DUA 32 - 40

DUA 32 - 40

32.

DUA 32 - 40


32.Dua ya Kulipa Deni "Allahummak-finiy bihalaalika'an haraamika wa-agh-niy bifadhw-lika 'amman siwaaka." Ee Allah! Nitosheleze na halali yako na Uniepushe na haramu yako, na Unitosheleze kwa fadhila zako nisiwahitaji wengine asiye wewe.

33.Dua anayoleta yule aliyefikwa na jambo gumu “Allahumma laasah-la illaa maaja-'al-tahu sah-laa, wa anta taj-'alul-haz-na idhaashi-ita sah-laa. Ee Allah hakuna jepesi ila ulilolifanya jepesi, nawe unalifanya gumu kuwa jepesi ukitaka.

34.Dua ya kuomba unapotokewa na jambo usiloliridhia au unaposhindwa kufanya jambo Amesema Mtume (s.a.w) (katika Sahihi Bukhari): "Muumini mwenye nguvu (qawiyyu) ni bora na anapendeza zaidi kwa Allah (s.w) kuliko muumini dhaifu, na wote wanakheri. Fanya pupa kwa kile kitakacho kunufaisha na taka msaada wa Allah wala usichoke, na kikikupata kitu chochote kibaya basi usiseme lau kama ningelifanya kadha na kadhaa yasingenitokea haya, lakini sema: "Qaddarallahu wamaa shaa-af-a'la. “Amepanga Allah na analolitaka anafanya." Hakika Allah analaumu mwenye kukata tamaa, lakini usivunjike moyo, na ukishindwa na jambo kabisa sema: "Has-biya llahu wani-i'mal-wakiilu" "Allah ananitosheleza, Naye ni mbora wa kutegemewa."

35.Dua ya Kumuombea mgonjwa wakati wa kumtembelea “Laa ba-asa twahuurun in-shaa-allahu." “Hakuna neno, (ugonjwa) ni kusafishwa na dhambi anapopenda Allah." (Al-Bukhari) Anasema Mtume wa Allah: "Hapana yeyote Muislamu anayemtembelea mgonjwa ambaye wakati wake wa kufa bado haujafika na anamuombea mara saba. “As-alullaah l-a'dhiima rabal-a'r-shi l-a'dhiimi an-yash-fiyaka. “Namuomba Allah Mtukufu, Mola wa arshi tukufu akuponyeshe." Isipokuwa Allah humponyesha mgonjwa huyo." (At-Tirmidh na Abu Daud)

36.Dua anayoomba mgonjwa aliyekata tamaa na kupona “Allahumma gh-fir-liy war-hamniy wa-alhiq-niy birrafiiq il-a-a'laa" 481 Ee! Allah, nisamehe na unirehemu na unikutanishe na waja walio katika daraja za juu".

37.Dua ya kuomba mvua “Allahumma asqinaa ghaythan mughiithan mariian mariia'a, naafia'an ghayradhwaarrin, a'ajilanghayra aajilin. Ee! Allah tunyesheleze mvua yenye kuokoa, nyingi, yenye kustawisha, yenye manufaa isiyodhuru.

38.Dua ya kuleta wakati unapovuma upepo Allahumma inniy as-aluka khayrahaa wa-au'udhubika minsharrihaa. Ee, Allah! Ninakuomba unipe kheri ya upepo huu na uniepushe na shari yake.

39.Dua ya kuleta wakati mvua inanyesha “Allahumma Swayyiban naafia'n “Ee Allah ijaalie iwe mvua yenye manufaa."

40.Dua ya kuleta baada ya mvua kunyesha Mutwir-haa bifadh-lillahi warah-matihi. Tumepata mvua kwa msaada na rehema ya Allah."


                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 203


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Dua za wakati wa shida na taabu
Hizi ni Dua ambazo unatakiwa uziombe wakati wa shida na taabu Soma Zaidi...

DUA 113 - 126
DUA ZA WAKATI WA SHIDA Dua ya wakati wa taabu 'LAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-'ADHIMUL-HALIIMU. Soma Zaidi...

kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii
11. Soma Zaidi...

MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA
MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA. Soma Zaidi...

Masomo ya Dua na Faida zake Dua
Soma Dua mbalimbali hapa, Soma Zaidi...

SHUGHULI ZA KILA SIKU
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Dua za kuwaombea wazazi
Kwenye Quran kuna duaambazo Allah ametufundisha tuziombe kwa ajili ya wazazi, familia na kwa ajili yetu wenyewe. Soma Zaidi...

Hadithi Ya 39: Allaah Amewasamehe Umma Wake Kukosea Na Kusahau Kwa Ajili Yake ( Mtume ' ' ' ' )
Soma Zaidi...

Hadithi ya pili: sifa za muumini wa kweli
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Jinsi ya kutoa salamu katika uislamu
MAkala hii itakwenda kukufundisha jinsi ya kutoa salamu kwenye uislamu Soma Zaidi...

MAANA NA FADHILA ZA KUOMBA DUA
DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani. Soma Zaidi...

darasa la dua
Soma Zaidi...