DUA 32 - 40

32.

DUA 32 - 40


32.Dua ya Kulipa Deni "Allahummak-finiy bihalaalika'an haraamika wa-agh-niy bifadhw-lika 'amman siwaaka." Ee Allah! Nitosheleze na halali yako na Uniepushe na haramu yako, na Unitosheleze kwa fadhila zako nisiwahitaji wengine asiye wewe.

33.Dua anayoleta yule aliyefikwa na jambo gumu “Allahumma laasah-la illaa maaja-'al-tahu sah-laa, wa anta taj-'alul-haz-na idhaashi-ita sah-laa. Ee Allah hakuna jepesi ila ulilolifanya jepesi, nawe unalifanya gumu kuwa jepesi ukitaka.

34.Dua ya kuomba unapotokewa na jambo usiloliridhia au unaposhindwa kufanya jambo Amesema Mtume (s.a.w) (katika Sahihi Bukhari): "Muumini mwenye nguvu (qawiyyu) ni bora na anapendeza zaidi kwa Allah (s.w) kuliko muumini dhaifu, na wote wanakheri. Fanya pupa kwa kile kitakacho kunufaisha na taka msaada wa Allah wala usichoke, na kikikupata kitu chochote kibaya basi usiseme lau kama ningelifanya kadha na kadhaa yasingenitokea haya, lakini sema: "Qaddarallahu wamaa shaa-af-a'la. “Amepanga Allah na analolitaka anafanya." Hakika Allah analaumu mwenye kukata tamaa, lakini usivunjike moyo, na ukishindwa na jambo kabisa sema: "Has-biya llahu wani-i'mal-wakiilu" "Allah ananitosheleza, Naye ni mbora wa kutegemewa."

35.Dua ya Kumuombea mgonjwa wakati wa kumtembelea “Laa ba-asa twahuurun in-shaa-allahu." “Hakuna neno, (ugonjwa) ni kusafishwa na dhambi anapopenda Allah." (Al-Bukhari) Anasema Mtume wa Allah: "Hapana yeyote Muislamu anayemtembelea mgonjwa ambaye wakati wake wa kufa bado haujafika na anamuombea mara saba. “As-alullaah l-a'dhiima rabal-a'r-shi l-a'dhiimi an-yash-fiyaka. “Namuomba Allah Mtukufu, Mola wa arshi tukufu akuponyeshe." Isipokuwa Allah humponyesha mgonjwa huyo." (At-Tirmidh na Abu Daud)

36.Dua anayoomba mgonjwa aliyekata tamaa na kupona “Allahumma gh-fir-liy war-hamniy wa-alhiq-niy birrafiiq il-a-a'laa" 481 Ee! Allah, nisamehe na unirehemu na unikutanishe na waja walio katika daraja za juu".

37.Dua ya kuomba mvua “Allahumma asqinaa ghaythan mughiithan mariian mariia'a, naafia'an ghayradhwaarrin, a'ajilanghayra aajilin. Ee! Allah tunyesheleze mvua yenye kuokoa, nyingi, yenye kustawisha, yenye manufaa isiyodhuru.

38.Dua ya kuleta wakati unapovuma upepo Allahumma inniy as-aluka khayrahaa wa-au'udhubika minsharrihaa. Ee, Allah! Ninakuomba unipe kheri ya upepo huu na uniepushe na shari yake.

39.Dua ya kuleta wakati mvua inanyesha “Allahumma Swayyiban naafia'n “Ee Allah ijaalie iwe mvua yenye manufaa."

40.Dua ya kuleta baada ya mvua kunyesha Mutwir-haa bifadh-lillahi warah-matihi. Tumepata mvua kwa msaada na rehema ya Allah."


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1130

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU.

Soma Zaidi...
MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA

MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA.

Soma Zaidi...
NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU

Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Hadithi ya pili: sifa za muumini wa kweli

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Dua sehemu ya 04

Soma dua mbalimbali za kila siku ambazo unatakiwa uzijuwe. Dua 120 ambazo muislamu anatakiwa kuzijua

Soma Zaidi...
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA

SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA.

Soma Zaidi...
Darsa za Dua

Download kitabu hiki na upate kusoma zaidi ya dua 120, pamoja na darsa mbalimbali za dini ya kiislamu.

Soma Zaidi...
Ijuwe swala ya Mtume na fadhila zake na jinsi ya kumswalia Mtume.

Post hii itakufundisha jinsi ya kumswalia mtume, pamoja na kuzijuwa fadhila unazopata kwa kumswalia Mtume

Soma Zaidi...