DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah.
![]()
![]()
DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI
Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah. Hakuna haja ya kumeza dawa za kupunguza maumivu kwa mwenye kumuamini Allah. Ila watu wasielewe vibaya maneno haya, maaana Mtume (s.a.w) amesisitiza watu wajitibu, ila pia ieleweke Allah amejaalia kuwa qurani ni dawa na ni ponyo kwa maradhi na mabo mengine. Leo hapa nimewaandalia dawa ya kuondowa maumivu katika sunnah nayo ni dua ambayo mtume (s.a.w) alikuwa akiwafundisha masahaba waombe pindi wakiwa na maumivu na maradhi.
1.Mtume (s.a.w) alimwambia swahaba kuwa: âweka mkono wako pale unaposikia maumivu katika mwili wako kisha sema âBISMILLAHIâ mara tatu kisha useme mara saba (maneno haya): âAâUDHU BILLAHI WAQUDRATIHI MIN-SHARI MAA AJIDU WA-UHAADHIRUâ. Hadithi hii ni sahihi na amepokea Muslim, Abu Daud na Ibn Maajah kutokana na masimulizi ya âUthman Ibn Abil-âAs.
2.Mtume (s.a.w) alimwambia Mainuna bint Abi Ubay kuwa :âweka mkono wako wa kulia pale panapokupatia maudhi (maumivu) kisha sema âBISMILLAHI ALLAHUMMA DAAWINI BIDAWAAIKA WASHFINII BISHAAIKA WAGHANII BIFADHLIKA âAN-MAN SIWAAKA WAHDHUR âANII ADHAAKAâ (Amepokea Tabrany)
3.Mume (s.a.w) alimwambia Asmaa bint AbuBakar kuwa: âweka mkono wako (pende maumivu) na useme mara tatu âBISMILLAHI ALLAHUMMA ADH-HAB âANNI SHARRA MAA AJIDU BIDAâAWATIKA NABIYYIKA TWAYYIBIL-MUBAARAKIL-MAKIIN âINDAKA. BISMILLAHI â (Amepokea ibn âAsakir)
4.amesimulia Ibn âAbas (r.a) kuwa : âalikuwa Mtume (s.a.w) akitufundisha dua kwa ajili ya maradhi na maumivu yote tunayoyapata kuwa Mtu aseme: âBISMILLAHI, AâUDHUBILLAHIL-âADHIIM MINSHARRI KULLI âARQIN-NAâAARI, WAMINSHARRI HARRIN-NAHAARIâ (Amepokea Ahmad, tirmidh na Alhaakim).
Umeionaje Makala hii.. ?
DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.
Soma Zaidi...Posti hii inakwenda kukupa orodha ya dua 10 ambazo unaweza kuziomba kila siku.
Soma Zaidi...Historia ya uandishi wa hadithibwakati wa Matabiina, yaani wafuasi wa maswahaba
Soma Zaidi...Hapa nitakuletea baadhi tu ya adhkari ambazo ni muhimu kwa muislamu
Soma Zaidi..."Si vibaya kwa kipofu, wala si vibaya kwa kiguru, wala si vibaya kwa mgonjwa, wala kwenu, kama mkila katika nyumba zenu, au nyumba za baba zenu, au nyumba za mama zenu, au nyumba za ndugu zenu, au nyumba za dada zenu, au nyumba za ami zenu, au nyumba za s
Soma Zaidi...Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukugundisha adabu zinazotakikana kwa mwenye kuomba dua.
Soma Zaidi...