DUA 32 - 40

32.

DUA 32 - 40


32.Dua ya Kulipa Deni "Allahummak-finiy bihalaalika'an haraamika wa-agh-niy bifadhw-lika 'amman siwaaka." Ee Allah! Nitosheleze na halali yako na Uniepushe na haramu yako, na Unitosheleze kwa fadhila zako nisiwahitaji wengine asiye wewe.

33.Dua anayoleta yule aliyefikwa na jambo gumu “Allahumma laasah-la illaa maaja-'al-tahu sah-laa, wa anta taj-'alul-haz-na idhaashi-ita sah-laa. Ee Allah hakuna jepesi ila ulilolifanya jepesi, nawe unalifanya gumu kuwa jepesi ukitaka.

34.Dua ya kuomba unapotokewa na jambo usiloliridhia au unaposhindwa kufanya jambo Amesema Mtume (s.a.w) (katika Sahihi Bukhari): "Muumini mwenye nguvu (qawiyyu) ni bora na anapendeza zaidi kwa Allah (s.w) kuliko muumini dhaifu, na wote wanakheri. Fanya pupa kwa kile kitakacho kunufaisha na taka msaada wa Allah wala usichoke, na kikikupata kitu chochote kibaya basi usiseme lau kama ningelifanya kadha na kadhaa yasingenitokea haya, lakini sema: "Qaddarallahu wamaa shaa-af-a'la. “Amepanga Allah na analolitaka anafanya." Hakika Allah analaumu mwenye kukata tamaa, lakini usivunjike moyo, na ukishindwa na jambo kabisa sema: "Has-biya llahu wani-i'mal-wakiilu" "Allah ananitosheleza, Naye ni mbora wa kutegemewa."

35.Dua ya Kumuombea mgonjwa wakati wa kumtembelea “Laa ba-asa twahuurun in-shaa-allahu." “Hakuna neno, (ugonjwa) ni kusafishwa na dhambi anapopenda Allah." (Al-Bukhari) Anasema Mtume wa Allah: "Hapana yeyote Muislamu anayemtembelea mgonjwa ambaye wakati wake wa kufa bado haujafika na anamuombea mara saba. “As-alullaah l-a'dhiima rabal-a'r-shi l-a'dhiimi an-yash-fiyaka. “Namuomba Allah Mtukufu, Mola wa arshi tukufu akuponyeshe." Isipokuwa Allah humponyesha mgonjwa huyo." (At-Tirmidh na Abu Daud)

36.Dua anayoomba mgonjwa aliyekata tamaa na kupona “Allahumma gh-fir-liy war-hamniy wa-alhiq-niy birrafiiq il-a-a'laa" 481 Ee! Allah, nisamehe na unirehemu na unikutanishe na waja walio katika daraja za juu".

37.Dua ya kuomba mvua “Allahumma asqinaa ghaythan mughiithan mariian mariia'a, naafia'an ghayradhwaarrin, a'ajilanghayra aajilin. Ee! Allah tunyesheleze mvua yenye kuokoa, nyingi, yenye kustawisha, yenye manufaa isiyodhuru.

38.Dua ya kuleta wakati unapovuma upepo Allahumma inniy as-aluka khayrahaa wa-au'udhubika minsharrihaa. Ee, Allah! Ninakuomba unipe kheri ya upepo huu na uniepushe na shari yake.

39.Dua ya kuleta wakati mvua inanyesha “Allahumma Swayyiban naafia'n “Ee Allah ijaalie iwe mvua yenye manufaa."

40.Dua ya kuleta baada ya mvua kunyesha Mutwir-haa bifadh-lillahi warah-matihi. Tumepata mvua kwa msaada na rehema ya Allah."


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1246

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kuzuru makaburi na dua unazotakiwa kuzisoma ukiwa makaburini.

Posti hii inakwenda kukufundisha maneno unayotakiwa kuyasema unapozuru makaburi.

Soma Zaidi...
DUA 94 - 114

DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 94.

Soma Zaidi...
NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU

Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
SWALA YA MTUME (s.a.w)

SWALA YA MTUME Kumswalia Mtume (s.

Soma Zaidi...
Vyanzo vitano vya elimu zote duniani: Chanzo cha Elimu ni Allah (s.w)

Kama tunavyojifunza katika surat ‘Alaq (96:4-5), chanzo cha elimu au mkufunzi wa binadamu ni Allah (s.

Soma Zaidi...
Maana ya sunnah (suna) na maana ya hadithi

Post hii itakufundisha maana ya neno sunnah katika Uislamu. Pia utajifunza maana ya neno hadithi katika uislamu

Soma Zaidi...
Nafasi ya Elimu na wenye elimu katika Uislamu

Nafasi ya elimu na mwenye elimu katika uislamu inaonkana katika maeneo yafuatayo: Kwanza, Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.

Soma Zaidi...