32.
32.Dua ya Kulipa Deni "Allahummak-finiy bihalaalika'an haraamika wa-agh-niy bifadhw-lika 'amman siwaaka." Ee Allah! Nitosheleze na halali yako na Uniepushe na haramu yako, na Unitosheleze kwa fadhila zako nisiwahitaji wengine asiye wewe.
33.Dua anayoleta yule aliyefikwa na jambo gumu “Allahumma laasah-la illaa maaja-'al-tahu sah-laa, wa anta taj-'alul-haz-na idhaashi-ita sah-laa. Ee Allah hakuna jepesi ila ulilolifanya jepesi, nawe unalifanya gumu kuwa jepesi ukitaka.
34.Dua ya kuomba unapotokewa na jambo usiloliridhia au unaposhindwa kufanya jambo Amesema Mtume (s.a.w) (katika Sahihi Bukhari): "Muumini mwenye nguvu (qawiyyu) ni bora na anapendeza zaidi kwa Allah (s.w) kuliko muumini dhaifu, na wote wanakheri. Fanya pupa kwa kile kitakacho kunufaisha na taka msaada wa Allah wala usichoke, na kikikupata kitu chochote kibaya basi usiseme lau kama ningelifanya kadha na kadhaa yasingenitokea haya, lakini sema: "Qaddarallahu wamaa shaa-af-a'la. “Amepanga Allah na analolitaka anafanya." Hakika Allah analaumu mwenye kukata tamaa, lakini usivunjike moyo, na ukishindwa na jambo kabisa sema: "Has-biya llahu wani-i'mal-wakiilu" "Allah ananitosheleza, Naye ni mbora wa kutegemewa."
35.Dua ya Kumuombea mgonjwa wakati wa kumtembelea “Laa ba-asa twahuurun in-shaa-allahu." “Hakuna neno, (ugonjwa) ni kusafishwa na dhambi anapopenda Allah." (Al-Bukhari) Anasema Mtume wa Allah: "Hapana yeyote Muislamu anayemtembelea mgonjwa ambaye wakati wake wa kufa bado haujafika na anamuombea mara saba. “As-alullaah l-a'dhiima rabal-a'r-shi l-a'dhiimi an-yash-fiyaka. “Namuomba Allah Mtukufu, Mola wa arshi tukufu akuponyeshe." Isipokuwa Allah humponyesha mgonjwa huyo." (At-Tirmidh na Abu Daud)
36.Dua anayoomba mgonjwa aliyekata tamaa na kupona “Allahumma gh-fir-liy war-hamniy wa-alhiq-niy birrafiiq il-a-a'laa" 481 Ee! Allah, nisamehe na unirehemu na unikutanishe na waja walio katika daraja za juu".
37.Dua ya kuomba mvua “Allahumma asqinaa ghaythan mughiithan mariian mariia'a, naafia'an ghayradhwaarrin, a'ajilanghayra aajilin. Ee! Allah tunyesheleze mvua yenye kuokoa, nyingi, yenye kustawisha, yenye manufaa isiyodhuru.
38.Dua ya kuleta wakati unapovuma upepo Allahumma inniy as-aluka khayrahaa wa-au'udhubika minsharrihaa. Ee, Allah! Ninakuomba unipe kheri ya upepo huu na uniepushe na shari yake.
39.Dua ya kuleta wakati mvua inanyesha “Allahumma Swayyiban naafia'n “Ee Allah ijaalie iwe mvua yenye manufaa."
40.Dua ya kuleta baada ya mvua kunyesha Mutwir-haa bifadh-lillahi warah-matihi. Tumepata mvua kwa msaada na rehema ya Allah."
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 650
Sponsored links
👉1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2
Madrasa kiganjani
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Simulizi za Hadithi Audio
👉5
Kitau cha Fiqh
👉6
Kitabu cha Afya
Adabu ya kukaa na kula katika nyumba za watu
"Si vibaya kwa kipofu, wala si vibaya kwa kiguru, wala si vibaya kwa mgonjwa, wala kwenu, kama mkila katika nyumba zenu, au nyumba za baba zenu, au nyumba za mama zenu, au nyumba za ndugu zenu, au nyumba za dada zenu, au nyumba za ami zenu, au nyumba za s Soma Zaidi...
KATU USITAMANI MAUTI (KIFO) YAANI KUFA, HATA UKIWA NA MARADHI AMA UKIWA MCHAMUNGU UKIWA NI MUOVU MTENDA MADHAMBI MAKUBWA NA MADOGO
Soma Zaidi...
DUA ZA WAKATI WA HASIRA
DUA ZA WAKATI UNAPOKUWA NA HASIRA. Soma Zaidi...
hadithi ya 8
عَنْ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "أُمِرْتُ أَنْ أُقَاتِلَ النَّاسَ حَتَّى ?... Soma Zaidi...
Adhkari unazoweza kuomba kila siku
Hapa nitakuletea baadhi tu ya adhkari ambazo ni muhimu kwa muislamu Soma Zaidi...
Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 3: Nguzo za uislamu
Katika hadithi hii utakwenda kujifunza nguzo za uislamu Soma Zaidi...
SWALA YA MTUME (s.a.w)
SWALA YA MTUME Kumswalia Mtume (s. Soma Zaidi...
Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote
Soma Zaidi...
Masharti ya kukubaliwa kwa dua
Post hii itakwenda kukugundisha masharti yanayofungamana na kukubaliwa kwa dua. Soma Zaidi...
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA
SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA. Soma Zaidi...