...
NYAKATI AMBAZO DUA HUJIBIWA

NYAKATI AMBAZO DUA HUJUBIWA.

Soma Zaidi...
Dua za kuondoa wasiwasi, woga na kujikinga na uchawi, na mashetani

Post hii itakufundisha dua za kuomba wakati wa woga, wasiwasi na kujikinga na wachawi na mashetani

Soma Zaidi...
MAANA NA FADHILA ZA DUA

DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.

Soma Zaidi...
Maana ya Hadith al Quds na Hadith an-Nabawiy

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya hadithi al Quds na Hadith an-Nabawiy

Soma Zaidi...